Tuesday 28 February 2023

MANJU MAARUFU JAMES MAKUNGU SOMBI AFARIKI DUNIA... KUZIKWA JUMAMOSI KWA NGOMA

...

James Makungu Sombi akitoa burudani enzi za uhai wake
James Makungu Sombi enzi za uhai wake akizungumza na Malunde 1 blog nyumbani kwake Kisesa Mwanza
*****

Manju maarufu na Mtaalamu wa Masuala ya Utamaduni wa Kabila la Kisukuma James Sombi (89) amefariki dunia.

James Sombi miongoni mwa waanzilishi wa Makumbusho ya Kabila la Wasukuma Bujora Mwanza ambaye enzi za uhai wake alikuwa mcheza ngoma maarufu ya Bugobogobo na Zeze aliyetangaza utamaduni wa Kabila la Wasukuma ndani na nje ya Tanzania.

Kwa mujibu wa mtoto wake aitwaye Veronica aliyezungumza na Malunde 1 blog, amesema Mzee James Sombi amefariki dunia Jumatatu Februari 27,2023 saa nane mchana baada ya kuanguka.

"Mzee ametutoka baada ya kuanguka ghafla akiwa nyumbani kwake Kisesa Mwanza. Alikuwa anasumbuliwa na tatizo kwenye mishipa ya moyo na alikuwa anasema kifua kinauma na ghafla mchana akaanguka", ameeleza Veronica.

 "Mazishi yatafanyika siku ya Jumamosi Machi 4,2023 katika kijiji cha Mwamanga Magu kama alivyotaka yeye kabla ya kifo chake na kwa kuwa enzi za uhai wake alikuwa mcheza ngoma pia atachezewa ngoma siku ya mazishi yake",amesema Veronica.

James Makungu Sombi alizaliwa mwaka 1934 katika kijiji cha Mwamanga wilayani Magu mkoani Mwanza.
James Makungu Sombi akitoa burudani enzi za uhai wake
\


Soma pia

JAMES SOMBI : KUFANYA SANA MAPENZI KUNAPUNGUZA SIKU ZA KUISHI

MZEE SOMBI : VIJANA WANAOGOPA KUOA KWA SABABU HAWANA KAZI....HAWATAKI USUMBUFU

BABU ATOA DAWA YA KUKOMESHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME...VIBAMIA

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger