Tuesday 28 April 2015

MPYA:"AJIRA ZA WALIMU ZAONDOLEWA KWA MUDA,NI BAADA YA TAMISEMI KUAJIRI WALIMU WALIOAJIRIWA TAYARI 2013"

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Tokeo la picha la NGAO YA TANZANIA
OFISI YA WAZIRI MKUU
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (OWM - TAMISEMI)


TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUONDOLEWA KWA MUDA KATIKA TOVUTI ORODHA YA WALIMU WA MASOMO YA SANAA NA BIASHARA WA SHULE SEKONDARI -AJIRA MPYA MWAKA 2014/15
Orodha ya wahitimu wa shahada na stashahada waliopangiwa katika halmashauri mbalimbali inafanyiwa marekebisho baada ya kubainika kuwa uongozi wa Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa (Sebastian Kolowa University College-SEKUCO) cha Lushoto uliwasilisha orodha ya wahitimu wapatao 491 wa mwaka 2013 ambao walishaajiriwa badala ya wahitimu wa mwaka 2014.
Kutokana na sababu hiyo, orodha tajwa imesitishwa kwa muda ili kufanyiwa marekebisho na kuwekwa orodha sahihi itakayojumuisha wahitimu wa SEKUCO wa mwaka 2014.
Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na kasoro hiyo.
Imetolewa na
OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI
ZA MITAA
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger