
Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Dkt. Hellen Maziku, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanzilishi wa HCD Services Tanzania, amesema mafunzo hayo yanasisitiza umuhimu wa kutumia mtazamo unaomlenga mtumiaji katika kutafuta suluhisho la changamoto ya taarifa potofu.
Amesema mtazamo huo unazingatia mahitaji, matarajio, uzoefu na tabia za wananchi wanaokumbwa na changamoto ya taarifa potofu, hatua inayolenga kuhakikisha suluhisho zinazobuniwa zinakidhi mahitaji halisi ya watumiaji wa taarifa.
Kwa upande wao, washiriki wa mafunzo hayo wamesema yatawasaidia kupata uelewa na mbinu mbalimbali zitakazowasaidia kutambua, kuchambua na kukabiliana na habari potofu na taarifa za upotoshaji katika kazi zao za kila siku.











































































0 comments:
Post a Comment