Sunday 26 February 2023

ASIYEJULIKANA AVAMIA KANISA KATOLIKI GEITA, AHARIBU VITU VITAKATIFU

...

Sehemu ya uharibifu uliofanywa

NA ROSE MWEKO, GEITA
MTU asiyefahamika amevamia na kuingia ndani ya kanisa Katoliki jimbo la Geita na kufanya uharibifu katika altare na sakrestia na kuvunja tabernakulo huku akimwaga ekaristi takatifu na kuchana kitabu kitakatifu Biblia huku akiharibu mfumo wa camera za ulinzi.

Taarifa iliyotolewa na Askofu wa Jimbo katoliki la Geita kwa njia ya simu Flavian Matindi Kasalla amesema mtu huyo alivunja kioo cha mlangoni na kuharibu madhabahu takatifu huku akiharibu sehemu mbalimbali za ibada na kuharibu vitabu vitakatifu.
“mpaka sasa hatujajua alikotokea na wala hatujui aliingia saa ngapi japo ilikua ni usiku wa kuamkia siku ya jumapili, kanisa letu linalindwa na kampuni ya ulinzi ila mpaka sasa ni kitendawili kuwa mlinzi alikuwa wapi, mtu aliyefanya tukio hilo amekamatwa na ameshafikishwa katika vyombo vya usalama pamoja na mlinzi aliyekuwa zamu siku hiyo” alisema Askofu Kasalla.
Watu wawili wanashilikiwa na jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi akithibithisha kukamatwa kwa watu hao Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita ACP Berthaneema Mlay alisema jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi zaidi ili kubaini nani kamtuma na sababu za kufanya uharibifu huo.
“mtu huyo anaonekana alikuwa mlinzi na ni mtu ambaye amekuwa akihudumu katika kanisani haswa huko alikotoka Bukoba hivyo jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi na itakapobainika tutatoa taarifa zaidi kwani mpaka sasa kuna mambo tunayafuatilia tatutayazungumza ili kutovuruga upelelezi.

Chanzo - The Profiletv blog

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger