Friday 21 June 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 21, 2024

   
Share:

Thursday 20 June 2024

DC SIIMA : UJIO WA MADAKTARI BINGWA KUONDOA CHANGAMOTO KWA WANANCHI KAGERA

Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh. Erasto Siima akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera  katika hospitali ya Wilaya ya Bukoba Nshambya katika uzinduzi wa kambi ya madaktari bingwa. 

Na Mbuke Shilagi Kagera. 

Mkuu wa wilaya ya Bukoba amesema kuwa Ujio wa madaktari bingwa katika Mkoa wa Kagera unaenda kusaidia kuondoa changamoto kwa wananchi kufuata huduma za kibingwa nje ya mkoa wa Kagera na kupunguza umbali mrefu pamoja na gharama.

Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh. Erasto Siima  amesema hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera  June 17,2024 katika hospitali ya Wilaya ya Bukoba Nshambya katika uzinduzi wa kambi ya madaktari bingwa wa magonjwa ya usingizi, mama na mtoto, upasuaji mkubwa pamoja na magonjwa ya ndani. 

Ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuboresha zaidi huduma za afya kwa maslahi ya watanzania huku akisema asilimia 85.2 imehudumia jamii ya mama na mtoto kwa mwaka 2024.

Hata hivyo ameongeza kuwa huduma za afya ya mama na mtoto imezidi kuimarika na kuongezeka zaidi na kuondoa changamoto iliyokuwepo kwani huduma hii itaondoa changamoto ya wananchi kwenda nje ya mkoa.

"Nipende kuishukuru Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na nimshukuru Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan japokuwa na kazi na ratiba nyingine alizonazo lakini suala zima la afya zetu halipo nyuma katika majukumu yake ya kila siku kwamaana madakitari wote waliopo hapa leo ni kwamatakwa yake",amesema Dc Siima.

Kwa upande wake afisa idara ya afya ya uzazi mama na mtoto bi Grace malick ambae ameongozana na madaktari bingwa kutoka wizara ya afya nchini amesema lengo la kambi hiyo ni kuhakikisha huduma za kibingwa zinawafikia wananchi wote na kupata huduma hizo kwa bei nafuu na kupunguza umbali kwa wananchi wanaotoka maeneo ya mbali.

Ameongeza kuwa Huduma hiyo ya mama Samia Mentorship inatekelezwa katika mikoa yote 26 na sasa mikoa 23 tayari ishapata huduma hii  na halmashauri  139 kati ya halmashauri 184 na  ipo katika mkoa wa Kagera tayari kwa huduma hiyo katika halmashauri zote 8.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba Mh. Jakob Nkwera amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia kwa kusogeza huduma ya kibingwa katika ngazi ya chini ili kuwafikia watu wote bila ya kuingia gharama kubwa. 

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba ameshukuru kwa ujio wa madaktari hao na kuwataka wananchi ndani ya Manispaa ya Bukoba kuhakikisha wanafika katika kata ya nshambya na hospitali ya Nshambya ili kuweza kujipatia huduma hizo za kibingwa ambapo yameanza jumatatu June 17,2024 mpaka Ijumaa June 21,2024.
Share:

TVLA YAANZA MIKUTANO NA VYAMA VYA MIFUGO KUPATA VYAKULA BORA

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari nchini (TVLA) Dkt. Stella Bitanyi, akizungumza wakati wa kikao na wazalishaji wa vyakula vya mifugo nchini ili kuzalisha chakula bora na chenye tija, kikao kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Na. Edward Kondela - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Serikali imeanza kufanya kazi kwa karibu na vyama vya mifugo nchini kupitia vikao mbalimbali ili kuhakikisha usalama na ubora wa vyakula vya mifugo.

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Dkt. Stella Bitanyi amebainisha hayo ofisini kwake jijini Dar es Salaam, mara baada ya kufanya kikao na wazalishaji wa vyakula vya mifugo nchini ili kuzalisha chakula bora na chenye tija.

Dkt. Bitanyi amesema kuwa serikali itahakikisha inasimamia suala la ubora na wakala hiyo itakuwa na mikutano ya mara kwa mara pamoja na kutoa elimu na kutembelea maeneo yanayotengenezwa vyakula vya mifugo na kusimamia ubora.

“Tumeanza kufanya kazi kwa karibu na vyama vya mifugo nchini na mkutano wa leo tumeanza na Chama cha Wazalishaji wa Vyakula vya Mifugo nchini (TAFMA) pamoja na vyama vingine vya ndege wa wafugwao vikao hivi vinalenga kusimamia usalama na ubora wa mifugo, maana wafugaji wadogo nchini wanategemea wazalishaji wa vyakula vya mifugo kuzalisha vyakula bora ili kuongeza tija kwa wafugaji na wapate matokeo mazuri ya mifugo yao.” Amesema Dkt. Bitanyi

Kwa upande wao baadhi ya wadau waliohudhuria kikao hicho, wamepata nafasi ya kutoa maoni yao pamoja na kutaka ufafanuzi wa baadhi ya majukumu ya TVLA na kuomba uwepo wa vikao vya mara kwa mara ili kuwakumbusha wazalishaji wa vyakula vya mifugo kuzalisha vyakula bora.

Wamesema wananufaika na elimu ambayo inatolewa na TVLA pamoja na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa vyakula vya mifugo nchini ili kuhakikisha wafugaji wanapata vyakula bora na hatimaye kufikia malengo ya ufufgaji wao.

TVLA inatarajia kuendelea kutoka elimu na kufanya ukaguzi wa rasilimali na vyakula vya mifugo katika kanda mbalimbali za wakala hiyo pamoja na kusimamia sheria ili wafugaji ili waweze kufuga kwa tija na kupata matokeo bora kupitia ufugaji.
Baadhi ya wadau kutoka vyama vya mifugo nchini wakiwa kwenye kikao kilichoitishwa na Wakala ya Maabara ya Veterinari nchini (TVLA) kujadili mustakbali wa kupata vyakula bora vya mifugo ili viwe na tija kwa wafugaji. Kikao hicho kimefanyika makao makuu ya TVLA jijini Dar es Salaam.
Share:

WANA-GDSS WAJENGEWA UWEZO JUU YA ULINZI WA MTOTO KISHERIA, USAWA WA KIJINSIA NA NAMNA YA KURIPOTI TAARIFA ZA UVUNJWAJI WA HAKI ZA MTOTO


Na mwandishi wetu, Dar es Salaam

Imeelezwa kuwa, Serikali kuu hutoa majukumu kwa serikali za mitaa katika kulinda na kutetea maslahi ya mtoto ili kuhakikisha kuwa analelewa katika mazingira stahiki na kwa maadili ya jamii.

Vilevile maafisa ustawi wa jamii wana wajibu wa kushirikiana na serikali za mitaa kutoa ushauri na elimu kwa wazazi, walezi, ndugu na jamii kwa ujumla juu ya ustawi wa mtoto.

Hayo yamesemwa kwa nyakati Juni 19, 2024 jijini Dar es Salaam na Nasra Mrisho pamoja Wenseslaus Kidakule ambao ni wawazesheaji kutoka Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), kwenye Semina za Jinsia na Maendeleo iliyofanyika katika ofisi za TGNP Mabibo ambapo mada kuu kwa hii leo ilikuwa ikiangazia kauli mbiu ya Siku ya Mtoto wa Afrika mwaka huu (2024) inayosema Elimu Jumuishi kwa Watoto, Izingatie Maarifa, Maadili na Stadi za Kazi.

Wawili hao, wametilia mkazo suala la ulinzi wa kisheria wa makazi ya mtoto ambapo wamesema, watoto wana haki zote za kufurahia na kufaidika na mali za wazazi wake pasi na kumfanyia mtoto ukatili au unyama wa aina yoyote ile utakaoathiri akili au maumbile yake.

Kuhusu suala la usawa wa kijinsia, wawezeshaji hao wameeleza kuwa, sheria inakataa ubaguzi wa aina yoyote ile kwa mtoto iwe ni rangi, dini, ukimbizi, ulemavu au ubaguzi mwingine wowote na kwamba watoto wote wanapaswa kuchukuliwa kwa mizani sawa.

Vilevile wameikumbusha jamii kuwa, ina wajibu wa moja kwa moja wa kutoa taarifa kwa viongozi wa serikali za mitaa juu ya uvunjwaji wa sheria kuhusu watoto utakaofanywa na mzazi, mlezi, ndugu au mtu yeyote yule.

Akichangia mada katika semina hiyo, mwanaisaikolojia Sylvia Sostenes amewasihi na kuwakumbusha wazazi kukaa na watoto wao na kuwaeleza ni kwa lengo gani wanawapeleka watoto wao shule, kitu ambacho ni kinyume na sasa akibaini watoto wengi wanakwenda shule kwa kuwa kuna utamaduni wa kwenda shule kusoma au mtoto kuona watoto wa jirani wakienda shule lakini si kuwa na utambuzi wa lengo husika.

"Kama tukikaa nyumbani na kuongea na watoto wetu na kuwaeleza kuwa ni kwa sababu gani wako shule itasaidia sana na pia itawafanya watoto wenyewe waweke bidii kutoka mioyoni mwao katika masomo yao" alisema Sylvia

Kando na hilo, amewataka wanaharakati wa jinsia kuendelea kupaza sauti na kupinga kila aina ya unyanyasaji ambapo kwa mazingira mjini wanafunzi wengi wananyanyaswa katika vyombo vya usafiri.

"Tukatae hilo na kupaza sauti tukiwa ndani ya vyombo vya usafiri na ikiwezekana tukutane na makondakta wa vyombo vya usafiri ili kuongea nao na kuwapa elimu, watoto wanafanyiwa unyanyasaji lakini watu wazima wapo ndani ya gari na wako kimya" amehoji Sylvia

Pia amezitaja baadhi ya changamoto ambazo zinakwamisha jitihada za watoto kupata elimu hususan maeneo ya pembezoni mwa miji na vijijini kuwa ni pamoja na uwezo mdogo kukidhi mahitaji ya msingi ya mwanafunzi.

Kufuatia hilo ameiomba serikali, kuweka wazi kiwango cha ruzuku inayotolewa kwa kila mwanafunzi ili iweze kutumika katika mahitaji ya kimsingi kama ununuzi wa sare za shule.

Kenedy Angeliter, ambaye ni mshiriki katika semina hiyo, ametoa rai kwa serikali kuhakika elimu inayotolewa na kuhakikisha inakuwa bora na si bora elimu pamoja na kusimamia sera ya elimu iliyopo ili kuleta mtazamo mpya wa fikra na kuachana na mtazamo wa awali wa kusoma kwa lengo la kujipatia ajira pekee.

Angeliter ameongeza kuwa, imekuwa ni utamaduni kwa sasa kwa wahitimu wa elimu mbalimbali kutembea na bahasha zenye wasifu wao kwa lengo la kutafuta fursa za ajira.

"Inabidi tubadilishe mitazamo ya wanafunzi wetu wafahamu kabisa kwamba pindi wanapohitinu wanapaswa kwenda kujiajiri"

Semina za Jinsia na Maendeleo hufanyika kila siku ya Jumatano na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali ikiwemo, wanahabari, wanasaiokolojia, wanaharakati na wanajamii kwa ujumla ambapo kwa pamoja huadili kuhusu mada mbalimbali zenye mrengo wa kijinsia na maendeleo.
Share:

Wednesday 19 June 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JUNI 20, 2024

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger