Thursday 6 June 2024

KIKOSI KAZI KUUNDWA KUDHIBITI UTOROSHAJI WA MADINI MKOANI SONGWE

...


 Na Mwanahamisi Msangi, Songwe

TUME ya Madini Mkoa wa Songwe  imeunda kikosi kazi maalum cha kupambana na kudhibiti utoroshaji  wa madini na kusababisha serikali kukosa mapato.

Hayo yamesemwa na Afisa Madini Mkazi - Songwe, Chone Malembo wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwatembelea wachimbaji wadogo katika eneo la Mbangala lililopo mkoani humo.

“Kwa sasa kuna mawasiliano ambayo yanaendelea tunataka kutengeneza kikosi kazi madini Mkoa ambacho kazi yake itakuwa ni kufanya uchunguzi  na kutoa taarifa kuhusu utoroshaji madini mahali husika ili kuchukua hatua stahiki lengo ni kudhibiti utoroshaji ambao husababisha Serikali kukosa mapato,”amesema Chone.

Katika hatua nyingine, Afisa huyo amesema wamegundua madini mapya aina ya Solidite ambayo yanapatikana Wilaya ya Momba.





Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger