Thursday 22 August 2024

MABORESHO HUDUMA YA MAJI GOBA

...

 


Kazi ya kuweka toleo la bomba la inchi 3 kutoka bomba la usambazaji maji la inchi 4 inaendelea kutekelezwa na mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) katika eneo la Simba Oil

Kazi hiyo inahusisha utolewaji wa maji katika bomba la inchi 4 kuelekea bomba la usambazaji maji la inchi 6 pamoja na ulazaji wa bomba la inchi 3 umbali wa mita 60 ili kuongeza msukumo maji katika eneo ilo.

Kukamilika kwa kazi hiyo itasaidia kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wakazi wa maeneo ya Simba Oil, Chasimba, Minji, River View, Goba Zahanati, Shimbi Kati na Mwamuyamu
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger