Friday 20 November 2015

Waziri Mkuu Mteule Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa kuapishwa Leo Saa Nne

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Sherehe za kumuapisha Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu Mteule zitafanyika katika Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 20 Novemba, 2015 kuanzia saa 4.00 Asubuhi.

Sherehe hizo zinafanyika siku moja baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitisha jina lake kwa kura nyingi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufuatia uteuzi uliofanywa na Mhe. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa ratiba ya sherehe hizo, Wageni waalikwa wote wanapaswa kuwasili katika Ikulu ya Chamwino kuanzia majira ya saa mbili asubuhi.

Sherehe hizo zinatarajiwa kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo Marais Wastaafu, Mawaziri Wakuu wastaafu na waheshimiwa wabunge.

Imetolewa na Idara ya Habari MAELEZO

19 Novemba, 2015
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger