Sunday 29 September 2019

Makonda Awaomba Mawaziri Wamvumilie....Awataka Wasitishe Ziara Zao Dar es Salaam Kwa Muda

Mkuu  wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewaomba Mawaziri wanaotaka kufanya ziara za miradi katika mkoa huo, kusitisha kwa muda ili kupisha utekelezaji wa maagizo ya Rais John Magufuli aliyoyatoa.
Amesema mwezi huu na Octoba watamalizia pia utekelezaji wa mikakati waliyopeana na kuanzia hapo mawaziri wataweza kufika na kuendelea na ziara zao za kikazi.

Makonda ameyasema hayo ni leo wakati akikagua mradi wa ujenzi machinjio  ya kisasa ya Vingunguti ambao ujenzi wake umefika asilimia 25.

"Nawaomba mawaziri ambao wanataka kufanya ziara katika mkoa huu, tutekeleze miradi ambayo tumepewa maelekezo na Rais Magufuli alipofanya ziara na baada ya hapo waendelee kama walivyopanga," Makonda alisema.

Kuhusu ujenzi wa machinjio hayo alilipongeza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa kutekeleza mradi huo kwa haraka.

Makonda alimuagiza Meya wa Manispaa ya Ilala, Omary Kumbilamoto, kukaa na baraza la madiwani kwa ajili ya kutenga fedha za kujenga barabara ya kuelekea katika machinjia hayo yenye urefu wa Kilometa moja.

"Baraza la madiwani likae litenge fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii ya kuingia katika machinjio haya ya kisasa ili wafanyabishara wanaokuja wasikwame kwa sababu ya ubovu wa barabara," Makonda alisema.

Alisema pia kuwapo kwa machinjio hayo ni fursa kwa Manispa kujenga reli ya kuingia eneo hilo ili mizigo isafirishwe kwa treni.

Aidha, aliwataka kuangalia namna ya kuwalipa fidia wakazi wa maeneo hayo ili kuandaa eneo kwa ajili ya kupanua machinjio hayo kwa miaka ijayo.

Makonda alisema ujenzi huo unatarajiwa kukamilika Disemba mwaka huu na kuukabidhi kwa ajili ya kuanza shughuli za kuchinja ng'ombe.

Naye Mhandisi Elisante Ulomi, alisema wanamalizia kazi ya kushindilia kifusi kwa ajili ya kuanza kusuka nondo na kumwaga zege.

Alisema mwishoni mwa mwezi Novemba wataanza kupaua, wakati kazi za kufunga umeme na kumalizia kazi za ndani zikiendelea.

Naye Meya wa Ilala, Omary Kumbilamoto, alisema wanatekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Makonda na kwamba lengo ni kuhakikisha mradi huo unakamilika Disemba na unakuwa kivutio.

Mbali na mradi huo, Makonda alitembelea mradi wa ujenzi wa soko la Kisutu na kuagiza mradi huo kukamilika mwezi Mei mwakani.


Share:

BONANZA LA MIAKA MITATU YA MISENYI JOGGING CLUB LAFANA..DC MWILA ATAKA WANANCHI WAFANYE MAZOEZI


Lydia Lugakila - Malunde 1 blog
Mkuu wa wilaya ya Misenyi mkoani Kagera Kanali Denice Mwila amewataka wananchi wilayani humo kuepuka kutumia gharama nyingi katika matibabu badala yake wajikinge na maradhi kwa kufanya mazoezi.

Kanali Mwila ametoa wito huo Septemba 28,2019 wakati wa Bonanza la kwanza la kuadhimisha miaka 3 ya Misenyi Jogging Club lililofanyika katika uwanja wa mashujaa Bunazi wilayani humo likiwa na lengo la kuwahamasisha wananchi kuipenda michezo ili kutekeleza agizo la Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan la kufanya mazoezi.

Kanali Denice Mwila amesema kuwa kupitia Bonanza hilo wananchi wanapaswa kujenga utamaduni wa kupima afya zao na kufanya mazoezi kwani michezo ni afya.

"Naomba tushirikiane kuhamasisha jamii kuwa na mwamuko wa kufanya mazoezi ili kufukuza magonjwa nyemelezi",amesema.

Kwa upande wake Mratibu wa Tamasha la Misenyi Jogging Respicius John amewapongeza wadau wote walioshiriki kikamilifu vikiwemo vyombo vya habari mkoani Kagera vilivyotangaza tamasha hilo bure kuanzia mwanzo mpaka linamalizika kuwaomba wananchi wilayani Misenyi kujitokeza kwa wingi katika kufanya mazoezi.

Respicius amesema malengo ya baadae ni kuhakikisha jamii inakuwa na nguvu kubwa katika mazoezi na kuwataka wazazi kuwaruhusu watoto wao kushiriki mazoezi ili kukuza na kuimalisha miili yao.

Bonanza hilo limeenda sanjari na utoaji wa huduma za upimaji afya ikiwemo upimaji wa VVU na kuchangia damu pamoja na michezo mbali mbali ikiwemo kuvuta kamba, kukimbia kwenye magunia kucheza Draft, pete, mpira, kumenya ndizi kwa wanaume mchezo ambao ulienda kiushindani kati ya timu zilizopewa majina ya Simba na Yanga.
Wanafunzi wa shule ya msingi Bunazi wilayani Misenyi wakionesha vipaji vyao wakati wa Bonanza la kwanza la kuadhimisha miaka 3 ya Misenyi Jogging Club lililofanyika katika uwanja wa mashujaa Bunazi wilayani humo.

 Mwanafunzi wa shule ya msingi Bunazi wilayani Misenyi akionesha kipaji chake.

Mkuu wa wilaya ya Misenyi Kanali Denice Mwila akiwa katika michezo pete

Mkuu wa wilaya ya Misenyi Kanali Denice Mwila akihamasisha wananchi kuipenda michezo.
Mratibu wa bonanza hilo Respicius John akizungumza wakati wa  bonanza.
Mchezo wa  kuvuta kamba ukiendelea

Mchezo  wa kushindana kumenya ndizi ukiendelea.
Mbio za magunia zikiendelea.
Share:

Hatimaye Mugabe azikwa katika kijiji alikozaliwa

Kiongozi mwanzilishi wa taifa la Zimbabwe Robert Mugabe amezikwa Jumamosi katika kijiji alikozaliwa cha Kutama katika eneo la Zvimba na hivyo kuhitimisha mgogoro baina ya serikali na mrithi wake, Rais Emmerson Mnangagwa kuhusu sehemu yake ya kuzikwa.

Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe aliaga dunia Septemba 6 mwezi huu huko nchini Singapore alipokuwa akipatiwa matibabu.

Awali, serikali ilikuwa imesema Mugabe angezikwa katika makaburi ya mashujaa jijini Harare. Uamuzi huo wa serikali ulikataliwa na familia ya hayati Mugabe. 

Waziri wa Habari nchini humo Nick Mangwana amesema katika taarifa kwamba, serikali imeona ni vema itii matakwa ya familia kuhusu ni wapi mpendwa wao azikwe.

Mugabe ambaye aliiongoza Zimbabwe kwa karibu miongo minne tangu nchi hiyo ipate uhuru kutoka Uingereza mwaka 1980 alilazimishwa kujiuzulu mwezi Novemba mwaka juzi baada ya mapinduzi ya jeshi.

Mugabe alikuwa na mchango mkubwa katika harakati za ukombozi wa Zimbabwe na kuiondoa nchi hiyo katika makucha ya mkoloni na hata baada ya uhuru wa Zimbabwe, alisimama kidete kutetea mamlaka ya kujitawala nchi hiyo.


Share:

AUA WAZAZI WAKE KISA WAMEINGILIA MAPENZI ALIYONAYO KWA MREMBO WA TWITTER


Mwanaume mmoja raia wa Marekani Grant Amanto (29), mwenye hisia kali za mapenzi dhidi ya mwanamke aliyemuona mtandaoni aliyefahamika kwa jina moja la Sylivia, amewaua wazazi wake pamoja na kaka yake, kwa kile kilichodaiwa kuingilia kati mapenzi yake na mpenzi wake aliyemuona mtandaoni.

Wawili hao hawakuwahi kukutana bali walikuwa wakiwasiliana kupitia mtandao wa Twitter na Skype, ambapo kijana huyo alimlaghai mrembo huyo kwa kujifanya ana uwezo mkubwa wa kifedha huku kiuhalisia alikuwa akiishi katika nyumba ndogo ya wazazi wake, mjini Chuluota, Florida .

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Polisi mjini humo, familia ya Grant ilibaini kijana wao aliiba pesa za mkopo uliochukuliwa na wazazi wake kiasi cha Dola za Kimarekani 150000, na mara baada ya wazazi kugundua hilo walimlazimisha kijana wao amwambie ukweli Sylivia juu ya hali yake ya kipato, ambapo mwenyewe alidai jambo hilo lilikuwa ni udhalilishaji kwake.

Siku ya tukio Grant alianza kwa kumuua Mama yake Marget (61), kisha Baba yake Chad (59) na hatimaye alimaliza kwa kufanya mauaji ya kaka yake Cody (30).

##SOURCE; Mirrow.co.uk news
Share:

KUNGUNI WAZUA GUMZO KWENYE BASI LA ARIZONA DAR - KIGOMA



Abiria waliokuwa wakisafiri na Basi la Kampuni ya Arizona kutoka mkoani Kigoma kuelekea jijini Dar es salaam, wamegoma kuendelea na safari baada ya kufika Tabora na kubaini uwepo wa Kunguni katika viti vya basi hilo.

Baadhi ya abiria wameleeza malalamiko yao juu ya usafiri huo kwa kudai kuwa hawawezi kuendelea na safari hiyo kwa sababu kunguni wamezidi.

Akizungumzia hali hiyo, Hamisi Mshihiri ambaye ni Kamanda wa kitengo cha ukaguzi wa Mabasi Mkoa wa Tabora, amesema baada ya gari kufika mkoani humo alichukua jukumu la kuzuia basi hilo kutokana na kukosa vigezo pamoja na kuwa na mapungufu ya usafi.

"Mimi kama Mtaalam wa Magari na mwenye dhamana eneo hili, baada la kulijaribu nimeona gari hili lina mapungufu ya ufundi na usafi, kwa kweli hatuna namna nyingine zaidi ya kulizuia, kwa sababu abiria wanateseka” amesema Kamanda Hamisi Mshihiri

Serikali ipo katika mpango wa kuweka vituo maalum vya ukaguzi wa Mabasi katia kila vituo vikuu vya Mabasi kwa kila Mkoa, ambapo mabasi ya abiria yatafanyiwa ukaguzi kabla ya kuanza safari na mwisho wa safari.
Share:

Usalama waimarishwa Misri kukabiliana na maandamano dhidi ya Rais Abdul-Fattah al-Sisi

Usalama umeimarishwa kote nchini Misri ili kukabiliana na maandamano ya wananchi dhidi ya Rais wa nchi hiyo Abdul-Fattah al-Sisi ambayo yameanza kutishia uongozi wake.

Duru za habari zinaripoti kutoka nchini Misri kwamba, vikosi vya usalama vimepelekwa katika miji muhimu ya nchi hiyo hususan ile ambayo imekuwa mstari wa mbele kwa maandamano dhidi ya Rais Abdul-Fattah al-Sisi.

Wananchi wa Misri wamekuwa wakiandamana kulalamikia matatizo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii wanayokabiliana nayo na kutaka kuondoka madarakani rais wa nchi hiyo Abdul-Fattah al-Sisi baada ya kupita miaka 8 ya vuguvugu la harakati ya wananchi wa Misri lililopelekea kung'olewa madarakani dikteta wa zamani wa nchi hiyo Hosni Mubarak.

Maandamano hayo yanafanyika kufuatia wito wa Muhammad Ali tajiri Mmisri ambaye yuko uhamishoni nchini Uhispania  baada ya kuweka wazi ufisadi wa kisiasa na kiuchumi wa al Sisi.

Muhammud Ali alituma jumbe kwa njia ya video katikia mitandao ya kijuamii akibainisha kuwa, alikuwa mkandarasi katika jeshi la Misri kwa muda wa miaka 15 na kwamba alimjengea al Sisi jumba la kifahari katika kituo cha kijeshi nchini humo.


Share:

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0673878343

watsap +255 0620510598

Huduma hii inakufikia popote ulipo


Share:

Polisi Nigeria Yawaokoa Watu 500 Waliofungwa na Kunyanyaswa Katika Jumba la Mateso

Polisi nchini Nigeria imefanikiwa kuwaokoa watoto na vijana kutoka katika kituo kimoja ambacho walikuwa wakifanyiwa mateso.

Maafisa usalama katika jimbo la Kaduna la kaskazini mwa Nigeria wametangaza kuwa, vikosi vya usalama vimefanikiwa kugundua shule moja katika jimbo hilo na kuwaokoa watoto na wanaume 500 waliokuwa wakiteswa kwa mateso mbalimbali kwa ajili ya malengo maalumu.

Vyombo vya usalama vya Kaduna havijaashiria wamiliki wa shule hiyo ingawa vimesema kuwa, wahanga wa mateso hayo walikuwa watoto  na vijana wadogo wa kiume ambao walikuwa wakitumiwa kwa malengo ya kiuchumi.

Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa, vijana hao walikuwa wakiteswa vikali kimwili, kiroho na hata kunajisiiwa.

Wengi wa  wahanga hao ni raia wa Nigeria huku wengine wakiwa ni kutoka katika nchi jirani za Burkina Faso, Mali na Ghana na walipelekwa katika shule hiyo na watu wasiojulikana au wazazi wao kwa ahadi ya kwenda kusoma masomo ya dini.

Tayari polisi ya Kaduna imewatia mbaroni watu wanane kwa tuhuma za kuhusina na mateso dhidi ya vijana hao huku walimu kadhaa wa shule hiyo ambao wanasadikiwa kuhusika katika mateso hao nao wametiwa mbaroni.

Polisi ya Nigeria imetangaza kuwa, imefungua faili la uchunguzi kuhusiana na kashfa hiyo, huku wazazi wa wahanga hao wakipokea kwa mshangao mkubwa habari ya kuteswa watoto wao.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na 
0747100745


Share:

Kiboko Ya Maumbile Madogo Na Nguvu Za Kiume

*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*


Share:

SERIKALI YAVUNJA MKATABA NA MKANDARASI UJENZI WA JENGO LA POLISI MANYARA


Na Mwandishi Wetu
Serikali imewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Manyara kuanza na kumalizika kwa Mradi  Ujenzi wa Ofisi ya Makao Makuu ya Jeshi la Polisi  ambao ulisimama tangu mwaka 2012 kutokana na gharama kubwa ya ukandarasi na sasa utajengwa kwa kutumia utaratibu mpya wa serikali wa nguvu mali ambao utapunguza gharama za ujenzi kulinganisha na kutumia mkandarasi.


 Hayo yamesemwa leo  na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni alipotembelea mradi huo uliopo katika eneo la Komoto Kata ya Bagara Wilayani Babati Mkoani Manyara ambao gharama za awali za mradi huo ni  Milioni Mia Tano Themanini na Moja,Laki tatu na Thelathini.

“Serikali tunawahakikishia wananchi wa Mkoa wa Manyara kujengwa kwa jingo la polisi ili masuala ya ulinzi na usalama yaweze kuwa imara katika mkoa huu,tayari timu maalumu kutoka makao makuu ya polisi ilishafika hapa na kuona jinsi mradi huu utakavyoweza kuendelea baada ya kusimama kwa takribani miaka saba sasa,” alisema Naibu Waziri Masauni

“Juhudi mbalimbali zishaanza na hivi navyozungumza tayari Jeshi la polisi mkoani hapa likishirikiana na wadau wameshafanya harambee na kufanikiwa  kukusanya  takribani  kiasi cha Shilingi Milioni Arobaini na Tano na sisi kama Wizara tutachangia ujenzi huo” aliongeza Masauni

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea eneo la mradi Mbunge wa Babati Mjini Pauline Gekul alisema Jeshi la Polisi linafanya kazi katika mazingira madogo,ofisi ni ndogo hali inayopelekea huduma kutolewa kwa uchache tofauti na mahitaji

“Nashukuru kuona serikali leo imefika kuona maendeleo ya huu mradi kwa kweli polisi wanahitaji jingo jipya ili kazi ya kulinda amani na utulivu iwe rahisi kwao,tunashukuru pia wadau mbalimbali wameanza kutuunga mkono ikiwa pia na ujenzi wa nyumba kwa ajili ya makazi ya askari wetu” alisema Mbunge  Gekul

Awali akitoa taarifa ya Uhalifu Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara,Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Cyprian Mushi alikiri kupungua  kwa uhalifu huku akikiri kuwepo changamoto katika kutatua baadhi ya kesi za ubakaji baada ya familia za mtuhumiwa na familia ya mtuhumu kutotokea mahakamani baada ya kuzimaliza kesi hizo kifamilia.


Share:

WAZIRI LUGOLA AWATAKA WANANCHI KUTOA TAARIFA ZA WAHAMIAJI HARAMU KUONDOA UJAMBAZI, UTEKAJI MIKOA YA MIPAKANI NCHINI


Na Felix Mwagara, MOHA-Katavi
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewataka wananchi wa mikoa ya mipakani nchini kutoa taarifa za wahamiaji haramu ili kudhibiti matukio ya ujambazi, utekaji katika maeneo hayo.


Lugola alisema uhalifu katika mikoa hiyo licha ya kuwa imethibitiwa kwa kiasi kikubwa lakini bado baadhi ya mikoa ukiwemo Mkoa wa Katavi, wahalifu utumia njia zisizo rasmi kuingia nchini na kufanya matukio ya uhalifu.

Akizungumza na mamia ya wananchi wa Kijiji cha Ikola, Wilayani Tanganyika, Mkoa wa Katavi, leo, Lugola aliwataka wananchi hao kutoa taarifa kwa vyombo vya dola, kwa mtu au watu ambao wanawatilia mashaka ili kudhibiti matukio mbalimbali ya uhalifu.

“Mnapaswa kuwa wazalendo kwa kutoa taarifa za wahamiaji haramu katika maeneo yenu ili kuisaidia serikali yenu kuwasambaratisha wahamiaji haramu ambao wanafanya uhalifu wakishirikiana na Watanzania wasiowaaminifu waishio mipakani, hii haiwezekani, na kamwe Serikali haiwezi kuchezewa,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kuwa, Tanzania ina Serikali ambayo ipo makini katika kuwalinda watu wake, hivyo kwa majambazi ambao wanafanya matukio mbalimbali ya utekaji lazima washughulikiwe ipasavyo bila kuonewa huruma.

“Wahamiaji haramu wapo mitaani kwetu, na mnawajua, hivyo mnapaswa kutoa taarifa kwa maafisa uhamiaji, Jeshi la Polisi au vyombo vingine vya dola nchini, ili Serikali ya Dkt. Magufuli iweze kuwatia mbaroni haraka iwezekanavyo,” alisema Lugola.

Kwa upande wake, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Katavi, Kamishna Msaidizi, Vicent Haule alikiri kuwepo na changamoto hiyo, na kuahidi kuwasaka wahamiaji haramu kupitia vyanzo vyote vya uchunguzi.

Haule alisema maeneo ya mipakani yana changamoto licha ya kuwa ofisi yake inafanya kazi usiku na mchana kupambana na wahamiaji haramu, na wapo tayari kupokea taarifa za wahamiaji hao watakapopewa na wananchi.

“Tunamshukuru sana mheshimiwa Waziri kwa kutupa maelekezo mbalimbali, hasa ya kuhusu masuala ya wahamiaji haramu, na uraia hasa pale makazi ya Katumba na Mishamo, kwasababu amewataka wakazi waliopewa uraia wasivunje sheria za nchi kwa kwenda Burundi na kurudi nchini bila kufuata sheria,” alisema Haule.

Aidha, Lugola aliwataka Polisi kuwasaka na kuwakamata majambazi na kuwasambaratisha bila woga wowote maana mhalifu hawezi kuchekewa.

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Lilian Matinga, alimshukuru Waziri Lugola kwa kufika katika wilaya hiyo na kuahidi maagizo yote aliyoyatoa kwa Wilaya hiyo watayafanyia kazi kupitia vikao vyao vya kamati ya ulinzi na usalama.

Waziri Lugola amemaliza ziara yake Mkoani Katavi kwa ksuikiliza kero mbalimbali za wananchi kupitia mikutano ya hadhara na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo.


Share:

MPISHI AKAMATWA KWA KUPIKA CHAKULA CHENYE BANGI

Mpishi mmoja amekamatwa kwa kutuhumiwa kwa ulanguzi wa madawa ya kulevya baada ya polisi kugundua bangi nyumbani kwake, vyombo vya habari Italia vinaripoti.

Carmelo Chiaramonte ambaye ni mpishi anayeshiriki kipindi kwenye televisheni alipatikana na mimea miwili mikubwa ya bangi na kilo mmoja ya Indian hemp, polisi inasema.

Mvinyo uliochanganywa na bangi, zaituni, kahawa, na samaki aina ya tuna pia vilikusanywa nyumbani mwake karibu na Catania huko Sicily mashariki.

Inaarifiwa mpishi huyo aliwaeleza maafisa wapolisi kwamba alikuwa anajaribu 'viungo vipya vya upishi'.

Chiaramonte amesema yeye ni mshauri wa vyakula asili kwa upishi wa kileo ", gazeti la Italia La Sicilia limeripoti.

Mpishi huyo wa miaka 50, anayeishi katika kijiji cha Trecastagni, chini ya mlima Etna ameachiwa huru huku kesi ikisubiriwa kuwasilishwa.

Chiaramonte ni mpishi katika hoteli ya Katane Palace huko Catania.

Yeye hupika vyakula vya watu wa Meditarenia kwa mujibu wa maelezo kwenye mtandao wake.

Alishiriki kipindi cha mapishi kwenye televisheni kuhusu "historia ya mazao na utamaduni wa kilimo cha Sicily", La Sicilia limeripoti.

Mojawapo ya vipindi vyake kiliitwa 'upishi uliokosa nidhamu' na 'vyakula vya kutia hamu ya tendo la ndoa', gazeti hilo limesema.
CHANZO- BBC
Share:

DC SHEKIMWERI AWAPA NENO WATAALAM WA MALISHO NCHINI

Mkurugenzi wa Utafiti,Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya Mifugo Dkt.Angello Mwillawa,akiongozana na Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mhe.Jabir Shekimweri,alipowasili kwa ajili ya kufungua mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mhe.Jabir Shekimweri,akisalimiana na Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Mifugo(LITA) Mpwapwa, Moses Mlahagwa anayefatia ni Afisa mifugo Mkuu Idara ya malisho na Rasilimali ya vyakula vya mifugo Israel Kilonzo alipowasili kwa ajili ya kufungua mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mhe.Jabir Shekimweri,akisaini kitabu mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kufungua mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa kulia kwake ni Mkurugenzi wa Utafiti,Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya Mifugo Dkt.Angello Mwillawa wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mhe.Jabir Shekimweri,akizungumza wakati wa kufungua Kikao cha mafunzo rejea kwa wataalam wa malisho kutoka mashamba ya Serikali na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika leo kushoto ni Mkurugenzi wa Utafiti,Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya Mifugo Dkt.Angello Mwillawa na upande wa kulia ni Mkuu wa Kampasi Lita Mpwapwa yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkurugenzi wa Utafiti ,Mafunzo na Ugani kutoka wizara ya Mifugo Dkt.Angello Mwillawa,akifafanua jambo kwa washiriki wa mafunzo rejea kwa wataalam wa malisho kutoka mashamba ya Serikali na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Meneja wa shamba la kuzalisha malisho na mbegu za malisho Vikuge Kibaha Ricahard Mdegipala,akitoa taarifa katika kikao cha mafunzo rejea kwa wataalam wa malisho kutoka mashamba ya Serikali na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Sehemu ya washiriki kutoka sehemu mbalimbali wakifatilia ufunguzi wa mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Afisa Mifugo na Mtaalam wa malisho kutoka Mabuki Bi.Asteria Mwaya,akitoa taarifa wakati semina ya mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Mifugo(LITA) Mpwapwa, Moses Mlahagwa,akisisitiza jambo kwa wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Meneja wa Shamba la malisho Langwira Mbarali mkoani Mbeya ,akitoa taarifa wakati semina ya mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkurugenzi wa Utafiti,mafunzo na Ugani kutoka wizara ya Mifugo Dkt.Angello Mwillawa,akizungumza jambo na Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mhe.Jabir Shekimweri mara baada ya semina ya mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkurugenzi wa Utafiti,Mafunzo na Ugani kutoka wizara ya Mifugo Dkt.Mwillawa akitoa maada katika kikao cha mafunzo ya rejea kwa wataalam wa malisho kutoka mashamba ya Serikali na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Sehemu ya wataalam kutoka sehemu mbalimbali wakiendelea kuchangia mada katika semina ya mafunzo ya wataalam na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
...................

Wataalamu wa malisho kutoka halmashauri mbalimbali hapa nchini, wametakiwa kutoa elimu hiyo kwa wafugaji ili kuwajengea uwezo wa kutambua matumizi bora na endelevu ya nyanda za malisho.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri wakati akifungua mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.

Mkuu wa Wilaya Shekimwer alisema elimu ya utunzaji malisho ni muhimu kwa wafugaji kwa sababu itawasaidia kujua nini wanatakiwa kufanya ili kudhibiti uhaba wa malisho pale unapotokea.

Alisema lengo lao ni kuona maafisa ugani hao wanatumia nafasi walionayo kutoa elimu hiyo kiufanisi kwa wafugaji katika halmashauri mbalimbali wanazotoka ambayo itasaidia kupunguza migogoro baina ya wafugaji na wakulima kugombea maeneo ya malisho.

"Mafunzo mliyoyapata mkayatoe kwa wafugaji katika sehemu mnazotoka tumieni nafasi yenu ili kuisaidia serikali ya awamu ya tano kuboresha sekta ya Mifugo," amesema Shekimwer.

"Mnapaswa kuhamasisha na kuongeza uvunaji wa malisho na matumizi ya teknolojia rahisi za kukata,kufunga,na kuhifadhi majani na masalia ya mazao ili yatumike wakati wa uhaba" alisema.

Alisema kuwa hayo yakitekelezwa anaimani itasaidia wafugaji kujenga Utamaduni wa kusindika masalia ya nafaka na kuchakata kwa ajili ya kulisha Mifugo yao.

Pia ameiopongeza wizara ya Mifugo kutokana na kuwa mstari wa mbele kutoa mafunzo kwa maafisa ugani mara kwa mara ambayo yanasaidia kuwakumbusha majukumu yao ya kazi.



Aidha alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inalenga kuboresha sekta hivyo,hivyo ni vema maafisa ugani na wataalamu wa malisho kuzingatia elimu wanayopewa ili nao wakaitoe kwa wafugaji.

Awali akieleza lengo la semina hiyo, Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara hiyo,Dkt.Angello Mwillawa, alisema ili kukabiliana na changamoto pamoja na migogoro inayowakumba wakulima na wafugaji, wizara umeona iwakutanishe wataalam wa malisho nchi nzima ili kila mmoja aainishe changamoto anazokutana nazo katika eneo lake.

Dkt.Mwillawa aliwataka wataalam hao kuwa wa wazi kueleza changamoto zilizopo ili wizara iweze kufahamu wapi pa kuanzia katika kutatua changamoto na migogoro hiyo.

Akizungumzia changamoto ya upatikanaji wa mbegu za malisho ambayo ilielezwa na washiriki, alisema hakuna changamoto kama hiyo mbegu zipo nyingi tatizo ni uzembe wa wataalam hao katika kuagiza na kufuatilia kwa karibu ili ziwafikie katika vituo vyao.

Mkurugenzi huyo aliwataka kuhakikisha wanakuwa 'na mtandao bora na kubadilishana uzoefu baina ya eneo moja na jingine jambo ambalo litawapa wepesi katika kutatua kila changamoto.

Pia aliwataka kuongeza thamani katika bidhaa zao 'na kuainisha aina ya mbegu wanazozalisha na kuuza kwa wafugaji pamoja na faida au hasara yake hiyo itakuwa rahisi kufanya biashara.

Kwa upande wao washiriki wa semina hiyo waliishukuru wizara kwa kuandaa warsha hiyo huku wakieleza changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo uwezo mdogo wa kuendeleza maeneo yao hivyo kujikuta maeneo mengi yakubali kuwa vichaka licha ya kuwa na uhitaji wa maeneo.

Akizungumza Meneja wa Shamba la Malisho Vikuge wilayani kibaha mkoani Pwani, Richard Mdegipala, alisema wao wana eneo la ukubwa wa hekta 515 lakini hekta 215 ya shamba au eneo hilo ni pori wameshindwa kuliendeleza wakiiomba serikali iwasaidie.

Naye Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Mifugo(LITA) Mpwapwa, Moses Mlahagwa, aliwataka wataalam hao kuhakikisha wanatafuta alama ya kuiweka watakaporejea katika vituo vyao vya kazi mara baada ya warsha hiyo ili kuonyesha kuwa ilikuwa na tija kubwa wao.

"Hapo mlipo mtambue kuwa mmebeba dhamana ya mifugo ya Taifa nanyi ndio mnaotarajiwa kubadili changamoto za wafugaji kuwa fulsa, jambo la muhimu kwenu mnalotakiwa kulifanyia kazi ni alama gani mnakwenda ukiacha,"alisema.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger