Sunday 29 September 2019

Hatimaye Mugabe azikwa katika kijiji alikozaliwa

Kiongozi mwanzilishi wa taifa la Zimbabwe Robert Mugabe amezikwa Jumamosi katika kijiji alikozaliwa cha Kutama katika eneo la Zvimba na hivyo kuhitimisha mgogoro baina ya serikali na mrithi wake, Rais Emmerson Mnangagwa kuhusu sehemu yake ya kuzikwa.

Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe aliaga dunia Septemba 6 mwezi huu huko nchini Singapore alipokuwa akipatiwa matibabu.

Awali, serikali ilikuwa imesema Mugabe angezikwa katika makaburi ya mashujaa jijini Harare. Uamuzi huo wa serikali ulikataliwa na familia ya hayati Mugabe. 

Waziri wa Habari nchini humo Nick Mangwana amesema katika taarifa kwamba, serikali imeona ni vema itii matakwa ya familia kuhusu ni wapi mpendwa wao azikwe.

Mugabe ambaye aliiongoza Zimbabwe kwa karibu miongo minne tangu nchi hiyo ipate uhuru kutoka Uingereza mwaka 1980 alilazimishwa kujiuzulu mwezi Novemba mwaka juzi baada ya mapinduzi ya jeshi.

Mugabe alikuwa na mchango mkubwa katika harakati za ukombozi wa Zimbabwe na kuiondoa nchi hiyo katika makucha ya mkoloni na hata baada ya uhuru wa Zimbabwe, alisimama kidete kutetea mamlaka ya kujitawala nchi hiyo.


Share:

AUA WAZAZI WAKE KISA WAMEINGILIA MAPENZI ALIYONAYO KWA MREMBO WA TWITTER


Mwanaume mmoja raia wa Marekani Grant Amanto (29), mwenye hisia kali za mapenzi dhidi ya mwanamke aliyemuona mtandaoni aliyefahamika kwa jina moja la Sylivia, amewaua wazazi wake pamoja na kaka yake, kwa kile kilichodaiwa kuingilia kati mapenzi yake na mpenzi wake aliyemuona mtandaoni.

Wawili hao hawakuwahi kukutana bali walikuwa wakiwasiliana kupitia mtandao wa Twitter na Skype, ambapo kijana huyo alimlaghai mrembo huyo kwa kujifanya ana uwezo mkubwa wa kifedha huku kiuhalisia alikuwa akiishi katika nyumba ndogo ya wazazi wake, mjini Chuluota, Florida .

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Polisi mjini humo, familia ya Grant ilibaini kijana wao aliiba pesa za mkopo uliochukuliwa na wazazi wake kiasi cha Dola za Kimarekani 150000, na mara baada ya wazazi kugundua hilo walimlazimisha kijana wao amwambie ukweli Sylivia juu ya hali yake ya kipato, ambapo mwenyewe alidai jambo hilo lilikuwa ni udhalilishaji kwake.

Siku ya tukio Grant alianza kwa kumuua Mama yake Marget (61), kisha Baba yake Chad (59) na hatimaye alimaliza kwa kufanya mauaji ya kaka yake Cody (30).

##SOURCE; Mirrow.co.uk news
Share:

KUNGUNI WAZUA GUMZO KWENYE BASI LA ARIZONA DAR - KIGOMA



Abiria waliokuwa wakisafiri na Basi la Kampuni ya Arizona kutoka mkoani Kigoma kuelekea jijini Dar es salaam, wamegoma kuendelea na safari baada ya kufika Tabora na kubaini uwepo wa Kunguni katika viti vya basi hilo.

Baadhi ya abiria wameleeza malalamiko yao juu ya usafiri huo kwa kudai kuwa hawawezi kuendelea na safari hiyo kwa sababu kunguni wamezidi.

Akizungumzia hali hiyo, Hamisi Mshihiri ambaye ni Kamanda wa kitengo cha ukaguzi wa Mabasi Mkoa wa Tabora, amesema baada ya gari kufika mkoani humo alichukua jukumu la kuzuia basi hilo kutokana na kukosa vigezo pamoja na kuwa na mapungufu ya usafi.

"Mimi kama Mtaalam wa Magari na mwenye dhamana eneo hili, baada la kulijaribu nimeona gari hili lina mapungufu ya ufundi na usafi, kwa kweli hatuna namna nyingine zaidi ya kulizuia, kwa sababu abiria wanateseka” amesema Kamanda Hamisi Mshihiri

Serikali ipo katika mpango wa kuweka vituo maalum vya ukaguzi wa Mabasi katia kila vituo vikuu vya Mabasi kwa kila Mkoa, ambapo mabasi ya abiria yatafanyiwa ukaguzi kabla ya kuanza safari na mwisho wa safari.
Share:

Usalama waimarishwa Misri kukabiliana na maandamano dhidi ya Rais Abdul-Fattah al-Sisi

Usalama umeimarishwa kote nchini Misri ili kukabiliana na maandamano ya wananchi dhidi ya Rais wa nchi hiyo Abdul-Fattah al-Sisi ambayo yameanza kutishia uongozi wake.

Duru za habari zinaripoti kutoka nchini Misri kwamba, vikosi vya usalama vimepelekwa katika miji muhimu ya nchi hiyo hususan ile ambayo imekuwa mstari wa mbele kwa maandamano dhidi ya Rais Abdul-Fattah al-Sisi.

Wananchi wa Misri wamekuwa wakiandamana kulalamikia matatizo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii wanayokabiliana nayo na kutaka kuondoka madarakani rais wa nchi hiyo Abdul-Fattah al-Sisi baada ya kupita miaka 8 ya vuguvugu la harakati ya wananchi wa Misri lililopelekea kung'olewa madarakani dikteta wa zamani wa nchi hiyo Hosni Mubarak.

Maandamano hayo yanafanyika kufuatia wito wa Muhammad Ali tajiri Mmisri ambaye yuko uhamishoni nchini Uhispania  baada ya kuweka wazi ufisadi wa kisiasa na kiuchumi wa al Sisi.

Muhammud Ali alituma jumbe kwa njia ya video katikia mitandao ya kijuamii akibainisha kuwa, alikuwa mkandarasi katika jeshi la Misri kwa muda wa miaka 15 na kwamba alimjengea al Sisi jumba la kifahari katika kituo cha kijeshi nchini humo.


Share:

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0673878343

watsap +255 0620510598

Huduma hii inakufikia popote ulipo


Share:

Polisi Nigeria Yawaokoa Watu 500 Waliofungwa na Kunyanyaswa Katika Jumba la Mateso

Polisi nchini Nigeria imefanikiwa kuwaokoa watoto na vijana kutoka katika kituo kimoja ambacho walikuwa wakifanyiwa mateso.

Maafisa usalama katika jimbo la Kaduna la kaskazini mwa Nigeria wametangaza kuwa, vikosi vya usalama vimefanikiwa kugundua shule moja katika jimbo hilo na kuwaokoa watoto na wanaume 500 waliokuwa wakiteswa kwa mateso mbalimbali kwa ajili ya malengo maalumu.

Vyombo vya usalama vya Kaduna havijaashiria wamiliki wa shule hiyo ingawa vimesema kuwa, wahanga wa mateso hayo walikuwa watoto  na vijana wadogo wa kiume ambao walikuwa wakitumiwa kwa malengo ya kiuchumi.

Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa, vijana hao walikuwa wakiteswa vikali kimwili, kiroho na hata kunajisiiwa.

Wengi wa  wahanga hao ni raia wa Nigeria huku wengine wakiwa ni kutoka katika nchi jirani za Burkina Faso, Mali na Ghana na walipelekwa katika shule hiyo na watu wasiojulikana au wazazi wao kwa ahadi ya kwenda kusoma masomo ya dini.

Tayari polisi ya Kaduna imewatia mbaroni watu wanane kwa tuhuma za kuhusina na mateso dhidi ya vijana hao huku walimu kadhaa wa shule hiyo ambao wanasadikiwa kuhusika katika mateso hao nao wametiwa mbaroni.

Polisi ya Nigeria imetangaza kuwa, imefungua faili la uchunguzi kuhusiana na kashfa hiyo, huku wazazi wa wahanga hao wakipokea kwa mshangao mkubwa habari ya kuteswa watoto wao.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na 
0747100745


Share:

Kiboko Ya Maumbile Madogo Na Nguvu Za Kiume

*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*


Share:

SERIKALI YAVUNJA MKATABA NA MKANDARASI UJENZI WA JENGO LA POLISI MANYARA


Na Mwandishi Wetu
Serikali imewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Manyara kuanza na kumalizika kwa Mradi  Ujenzi wa Ofisi ya Makao Makuu ya Jeshi la Polisi  ambao ulisimama tangu mwaka 2012 kutokana na gharama kubwa ya ukandarasi na sasa utajengwa kwa kutumia utaratibu mpya wa serikali wa nguvu mali ambao utapunguza gharama za ujenzi kulinganisha na kutumia mkandarasi.


 Hayo yamesemwa leo  na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni alipotembelea mradi huo uliopo katika eneo la Komoto Kata ya Bagara Wilayani Babati Mkoani Manyara ambao gharama za awali za mradi huo ni  Milioni Mia Tano Themanini na Moja,Laki tatu na Thelathini.

“Serikali tunawahakikishia wananchi wa Mkoa wa Manyara kujengwa kwa jingo la polisi ili masuala ya ulinzi na usalama yaweze kuwa imara katika mkoa huu,tayari timu maalumu kutoka makao makuu ya polisi ilishafika hapa na kuona jinsi mradi huu utakavyoweza kuendelea baada ya kusimama kwa takribani miaka saba sasa,” alisema Naibu Waziri Masauni

“Juhudi mbalimbali zishaanza na hivi navyozungumza tayari Jeshi la polisi mkoani hapa likishirikiana na wadau wameshafanya harambee na kufanikiwa  kukusanya  takribani  kiasi cha Shilingi Milioni Arobaini na Tano na sisi kama Wizara tutachangia ujenzi huo” aliongeza Masauni

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea eneo la mradi Mbunge wa Babati Mjini Pauline Gekul alisema Jeshi la Polisi linafanya kazi katika mazingira madogo,ofisi ni ndogo hali inayopelekea huduma kutolewa kwa uchache tofauti na mahitaji

“Nashukuru kuona serikali leo imefika kuona maendeleo ya huu mradi kwa kweli polisi wanahitaji jingo jipya ili kazi ya kulinda amani na utulivu iwe rahisi kwao,tunashukuru pia wadau mbalimbali wameanza kutuunga mkono ikiwa pia na ujenzi wa nyumba kwa ajili ya makazi ya askari wetu” alisema Mbunge  Gekul

Awali akitoa taarifa ya Uhalifu Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara,Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Cyprian Mushi alikiri kupungua  kwa uhalifu huku akikiri kuwepo changamoto katika kutatua baadhi ya kesi za ubakaji baada ya familia za mtuhumiwa na familia ya mtuhumu kutotokea mahakamani baada ya kuzimaliza kesi hizo kifamilia.


Share:

WAZIRI LUGOLA AWATAKA WANANCHI KUTOA TAARIFA ZA WAHAMIAJI HARAMU KUONDOA UJAMBAZI, UTEKAJI MIKOA YA MIPAKANI NCHINI


Na Felix Mwagara, MOHA-Katavi
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewataka wananchi wa mikoa ya mipakani nchini kutoa taarifa za wahamiaji haramu ili kudhibiti matukio ya ujambazi, utekaji katika maeneo hayo.


Lugola alisema uhalifu katika mikoa hiyo licha ya kuwa imethibitiwa kwa kiasi kikubwa lakini bado baadhi ya mikoa ukiwemo Mkoa wa Katavi, wahalifu utumia njia zisizo rasmi kuingia nchini na kufanya matukio ya uhalifu.

Akizungumza na mamia ya wananchi wa Kijiji cha Ikola, Wilayani Tanganyika, Mkoa wa Katavi, leo, Lugola aliwataka wananchi hao kutoa taarifa kwa vyombo vya dola, kwa mtu au watu ambao wanawatilia mashaka ili kudhibiti matukio mbalimbali ya uhalifu.

“Mnapaswa kuwa wazalendo kwa kutoa taarifa za wahamiaji haramu katika maeneo yenu ili kuisaidia serikali yenu kuwasambaratisha wahamiaji haramu ambao wanafanya uhalifu wakishirikiana na Watanzania wasiowaaminifu waishio mipakani, hii haiwezekani, na kamwe Serikali haiwezi kuchezewa,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kuwa, Tanzania ina Serikali ambayo ipo makini katika kuwalinda watu wake, hivyo kwa majambazi ambao wanafanya matukio mbalimbali ya utekaji lazima washughulikiwe ipasavyo bila kuonewa huruma.

“Wahamiaji haramu wapo mitaani kwetu, na mnawajua, hivyo mnapaswa kutoa taarifa kwa maafisa uhamiaji, Jeshi la Polisi au vyombo vingine vya dola nchini, ili Serikali ya Dkt. Magufuli iweze kuwatia mbaroni haraka iwezekanavyo,” alisema Lugola.

Kwa upande wake, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Katavi, Kamishna Msaidizi, Vicent Haule alikiri kuwepo na changamoto hiyo, na kuahidi kuwasaka wahamiaji haramu kupitia vyanzo vyote vya uchunguzi.

Haule alisema maeneo ya mipakani yana changamoto licha ya kuwa ofisi yake inafanya kazi usiku na mchana kupambana na wahamiaji haramu, na wapo tayari kupokea taarifa za wahamiaji hao watakapopewa na wananchi.

“Tunamshukuru sana mheshimiwa Waziri kwa kutupa maelekezo mbalimbali, hasa ya kuhusu masuala ya wahamiaji haramu, na uraia hasa pale makazi ya Katumba na Mishamo, kwasababu amewataka wakazi waliopewa uraia wasivunje sheria za nchi kwa kwenda Burundi na kurudi nchini bila kufuata sheria,” alisema Haule.

Aidha, Lugola aliwataka Polisi kuwasaka na kuwakamata majambazi na kuwasambaratisha bila woga wowote maana mhalifu hawezi kuchekewa.

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Lilian Matinga, alimshukuru Waziri Lugola kwa kufika katika wilaya hiyo na kuahidi maagizo yote aliyoyatoa kwa Wilaya hiyo watayafanyia kazi kupitia vikao vyao vya kamati ya ulinzi na usalama.

Waziri Lugola amemaliza ziara yake Mkoani Katavi kwa ksuikiliza kero mbalimbali za wananchi kupitia mikutano ya hadhara na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo.


Share:

MPISHI AKAMATWA KWA KUPIKA CHAKULA CHENYE BANGI

Mpishi mmoja amekamatwa kwa kutuhumiwa kwa ulanguzi wa madawa ya kulevya baada ya polisi kugundua bangi nyumbani kwake, vyombo vya habari Italia vinaripoti.

Carmelo Chiaramonte ambaye ni mpishi anayeshiriki kipindi kwenye televisheni alipatikana na mimea miwili mikubwa ya bangi na kilo mmoja ya Indian hemp, polisi inasema.

Mvinyo uliochanganywa na bangi, zaituni, kahawa, na samaki aina ya tuna pia vilikusanywa nyumbani mwake karibu na Catania huko Sicily mashariki.

Inaarifiwa mpishi huyo aliwaeleza maafisa wapolisi kwamba alikuwa anajaribu 'viungo vipya vya upishi'.

Chiaramonte amesema yeye ni mshauri wa vyakula asili kwa upishi wa kileo ", gazeti la Italia La Sicilia limeripoti.

Mpishi huyo wa miaka 50, anayeishi katika kijiji cha Trecastagni, chini ya mlima Etna ameachiwa huru huku kesi ikisubiriwa kuwasilishwa.

Chiaramonte ni mpishi katika hoteli ya Katane Palace huko Catania.

Yeye hupika vyakula vya watu wa Meditarenia kwa mujibu wa maelezo kwenye mtandao wake.

Alishiriki kipindi cha mapishi kwenye televisheni kuhusu "historia ya mazao na utamaduni wa kilimo cha Sicily", La Sicilia limeripoti.

Mojawapo ya vipindi vyake kiliitwa 'upishi uliokosa nidhamu' na 'vyakula vya kutia hamu ya tendo la ndoa', gazeti hilo limesema.
CHANZO- BBC
Share:

DC SHEKIMWERI AWAPA NENO WATAALAM WA MALISHO NCHINI

Mkurugenzi wa Utafiti,Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya Mifugo Dkt.Angello Mwillawa,akiongozana na Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mhe.Jabir Shekimweri,alipowasili kwa ajili ya kufungua mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mhe.Jabir Shekimweri,akisalimiana na Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Mifugo(LITA) Mpwapwa, Moses Mlahagwa anayefatia ni Afisa mifugo Mkuu Idara ya malisho na Rasilimali ya vyakula vya mifugo Israel Kilonzo alipowasili kwa ajili ya kufungua mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mhe.Jabir Shekimweri,akisaini kitabu mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kufungua mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa kulia kwake ni Mkurugenzi wa Utafiti,Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya Mifugo Dkt.Angello Mwillawa wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mhe.Jabir Shekimweri,akizungumza wakati wa kufungua Kikao cha mafunzo rejea kwa wataalam wa malisho kutoka mashamba ya Serikali na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika leo kushoto ni Mkurugenzi wa Utafiti,Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya Mifugo Dkt.Angello Mwillawa na upande wa kulia ni Mkuu wa Kampasi Lita Mpwapwa yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkurugenzi wa Utafiti ,Mafunzo na Ugani kutoka wizara ya Mifugo Dkt.Angello Mwillawa,akifafanua jambo kwa washiriki wa mafunzo rejea kwa wataalam wa malisho kutoka mashamba ya Serikali na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Meneja wa shamba la kuzalisha malisho na mbegu za malisho Vikuge Kibaha Ricahard Mdegipala,akitoa taarifa katika kikao cha mafunzo rejea kwa wataalam wa malisho kutoka mashamba ya Serikali na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Sehemu ya washiriki kutoka sehemu mbalimbali wakifatilia ufunguzi wa mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Afisa Mifugo na Mtaalam wa malisho kutoka Mabuki Bi.Asteria Mwaya,akitoa taarifa wakati semina ya mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Mifugo(LITA) Mpwapwa, Moses Mlahagwa,akisisitiza jambo kwa wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Meneja wa Shamba la malisho Langwira Mbarali mkoani Mbeya ,akitoa taarifa wakati semina ya mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkurugenzi wa Utafiti,mafunzo na Ugani kutoka wizara ya Mifugo Dkt.Angello Mwillawa,akizungumza jambo na Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Mhe.Jabir Shekimweri mara baada ya semina ya mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Mkurugenzi wa Utafiti,Mafunzo na Ugani kutoka wizara ya Mifugo Dkt.Mwillawa akitoa maada katika kikao cha mafunzo ya rejea kwa wataalam wa malisho kutoka mashamba ya Serikali na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
Sehemu ya wataalam kutoka sehemu mbalimbali wakiendelea kuchangia mada katika semina ya mafunzo ya wataalam na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.
...................

Wataalamu wa malisho kutoka halmashauri mbalimbali hapa nchini, wametakiwa kutoa elimu hiyo kwa wafugaji ili kuwajengea uwezo wa kutambua matumizi bora na endelevu ya nyanda za malisho.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri wakati akifungua mafunzo ya wataalamu na wadau wa malisho nchini yaliyofanyika katika chuo cha Mifugo Lita Mpwapwa.

Mkuu wa Wilaya Shekimwer alisema elimu ya utunzaji malisho ni muhimu kwa wafugaji kwa sababu itawasaidia kujua nini wanatakiwa kufanya ili kudhibiti uhaba wa malisho pale unapotokea.

Alisema lengo lao ni kuona maafisa ugani hao wanatumia nafasi walionayo kutoa elimu hiyo kiufanisi kwa wafugaji katika halmashauri mbalimbali wanazotoka ambayo itasaidia kupunguza migogoro baina ya wafugaji na wakulima kugombea maeneo ya malisho.

"Mafunzo mliyoyapata mkayatoe kwa wafugaji katika sehemu mnazotoka tumieni nafasi yenu ili kuisaidia serikali ya awamu ya tano kuboresha sekta ya Mifugo," amesema Shekimwer.

"Mnapaswa kuhamasisha na kuongeza uvunaji wa malisho na matumizi ya teknolojia rahisi za kukata,kufunga,na kuhifadhi majani na masalia ya mazao ili yatumike wakati wa uhaba" alisema.

Alisema kuwa hayo yakitekelezwa anaimani itasaidia wafugaji kujenga Utamaduni wa kusindika masalia ya nafaka na kuchakata kwa ajili ya kulisha Mifugo yao.

Pia ameiopongeza wizara ya Mifugo kutokana na kuwa mstari wa mbele kutoa mafunzo kwa maafisa ugani mara kwa mara ambayo yanasaidia kuwakumbusha majukumu yao ya kazi.



Aidha alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inalenga kuboresha sekta hivyo,hivyo ni vema maafisa ugani na wataalamu wa malisho kuzingatia elimu wanayopewa ili nao wakaitoe kwa wafugaji.

Awali akieleza lengo la semina hiyo, Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara hiyo,Dkt.Angello Mwillawa, alisema ili kukabiliana na changamoto pamoja na migogoro inayowakumba wakulima na wafugaji, wizara umeona iwakutanishe wataalam wa malisho nchi nzima ili kila mmoja aainishe changamoto anazokutana nazo katika eneo lake.

Dkt.Mwillawa aliwataka wataalam hao kuwa wa wazi kueleza changamoto zilizopo ili wizara iweze kufahamu wapi pa kuanzia katika kutatua changamoto na migogoro hiyo.

Akizungumzia changamoto ya upatikanaji wa mbegu za malisho ambayo ilielezwa na washiriki, alisema hakuna changamoto kama hiyo mbegu zipo nyingi tatizo ni uzembe wa wataalam hao katika kuagiza na kufuatilia kwa karibu ili ziwafikie katika vituo vyao.

Mkurugenzi huyo aliwataka kuhakikisha wanakuwa 'na mtandao bora na kubadilishana uzoefu baina ya eneo moja na jingine jambo ambalo litawapa wepesi katika kutatua kila changamoto.

Pia aliwataka kuongeza thamani katika bidhaa zao 'na kuainisha aina ya mbegu wanazozalisha na kuuza kwa wafugaji pamoja na faida au hasara yake hiyo itakuwa rahisi kufanya biashara.

Kwa upande wao washiriki wa semina hiyo waliishukuru wizara kwa kuandaa warsha hiyo huku wakieleza changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo uwezo mdogo wa kuendeleza maeneo yao hivyo kujikuta maeneo mengi yakubali kuwa vichaka licha ya kuwa na uhitaji wa maeneo.

Akizungumza Meneja wa Shamba la Malisho Vikuge wilayani kibaha mkoani Pwani, Richard Mdegipala, alisema wao wana eneo la ukubwa wa hekta 515 lakini hekta 215 ya shamba au eneo hilo ni pori wameshindwa kuliendeleza wakiiomba serikali iwasaidie.

Naye Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Mifugo(LITA) Mpwapwa, Moses Mlahagwa, aliwataka wataalam hao kuhakikisha wanatafuta alama ya kuiweka watakaporejea katika vituo vyao vya kazi mara baada ya warsha hiyo ili kuonyesha kuwa ilikuwa na tija kubwa wao.

"Hapo mlipo mtambue kuwa mmebeba dhamana ya mifugo ya Taifa nanyi ndio mnaotarajiwa kubadili changamoto za wafugaji kuwa fulsa, jambo la muhimu kwenu mnalotakiwa kulifanyia kazi ni alama gani mnakwenda ukiacha,"alisema.
Share:

Waziri Mkuu: Tusikwepe Jukumu La Kuwatunza Wazee

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka vijana na jamii kwa ujumla wasikwepe jukumu la kuwatunza wazee kwa sababu nguvu zao za uzalishaji mali zimepungua kutokana na kazi waliyoifanya wakiwa vijana kwa ajili ya maendeleo na ustawi wa familia zao na Taifa kwa ujumla.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Kitaifa wa Kutokomeza Mauaji ya Wazee uliozinduliwa Januari, 2019 ili  kwa kutokomeza ukatili kwa wazee ifikapo 2023 na kuhakikisha wazee na watu wenye ulemavu wanatambuliwa na kulindwa dhidi ya ubaguzi, uonevu, ukatili na mila potofu.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Septemba 29, 2019) wakati akizindua kambi ya utoaji wa huduma za afya kwa wazee na watu wenye ulemavu katika viwanja vya Kichanganimjini Iringa. Kambi hiyo imeandaliwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Dkt. Ritta Kabati katika kuadhimisha siku ya Wazee Duniani.

Amesema wajibu wa kuwahudumia au kuwasaidia wazee na watu wenye ulemavu ni wa kila mmoja na wanapaswa watambue kwamba wazee hao wamelitumikia Taifa kwa muda mrefu tena kwa namna mbalimbali ikiwemo kuwaletea na kuhakikisha wanapata mafanikio hayo ambayo wanajivunia sasa.

“Kwa msingi huo, tunao wajibu wa kuwajali wazee wetu kwa hali na mali ikiwa ni sehemu ya matunda ya uwajibikaji wao kwetu na kwa Taifa kwa ujumla. Hivyo basi, tutumie vema Kambi hii kuwasaidia wazee wetu na watu wenye ulemavu kwa kutambua afya zao na kuwapatia matibabu ya kiafaya ili waendelee kuwa salama na wenye furaha nasi tuvune busara zao.”

Kutokana na umuhimu wa kuwatunza wazee na kuwasaidia watu wenye ulemavu, Waziri Mkuu ametoa rai kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa, wananchi na wadau mbalimbali kuendelea kuimarisha upatikanaji wa fursa, haki na ustawi wa wazee ikiwemo kuondokana kabisa na vitendo vya ukatili dhidi yao.

“Vituo vyote vya kutoa huduma za afya vya umma kutoa huduma bora na za haraka kwa wazee wetu wenye vitambulisho. Tengeni dirisha maalumu kwa ajili ya kuwahudumia ili wasikae kwenye foleni muda mrefu. Serikali itaendelea kuweka miundombinu na mazingira rafiki ili kuwawezesha kupata mahitaji yao.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kusimamia maelekezo yake kwa Halmashauri zote nchini kuwatambua wazee wasiojiweza na kuwapatia vitambulisho vya matibabu bila malipo. “Namshukuru Mbunge wa Viti Maalum Ritha Kabati amebainisha mafanikio yanayoendelea kupatikana kutokana na utekelezaji wa agizo hilo.

“Haidhuru nasi tukiiga mfano wa Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalumu na kaka yangu Mheshimiwa Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu kwa moyo wao wa kizalendo kabisa kuona kuna haja ya kusaidia na kuunga mkono juhudi za Rais wetu mpendwa Dkt. John Magufuli za kuwahudumia wanyonge.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu ameendelea kuziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha zoezi hilo linakuwa endelevu kwa kuwatambua na kuwapatia vitambulisho wazee wote nchini wasio na uwezo ili waweze kunufaika na huduma ya matibabu bila malipo pamoja na huduma zingine za kijamii.

Vilevile, Waziri Mkuu amesema kwa kuwa Novemba 2019 nchi inatarajia kufanya uchaguzi wa Serikali za Mitaa, wazee kama sehemu ya jamii wana haki ya kushiriki katika uchaguzi huo kwa kuchagua viongozi wanaoona watafaa kuwaongoza na wao kuchaguliwa kuongoza katika nafasi mbalimbali. Hivyo wasaidiwe kushiriki zoezi hilo.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu Mstaafu na Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa, Peter Pinda alimpongeza Dkt. Ritta kwa uamuzi wake wa kuandaa kambi hiyo ambayo itatoa fursa kwa wazee kupima afya zao na kupatiwa huduma pamoja na kutoa viungo bandia kwa baadhi ya walemavu.

“Uzee ni hali siyokwepeka upende usipende ila unaweza kucheleweshwa kutegemea na aina ya matunzo wanayopatiwa. Nashauri wazee wapate vyakula bora tena kwa uwiano sahihi, vyakula hivyo ni pamoja na vya jamii ya mizizi, mikunde, nafaka, mbogamboga na nyama ili waweze kuimarisha afya zao.”

Awali, Waziri Mkuu alipokea taariza za ujenzi wa jengo la Ustawi wa Jamii Manispaa ya Iringa lilojengwa kwa ufadhili wa Mkurugenzi wa Kundi la Makampuni ya Asas, Salim Abri kwa gharama ya sh. milioni 60.

Kwa upande wake,Afisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Iringa Tiniel Mmbaga alisema kukamilika kwa jengo hilo kutawawezesha kutoa huduma bora kwa jamii na kwa wakati kwani awali maafisa watano walikuwa wakilundikana katika chumba kimoja hali iliyosababisha wateja kushindwa kueleza matatizo yao baada ya kukosekana kwa usiri.

Alisema kwa siku wanashughulikia malalamiko yahusuyo masuala ya migogoro ya familia ikiwemo matunzo ya watoto kuanzia 15 hadi 30 pamoja na wanawake zaidi ya 50 ambao kila mwezi wanakwenda kuchukua fedha kwa ajili ya matunzo ya watoto zinazotolewa na wenza wao kufuatia kuwepo kwa migogoro baina yao.

Shughuli hiyo, imehudhuriwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Dkt. Augustine Mahiga, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI Josephat Kandege, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na wenye UlemavuStela Ikupa pamoja na Maafisa wengine wa Serikali.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Rais wa China amtunuku Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania Dr Salim Ahmed Salim Nishani ya Juu ya Urafiki

Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mheshimiwa Xi Jinping, leo asubuhi tarehe 29 Septemba 2019 amemtunukia Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa. Dk. Salim Ahmed Salim, Nishani ya Juu ya Urafiki ya Jamhuri ya Watu wa China ikiwa ni sehemu ya matukio ya maadhimisho ya miaka 70 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China iliyofanyika jijini Beijing.  Mheshimiwa Dkt. Salim anakuwa mwafrika wa kwanza kupewa heshima na tuzo hiyo ya juu katika historia ya China.

Nishani hiyo ilipokelewa na Bi. Maryam Salim, Binti ya Dk. Salim Ahmed Salim ambaye pia ni Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Albania kwa niaba ya Baba yake kutokana na kushindwa kuhudhuria kwa sababu za kiafya. Katika tukio hilo, Serikali ya Tanzania iliwakilisha na Balozi wa Tanzania nchini China Mheshimiwa Mbelwa Kairuki.

Hafla hiyo kubwa ya kitaifa ya kukabidhi nishani ilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa Chama na Serikali ya China akiwemo Makamu wa Rais Mheshimiwa Wang Qishan, Waziri Mkuu Mheshimiwa Li Keqiang, Spika wa Bunge Mheshimiwa Li Zhanshu na Wajumbe wote wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China na Baraza la Taifa.

Mbali na Dk.Salim,  wengine waliotunukiwa Nishani ya Urafiki ni pamoja na Kiongozi wa Chama cha Kikoministi cha Cuba Jenerali Raul Castro, Dada wa Mfalme wa Thailand Maha Chakri Sirindhorn, Kiongozi wa Jumuiya ya Urafiki ya China na Urusi Ndugu Galina Kulikova, Waziri Mkuu Mstaafu wa Ufaransa Jean-Pierre Raffarin na Bi  Isabel Crook  kutoka Canada.

Vilevile  Rais Xi alitoa Nishani  ya Jamhuri na Nishani ya Heshima ya Taifa kwa raia 36 wa China kwa kutambua mchango wao mkubwa katika maendeleo ya Taifa la China kupitia kazi zao katika fani mbalimbali.

Nishani ya Juu ya Urafiki ya Taifa la China imetolewa kwa Dkt. Salim  kutokana na mchango wake wa kuiwezesha Jamhuri ya Watu wa China kuwa Mwanachama wa Umoja wa Mataifa mwaka 1971 alipokuwa Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.  Aidha, mchango wa Dk. Salim katika kuimarisha mahusiano kati ya China na Tanzania wakati aliposhikilia nyadhifa mbalimbali umetajwa kama sababu ya kutunukiwa Nishani hiyo. Vilevile, mchango wa Dk.Salim katika kujenga mahusiano kati ya China na Afrika akiwa na nafasi ya Katibu Mkuu wa OAU umetajwa kuwa sababu nyingine ya kutunukiwa Nishani.

Tukio la Kutoa Nishani limetangazwa moja kwa moja na Televisheni zote za Jamhuri ya Watu wa China na kushuhudiwa na watu zaidi ya Milioni 500.

Kwa mujibu wa maelezo ya Balozi wa Tanzania nchini China Ndugu Mbelwa Kairuki Kupitia tukio la leo, mamilioni ya Wachina hususan vijana wamepata fursa ya kufahamu nafasi na mchango wa Tanzania na Bara la Afrika katika historia ya taifa lao. Aidha, tukio la leo limeifanya Tanzania kufahamika kwa watu wengi zaidi nchini China kupitia tukio mara moja. Hatua hiyo itaamsha udadisi na hamasa miongoni mwa Wachina wengi wa kizazi kipya kutaka kuifahamu zaidi Tanzania. Hali hii yaweza kujitafsiri katika fursa kubwa ya kukua kwa utalii, biashara na wawekezaji ikizingatiwa kuwa  wananchi wa China hutoa mwitikio mkubwa kwa nchi ambazo husemwa vizuri na kuthaminiwa na Serikali yao.

Aidha Balozi Kairuki ameeleza kwamba maadhimisho ya miaka 70 ya Jamhuri ya Watu wa China mwaka huu yanaambatana na maadhimisho ya miaka 55 ya urafiki na udugu kati ya China na Tanzania kufuatia kuanzishwa kwa mahusiano rasmi ya kidiplomasia mwaka 1964. Uhusiano wa China na Tanzania uliotokana na uhusiano mzuri wa waasisi wa mataifa haya mawili, Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Mao Tsetung. Uhusiano huo umeendelezwa na viongozi wa pande zote mbili ambao umekuwa ukiimarika siku hadi siku. Uhusiano huu umekwenda mbali zaidi ya uhusiano kati ya Serikali na Serikali na kushamiri kwa uhusiano wa watu kwa watu.

Ni kwasababu hiyo, katika maadhimisho ya miaka 70 ya Taifa la China, Jumuiya ya Urafiki wa watu wa China na Tanzania ni miongoni mwa Jumuiya za mataifa 17 yenye urafiki wa majira yote na China walioalikwa  kushiriki kwenye maadhimisho hayo na tarehe 1 Oktoba 2019 watakuwa na gwaride lao maalum. Katika jumuiya hizo 17, Kutoka Barani Afrika ni Tanzania na Zambia ndio watahudhuria.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,


Share:

Kabudi: Tanzania tumedhamiria kubadili maisha ya watu wetu

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania Profesa Palamagamba John Kabudi amesema Tanzania imedhamiria kubadili maisha ya wananchi wake ikijitahidi kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu SDGs.

Akihutubia mjadala Mkuu wa Baraza Kuu laUmoja wa Mataifa kikao cha 74 mjini New York Marekani Ijumaa usiku Profesa Kabudi amesema Tanzania imeweka ajenda kuu za kuzitekeleza ambazo ni pamoja na “kutokomeza ufisadi, kurejesha haki na heshma katika sekta za umma, na kuimarisha ukusanyaji kodi kama mbinu ya kufikiwa kwa haraka ukuaji wa kiuchumi." 

Mengine wanayoyapa kipaumbele ni “elimu bora kwa wote, huduma za afya, na uwajibikaji.”

Waziri huyo amesema  hivi juhudi hizo pia zinalenga kuboresha kiwango cha elimu nchini , kutokomeza umasikini, na kukabiliana na kushughulikia tatizo la ajira, uandikishaji watoto wanaoingia shule kimepanda kwa asilimia 35.2 ikiwa imechangiwa na hatua ya serikali ya kutoa elimu bure kwa shule za msingi hadi kitato cha nne.

Hatua zinazochukuliwa
Waziri Kabudi amesema serikali imechukua hatua madhubuti kukabiliana na ufisadi ambazo ni pamoja na “kuanzisha kitengo cha kupambana na uhalifu na ufisadi katika mahakama kuu, na kuimarisha suala la uwajibikaji na uwazi katika serikali. "

Katika miaka minne iliyopita Profesa Kabudi amesema serikali imetekeleza mabadiliko kadhaa yanayojumuisha kudhibiti utajiri na mali asili ya nchi hiyo kwa kupitia mikataba mbalimbali na hatua hizo zitasaidia kuongeza pato la taifa kwa ukusanyaji mapato, pia sheria mpya za madini zimeisaidia Tanzania kukusanya mabilioni ya fedha ambayo yameisaidia serikali kuongeza kiasi cha bajeti yake hadi asilimia 40 mwaka 2019 ukilinganisha na asilia 25 mwaka 2016.

Profesa Kabudi ameongeza kuwa mapato hayo yamesaidia kuboresha miradi mbalimbali ya miundombinu na kuinua hali ya wananchi kuanzia katika afya, maji, na usafi. Hatua hizo pia zimesaida kutoa elimu bure kwa shule za umma za msingi na sekondari akitolea mfani shule za msingi uandikishaji Watoto umeongezeka kwa asilimia 35.2.

Amesema serikali pia inahakikisha uhifadhi mazingira na kujumuisha kila mwananchi katika mchakato wa SDGs ikiwemo makundi yasiyojiweza.

Na katika upande wa nishati ambayo awali ilikuwa ni bidhaa adimu sasa takriban asilimia 67 ya wananchi wa Tanzania wana nishati ya umeme kutokana na mradi maalum wa kusambaza umeme vijijini, REA .

Pia kuna ujenzi wa bwawa kubwa kabisa la kuzalisha umeme unaoendelea  ambao utakuwa  mkombozi sio tu kwa wananchi wa taifa hilo bali hata nchi jirani.

Pia amesema mbali ya uhifadhi wa mazingira kuna masuala mengine yanayozingatiwa ikiwemo nishati endelevu na kuhakikisha teknolojia hiyo inawasaidia mengi.
Uhuru wa vyombo vya habari

Prosesa Kabudi amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika suala la uhuru wa vyombo vya habari na kuongeza kiwango cha utoaji leseni akitolea mfano kwamba taifa hilo lina jumla ya vituo vya redio 152 na ni vitatu tu ndivyo vinamilikiwa na serikali, huku vituo vya televisheni vikiwa 34 na viwili tu ndivyo vinavyomilikiwa na serikali. Kwa upande wa magazeti serikali imetoa jumla ya leseni 172.

Na mwisho ametoa wito kwa nchi zote wanachama kukumbatia ushirikiano wa kimataifa sio tu kwa ajili ya kutomoza umasikini, kuboresha kiwango cha elimu, kukabiliana na mabadiliko yatabianchi na kufikia uwajibikaji bali pia katika kudumisha amani na usalama lakini pia katika kuleta haki na kuwa na dunia bora.


Share:

Waziri Mkuu: Waliokula Fedha Za Maji Wakamatwe

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza kukamatwa na kuwekwa ndani viongozi wa kamati ya watumiaji maji wa mradi wa maji wa Matunguru uliopo katika Kijiji cha Tungamalenga wilayani Iringa kwa tuhuma za ubadhilifu wa sh. milioni saba.

Ametoa agizo hilo jana jioni (Jumamosi, Septemba 28, 2019) baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wakati akihutubia  mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Idodi wilayani Iringa.

Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela afuatilie suala hilo kwa kuwa kamati nyingi za watumiaji maji zimekuwa na tuhuma za matumizi mabaya ya fedha zinazokusanywa kutoka kwa wananchi jambo ambalo si sahihi.

Alisema ifikapo saa 4.00 asubuhi ya leo watuhumiwa wote wanaohusika na ubadhilifu huo wawe wameshakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya dola kwa ajili ya kwenda kujibu tuhuma zinazowakabili.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alisema kwamba Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Iringa hadi Ruaha yenye urefu wa kilomita 104 ili kuboresha huduma za usafiri kwa wakazi wa maeneo hayo na kuinua uchumi.

Waziri Mkuu aliyasema hayo baada ya kupokea malalamiko ya ubovu wa barabara hiyo kutoka kwa mbunge wa jimbo la Ismani, William Lukuvu ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Mbunge huyo alisema licha ya Serikali kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo ikiwemo ya maji, afya na umeme, lakini wanakabiliwa na tatizo la ubovu wa barabara ambapo aliomba Serikali iwasaidie.

Baada ya Waziri Mkuu kusema kuwa Serikali itahakikisha barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami wananchi walifurahi na kuishukuru Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kwa kuwajali wananchi wake.

Awali, Waziri Mkuu alikagua na kuzindua majengo matano ya kituo cha afya Idodi ambayo yamegharimu sh. milioni 400. Pia Serikali iliongeza sh. milioni 300 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba. Waziri Mkuu alisema ameridhishwa na ujenzi wa mradi huo.

Kwa upande waobaadhi ya wagonjwa waliolazwa katika wodi ya Mama na Mtoto ambao walikuwa wajifungua kwa njia ya upasuaji waliishukuru Serikali kwa kuboresha na kusogeza huduma za afya karibu na makazi ya wananchi.

Mmoja wa wagonjwa hao, Agusta Nyagawa alisema awali walikuwa wanalazimika kwenda hadi Iringa mjini kwa ajili ya kufuata huduma za afya lakini kwa sasa huduma hizo zikiwemo za kujifungua pamoja na vipimo wanazipata kituoni hapo.

Naye, Chipe Ngugi alisema anaishukuru Serikali kwa kuwa huduma za afya zimeboreshwa katika hospitali yao ya kata, hivyo hawatalazimika tena kusafiri umbali mrefu hadi Iringa kwa ajili ya kufuata huduma za afya zikiwemo za  upasuaji.

Alisema yeye alijifungua kwa njia ya upasuaji na anawashuwashukuru madaktari na wauguzi  kituoni hapo kwa huduma nzuri ambazo zimeokoa  Maisha yake na mtoto. Aliiomba Serikali iendelee kuboresha huduma kwa kuwa wapo mbali na mjini.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Wakandarasi Mradi Wa Maji Same-mwanga Watakiwa Kuongeza Kasi

Wakandarasi wanaotekeleza mradi wa maji wa Same-Mwanga wametakiwa kuongeza kasi ya utekelezaji wake ili ukamilike kwa wakati.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga ametoa maelekezo hayo Septemba 28, 2019 wakati wa ziara yake iliyolenga kukagua hatua ya ujenzi iliyofikiwa na Wakandarasi wanaotekeleza mradi huo ambao ni kampuni ya M.A Kharafi & Sons na kampuni ya Badr East Africa Enterprises.

Mara baada ya kujionea shughuli zilizokuwa zikiendelea na kupokea taarifa ya mradi kutoka kwa wakandarasi hao, Mhandisi Sanga alieleza kutoridhishwa na kasi ya utekelezwaji wake na aliwasisitiza kuhakikisha kuwa mradi unakamilika kwa wakati.

Mhandisi Sanga aliwataka Wakandarasi kuwa wepesi kwenye kufanya mawasiliano na Wizara kila wanapokutana na changamoto yoyote ambayo ipo nje ya uwezo wao ili ufumbuzi upatikane haraka bila kuchelewesha shughuli za ujenzi wa mradi.

“Sijaridhishwa na kasi yenu ya ujenzi wa mradi. Kama kuna changamoto mnakutana nazo zilizo nje ya uwezo wenu mhakikishe mnawasiliana na Wizara mapema iwezekanavyo ili tupate ufumbuzi,” alisema Mhandisi Sanga.

Aliongeza kwamba Serikali inachohitaji ni kuona matokeo na haipo tayari kumvumilia mkandarasi ambaye anachelewesha mradi bila ya kuwa na sababu za msingi.

“Wanachohitaji wananchi ni maji, Serikali haitomvumilia Mkandarasi ambaye atashindwa kwenda na kasi inayokubalika,” alibainisha Mhandisi Sanga.

Mhandisi Sanga vilevile aliwakumbusha wakandarasi hao kuhakikisha manunuzi ya vifaa vinavyohitajika kwenye ujenzi wa mradi huo yanafanyika hapa nchini badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi hasa ikizingatiwa kwamba vingi vinapatikana hapa hapa Nchini.

Wakandarasi hao kwa nyakati tofauti walimuahidi Naibu Katibu Mkuu Sanga kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi sambamba na kuzingatia maelekezo aliyoyatoa.

Mradi wa Same-Mwanga ni miongoni mwa miradi mikubwa inayotekelezwa na Serikali kwa lengo la kuondoa kero ya maji kwa wakazi wa Miji ya Same na Mwanga, Mkoani Kilimanjaro na baadaye Wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga.

Ziara hiyo ya Naibu Katibu Mkuu Sanga kwenye mradi huo ni ya kwanza tangu ameteuliwa na kuapishwa kushika wadhifa huo Septemba 22, 2019




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger