Askofu Dkt Fredrick Shoo amechaguliwa kwa kipindi kingine cha pili kuwa Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kwa kipindi cha miaka minne .
Dkt. Shoo ametangazwa mshindi usiku wa kuamkia leo dhidi ya wagombea wengine katika uchaguzi huo ambapo ataliongoza kanisa hilo kwa kipindi kingine cha miaka minne (2019-2023).
Askofu Shoo amepata kura 144 huku mshindani wake wa karibu, Dkt. Abednego Keshomshahara akipata kura 74 kati ya kura 218 zilizopigwa katika mzunguko wa mwisho baada ya kubaki wao wawili.
0 comments:
Post a Comment