Tuesday 3 January 2023

ANAYEDAIWA KUWA MWIZI ANUSURIKA KUUAWA BAADA YA KUDAKWA NA BATA TAMBUKARELI SHINYANGA MJINI

...
Kijana aliyejulikana kwa jina Musa amenusurika kuuawa kwa kupigwa na wananchi wenye hasira kali katika eneo la Tambukateli kata ya Ndembezi Mjini Shinyanga baada ya kukamatwa na bata anayedaiwa kumuiba katika mtaa huo huku mwenyewe akikiri kufanya matukio ya wizi katika eneo hilo.


Tukio hilo limetokea majira ya sita mchana leo Jumanne Januari 2,2023 ambapo wananchi wenye hasira wamemshambulia kijana huyo kabla ya askari polisi kufika eneo la tukio na kumuokoa kijana huyo.

Wakati hayo yanajiri mkazi wa eneo hilo ambaye hatukufanikiwa kupata jina lake naye anaugulia maumivu baada ya kupewa kichapo wakati akizuiwa asimpige mtuhumiwa huyo wa wizi.


Mtuhumiwa wa wizi akiwa na bata pembeni


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger