Wednesday 2 January 2019

DUDU BAYA KUKICHAFUA WASAFI?

Godfrey Tumaini anayefahamika kama Dudu Baya (Konki Masta) jina la kisanii ni miungoni mwa wasanii maarufu na wakongwe zaidi katika muziki wa kizazi kipya (Bongo fleva),pia ni msanii miungoni mwa waanzilishi na wajenzi wa muziki huu ambapo alivuma sana miaka ya 2000 na ngoma zake kali kama nakupenda tu,Mpenzi,nimeondoka na nyimbo zingine kadha wa kadha ambazo zilimuweka na zinaendelea kumuweka kwenye ramani ya muziki mpaka sasa.Lakini nje ya muziki Dudu Baya amejiweka wazi kwamba ni mpinga ushoga namba moja akifikia hatua ya kutaja watu kadhaa ambao alisema wanajihusisha na ushoga.…

Source

Share:

WALIMU NJOMBE WAMFAGILIA RAIS MAGUFULI

Na Amiri kilagalila Mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kutengua Matumizi ya Kikokotoo Kipya kwa Watumishi baada ya Kustaafu Chama Cha Walimu Mkoa wa Njombe kimempongeza Raisi kwa Utenguzi huo kwa kusema kuwa Rais Ametambua Shida wanazopiotia watumishi Mara baada ya Kustaafu. Akizungumza na mtandao huu Ofisini kwa hii Leo Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Mkoa wa Njombe Mekson Wizengo amesema Kwa kufanya Hivyo Raisi amerejesha imani na amani ya Mioyo ya Watumishi wa nchi hii wakiwemo walimu. “Msimamo wa chama cha…

Source

Share:

MSUMBIJI YASEMA WATANZANIA NDIO VIONGOZI WAKUU WA AL-SHABAAB NCHINI HUMO

Maputo, MSUMBIJI. Waendesha Mashitaka nchini Msumbiji wamewataja watu watatu raia wawili wa Tanzania na mmoja wa Afrika Kusini kuwa miongoni mwa makamanda wa kundi la kigaidi la al-Shabaab ambalo hapo awali lililikuwa linajiita Ahlu Sunna Wal Jamaa, linaoendelea kufanya matukio ya uvunjaji wa sheria na mauaji katika mkoa wa Cabo Delgado, kaskazini mwa nchi hiyo. Taarifa ya waendesha mashitaka hao wa Msumbji imesema Andre Mayer Hanekom, raia wa Afrika Kusini na Watanzania Chafim Mussa na Adamu Nhaungwa Yangue, ni miongoni mwa viongozi za ngazi za juu wa genge hilo la…

Source

Share:

SIMBA , AZAM ZAMNYIMA USINGIZI MWINYI ZAHERA

Share:

Picha: MAKAMU WA RAIS BUNGE LA AFRIKA AWAPONGEZA WALIOSHIRIKI MICHUANO YA UVCCM CUP SHINYANGA


Chama cha mapinduzi CCM kata ya Kambarage Mjini Shinyanga kimefanya sherehe ya kuzipongeza timu za vijana za mpira wa miguu, zilizoshiriki katika mashindano ya ya Kombe la Vijana (UVCCM CUP) Wilaya ya Shinyanga 

Sherehe hiyo imefanyika Jumanne , Januari 1, 2019 katika ukumbi wa Shy Villa uliopo kambarage Mjini Shinyanga ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika na Mbunge wa jimbo la Shinyanga Mjini Mh.Stephen Masele. 

Akizungumza wakati wa sherehe hizo Mh. Masele amewapongeza vijana walioshiriki katika michuano ya kombe la Umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) huku akiwataka kuongeza bidii zaidi katika soka ili waweze kuonekana na vilabu vikubwa . 

‘Endeleeni kushirikiana maana mpira wa miguu ni kama siasa ni kazi ya kitimu kwenye siasa huwezi fanikiwa peke yako lazima uende na wenzako, kwa hiyo mkijitahidi hata timu yetu ya stand lazima iweke jicho lake kuangalia wachezaji wa nyumbani’alisema Masele. 

Katika hatua nyingine Mh. Masele amewakumbusha UVCCM kupuuzia maneno ya watu yenye lengo la kuwakatisha tamaa na badala yake waongeze ushirikaiano zaidi katika kufanya kazi . 

‘Msiwe na wasiwasi maneno haya yapo tu siku zote kwa hiyo fanyeni kazi simamie misingi ya chama , ukisikia maneno na ukaendelea kufanya kazi ndio kukomaa huko’ alisema Masele. 

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kambarage Hasan Mwendapole amesema kuwa lengo la kufanya sherehe hiyo ni kuwakutanisha vijana wote walioshiriki katika mashindano hayo ili kujenga umoja na mshikamano ambao utakuwa chachu ya maendeleo katika wilaya ya Shinyanga. 

‘Haya mashindano yamechezwa karibu wiki tatu , kila siku vijana walikuwa wanakutana kwa hiyo unakuwa umewaweka pamoja hata muda wa kutembea hovyo haukuwepo’ alisema Mwendapole 

Mashindano ya kombe la umoja wa vijana wa CCM (UVCCM CUP) yalijumuisha kata zote za Wilaya ya Shinyanga na aliyeibuka kidedea ni timu ya Kata ya Kambarage na kukabidhiwa Ngao, cheti pamoja na Ng’ombe.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Abubakary Mkadam (kushoto) akiteta jambo na Mh. Stephen Masele
Diwani wa Kata ya Kambarage Hassan Mwendapole akisisitiza jambo wakati wa sherehe hizo ambapo amewataka vijana kuendeleza ushirikiano katika michezo ili kuwa chachu ya mendeleo . 
Mwenyekiti wa mashindano hayo BI. Jackline Chacha Amesema lengo la mashindano hayo ni kutekeleza ilani ya chama ,huku akiweka wazi kuwa wameunda timu ya wilaya itakayowahusisha vijana kutoka katika timu zilizoshiriki.
Katibu wa UVCCM wilaya ya Shinyanga Comrade Egobano akisisitiza jambo katika Sherehe hiyo
Andrew Manyonyi Kampteni  wa timu ya Kata ya Kambarage amewaomba wadau wa soka mkoani Shinyanga  kujitokeza kusapoti timu za vijana kwani wanakumbana na changamoto mbalimbali hasa upande wa vifaa vya michezo.

Mbunge wa Shinyanga Mjini Mh. Masele akipokea hati ya pongezi kutokana na mchango wake ndani ya Chama CCM Wilaya ya Shinyanga.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Geoffrey Mwangulumbi akipokea hati ya pongezi kutoka kwa mgeni rasmi Mh. Masele
Mh. Stephen Masele akimkabidhi Comrade Egobano (kushoto)  cheti cha pongezi kutokana na mchango wake kwa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM) Wilaya ya Shinyanga.
Mh.Stephen  Masele akikata Keki katika Sherehe hiyo, kulia ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Abubakary Mkadam na kushoto ni Mwenyekiti CCM kata ya Kambarage Rehema Nhamanilo.

Baadhi ya wachezaji wa Timu ya Kambarage wakiwa eneo la Sherehe wakifuatilia yanayojiri.
Wadau  wa michezo pamoja na wanachama wa CCM wakifuatilia kwa makini kinachoendelea katika Sherehe hizo.
Sherehe inaendelea


.
Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika  na Mbunge wa Shinyanga Mjini Stephen Masele akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa michuano ya UVCCM CUP Wilaya ya Shinyanga  timu kutoka Kata ya Kambarage Mjini Shinyanga.
Picha na Steve Kanyefu- Malunde1 blog
Share:

MHE. MABULA AKAGUA MIRADI YA MAJI YENYE THAMANI YA BI 46.81

Mbunge Jimbo la Nyamagana Mhe. Stanslaus Mabula afanya ziara ya kikazi MWAUWASA “Mwanza Urban Water Supply and Sanitation Authority” *Mamlaka ya maji safi na Maji taka Jijini Mwanza* kukagua miradi saba ya maji inayotekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza yenye thamani ya shilingi 46,810,000,000.00. Mhe. Mabula akiwa MWAUWASA amepokelewa na mwenyeji wake Kaimu Mkurugenzi Mhandisi. Magayane ambaye alipata fursa ya kutoa taarifa ya miradi yote inayotekelezwa na taasis hiyo matharani iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza ikiwemo Ujenzi wa Tank la maji Nyegezi pamoja na ulazaji wake wa…

Source

Share:

JAMII YATAKIWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUIBUA MATUKIO YA UKATILI DHIDI YA WATOTO.

Dodoma. Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto,imewataka wazazi,walezi na jamii kwa ujumla kuzingatia ulinzi wa mtoto ili kutekeleza lengo la la kupunguza matukio ya ukatili kwa silimia 50 ifikapo mwaka 2021!2022. Aidha,wizara hiyo imeitaka jamii kuwa makini na matumizi ya mitandao ya kijamii kwa kuepuka kutuma picha za watoto ambao ni wahanga wa ukatili na kuziweka wazi kinyume cha sheria ya mtoto ya mwaka 2009. Taarifa ya wizara imetolewa leo,baada ya kuwepo kwa taarifa mapema wiki hii juu ya mwalimu mmoja wa shule ya msingi jijini Dodoma,kumfungia mtoto…

Source

Share:

RAIS AL BASHIR ABANWA VIKALI NA WASUDANI, WAAMUA KUANDAMANA KWA MAMIA MJINI KHARTOUM

Khartoum, SUDAN. Maandamano makubwa yamefanyika mwisho wa mwaka 2018 katika mji mkuu wa Sudan Khartoum yakiitikia wito wa baadhi ya vyama vya upinzani na jumuiya za kiraia kwa ajili ya kulalamikia ughali wa maisha na hali mbaya ya uchumi wa nchi hiyo. Waandamanaji hao walikuwa wakielekea katika Ikulu ya Rais mjini Khartoum wakati walipokabiliwa na vyombo vya usalama vilivyolazimika kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji hao waliokuwa wakipiga kelele dhidi ya serikali ya Rais Omar Hassan al-Bashir. Waandamanaji wengi walikuwa wamebeba mabango na maberamu yenye maandishi yasemayo ‘Irhal’ yaani…

Source

Share:

DRC:HUDUMA YA INTANETI NA KUTUMA SMS YAKATWA GHAFLA MPAKA MATOKEO YA UCHAGUZI YATAKAPOTANGAZWA.

Kinshasa, DRC. Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imekata huduma ya intaneti na ujumbe wa mfupi wa simu za mkononi (SMS) kote nchini humo kwa siku ya tatu mfululizo hii leo wakati nchi hiyo ikisubiri kwa hamu kubwa matokeo ya kwanza ya uchaguzi wa Rais. Hali hii imetokea kuanzia juzi Desemba 31 kufuatia uchaguzi wa Rais nchini humo, uliofanyika Jumapili iliyopita, huku baadhi ya mikoa ikigubikwa na ghasia na machafuko. Pande mbili za upinzani na muungano wa chama tawala hapo juzi (Desemba 31) zilieleza kuwa, zinaelekea kuibuka na…

Source

Share:

WAWILI WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUHUJUMU UCHUMI

Na, Naomi Milton Serengeti Mongatoni Sururu(49) na Mashaka Machemba(33) wakazi wa Kijiji cha Mihale wilayani Bunda Mkoani Mara wamefikishwa mbele ya mahakama ya wilaya ya Serengeti kujibu mashtaka yao katika kesi ya Uhujumu Uchumi namba 1/2019 Akisoma mashtaka mbele ya Hakimu mkazi Felix Ginene mwendesha mashtaka wa Jamhuri Faru Mayengela alisema washitakiwa hao wanashitakiwa kwa makosa mawili kosa la kwanza ni kuingia ndani ya pori la Akiba kinyume na kifungu 15(1)(2)cha sheria ya wanyamapori namba 5/2009 Kosa la pili ni kupatikana na silaha ndani ya hifadhi kinyume na kifungu 17(1)(2)…

Source

Share:

RAIS ESSEBSI ATOA SALAMU ZA MWAKA 2019 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Tunis, TUNISIA. Rais wa Tunisia, Beji Caid Essebsi, amezungumzia uchaguzi ujao wa rais na bunge nchini humo na kusema kuwa mwaka 2019 utakuwa mwaka muhimu kwa nchi hiyo. katika ujumbe wake mwaka mpya wa 2019, Rais Essebsi ameeleza kuwa jitihada kubwa zinapaswa kufanyika kuandaa mazingira bora ya kufanyika uchaguzi wa wazi, huru na wa kidemokrasia katika mwaka huu wa 2019. Aidha, Kiongozi huyo amewataka wananchi wa nchi hiyo kutumia haki yao ya kikatiba na kushiriki kwenye chaguzi hizo, ambapo amewataka Watunisia kuwachagua watu wanaofaa kwa ajili ya kushika nyadhifa za…

Source

Share:

IRENE UWOYA AMWAGA MACHOZI USIKU WA MWAKA MPYA

Rasmi ni mwaka 2019 ikiwa ni siku ya kwanza sehemu mbalimbali ulimwenguni sherehe zinaendelea huku kila mtu akiwa na matumaini yake katika maisha. Kutoka kiwanda cha filamu Bongo wasanii mbalimbali wameupokea mwaka mpya (2019) kwa hisia tofauti tofauti.Wengine wameupokea kawaida huku wengine wakiupokea kwa matumaini mengi wakiamini kwamba inaweza kuwa nafasi ya wao kurekebisha ama kusonga mbele zaidi katika mihanagaiko yao Msanii mrembo na mwenye mvuto wakutosha Irene Uwoya yeye ameupokea kitofauti kabisa mwaka mpya usiku wakuamkia leo.Tofauti na matarajio ya wengi ambao walimuona na kuamini kwamba Irene alikuwa na…

Source

Share:

MSIOMBE RUSHWA WANAOTAKA VITAMBULISHO VYA MAGUFULI


Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa, Dk Halfany Haule amewataka watumishi na wenye viti wa serikali za mitaa Manispaa ya Sumbawanga, wajiepushe na visa vya kuomba rushwa wanapopitisha barua za wajasiriamali, wanaoomba vitambulisho maalumu vilivyotolewa na Rais John Magufuli.

Aidha, amewataka wajasiriamali wadogo wakiwemo machinga waliopewa na watakaopewa vitambulisho hivyo maalumu, wasivitumie kama tiketi ya kuvunja sheria na kukiuka maelekezo ya serikali.

Hayo yamebainishwa na Dk Haule wakati wa kuwagawia wajasiriamali wadogo wa manispaa hiyo vitambulisho maalumu. 

Alisema miongoni mwa watakaopewa ni machinga na waganga wa tiba asili waliosajiliwa. Wilaya ya Sumbawanga kiutawala ina halmashauri mbili za wilaya ya Sumbawanga na manispaa ya Sumbawanga, ambapo kila moja imepewa vitambulisho 6,250.

“Wenyeviti wa serikali za mitaa msijihusishe kuomba rushwa ili kupitisha barua za wajasiriamali wadogo za utambulisho ambao wana sifa ya kupewa... wanapofika kwenye ofisi hizo wasiombwe rushwa na wapitishiwe barua zao za utambulisho bila kutoa hata senti tano watakaobainika watachukuliwa hatua kali za kinidhamu na kihalifu,” alionya.

 Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga, Jacob Mtalitinya alitaja sifa za wajasiriamali ambao watapewa vitambulisho hivyo kuwa ni kuwa na mtaji wa biashara usiozidi Sh milioni nne, wasiwe wamesajiliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na pia watalipa Sh 20,000, ikiwa ni gharama ya kitambulisho.

“Niwahakikishie kila mwananchi mwenye sifa atapata kitambulisho... nawaasa wawe waaminifu katika kutoa taarifa zao waepuke kudanganya kwa kuwa ni kosa pia,” alibainisha.
 
Aliwataka wajasiriamali wadogo watakaopewa vitambulisho hivyo, wahakikishe wanavivaa ili wasibughudhiwe.

Petro Makasa ambaye ni baba lishe aliyepatiwa kitambulisho chake, alimshukuru Rais Magufuli kwa nia yake njema kufanya jambo hilo kubwa huku akisisitiza azidi kubarikiwa.

 “Niwaombe wajasiriamali wadogo wenye sifa wasipoteze nafasi hii wala wasipuuzie wajitokeze kwa wingi kuviomba,” alieleza Makasa. 

Christina Mtawa anayemiliki saluni ya kike alisema, “Hatua hii ya serikali ya awamu ya tano ni ya kupongezwa sana hakika sasa tutapumzika na usumbufu wa maofisa wa TRA,” alisema Makasa.

Peti Siyame, Sumbawanga
 
Chanzo - Habarileo
Share:

CHELSEA YAMSAJILI MSHAMBULIAJI KINDA WA DORTMUND


Klabu ya Chelsea imemsaini mshambuliaji wa Borussia Dortmund Christian Pulisic kwa dau la Yuro 64m lakini itamtoa kwa mkopo kwa klabu hiyo ya Ujerumani hadi mwisho wa msimu.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 raia wa Marekani , ambaye alikuwa amehusishwa na vilabu vya Liverpool na Arsenal , alijiunga na Dortumund akiwa mchezaji mchanga 2015.

Pulisic amefunga magoli tisa katika mechi 23 akiichezea Marekani.

''Ilikuwa ndoto ya Christian kujiunga na ligi ya Uingereza'' , alisema mkurugenzi wa klabu ya Dortmund Michaek Zorc.

Hiyo ni kutokana na mizizi yake ya Marekani na kutokana na hilo tulishindwa kuongeza mkataba wake.

''Kutokana na hali hiyo tumekubali ombi zuri la Chelsea''.

Kandarasi ya Pulisic katika klabu ya Dortmund ilitarajiwa kukamilika kufikia 2020.
Share:

KATIBU MKUU AWATAKA WATANZANIA KUJIANDAA KUIPOKEA SERIKALI MPYA YA CHADEMA 2020


Katibu Mkuu wa Chama cha Deokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Vicent Mashinji amewataka watanzania pamoja na dunia kujiandaa kuipokea serikali mpya chini ya chama anachokiongoza.


Dkt. Mashinji ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter, akisisitiza wananchi kuielewa na kuipokea sera mbadala ya chama hicho.

"Pokeeni Sera Mbadala na jiandaeni kuipokea Serikali mpya inayoongozwa na CHADEMA baada ya October 25, 2020," amesema Dkt. Mashinji.

Aidha kiongozi huyo ametoa ujumbe kwa watu wasiopenda siasa kwa kuwakumbusha kwamba siasa ni utaratibu mzima wa kufanya maaamuzi katika jamii hivyo waipende na wasiichukie.

"Wasiopenda siasa, waambieni hivi “siasa ni utaratibu mzima wa kufanya maamzi katika jamii au kundi fulani la watu ikiwemo familia, na pili, ni matumizi ya mamlaka katika kutekeleza maamzi hayo. Tafadhari Watanzania wenzangu tuipende, tuifanye na tuiishi Siasa" Dkt. Mashinji.

Share:

RAIS MAGUFULI AWAUMBUA VIONGOZI WANAOSINGIZIA 'NI MAAGIZO KUTOKA JUU'

Rais John Magufuli juzi usiku alitoa salamu za mwaka mpya wa 2019 kwa kuhoji tabia ya watumishi wa umma kutojiamini katika utendaji wao wa kazi kiasi cha kila jambo wanalolifanya kudai kuwa “ni maagizo kutoka juu”, akisema neno hilo sasa limekuwa kama ugonjwa.

Kauli hiyo ya Rais imekuja kipindi ambacho watendaji mbalimbali serikalini wamekuwa wakitumia neno hilo katika utekelezaji wa majukumu yao, hasa masuala yanayowahusu wananchi.

Akizungumza dakika chache kabla ya kufika saa 6:00 usiku juzi, Rais Magufuli alisema, “Na mara nyingi maagizo yanakuwa hayapo, bali ni utekelezaji wa wajibu wa sheria, wajiamini na wasiwaonee watu lakini watimize wajibu wao.”

Mbali na kuwataka watendaji serikalini kujiamini, Rais Magufuli alisema mwaka huu utakuwa wa mafanikio zaidi kiuchumi na kuwataka Watanzania kudumisha amani, upendo, umoja na mshikamano.

“Ujumbe wangu kwa watumishi wa umma, ni kama nilivyotoa ujumbe kwa Watanzania wengine, wachape kazi, wajiamini,” alisema Rais Magufuli na kuongeza:


“Waachane na utamaduni wa kila kitu wanachokifanya kudai ni maagizo kutoka juu, huo ni ugonjwa ambao umeanza kuwapata watumishi wa umma ambapo kila wanalolifanya hata kama ni kwa mujibu wa sheria hawataki kujiamini, na wanasema hili ni maagizo kutoka juu.”



Via Mwananchi
Share:

TETESI ZA SOKA ULAYA , INTER MILAN WAMTAMANI ASHLEY YOUNG

Inter Milan wanamnyatia beki kamili wa Manchester United Ashley Young, 33, na wanatumai kwamba wataweza kumchukua bila kulipa ada yoyote mwisho wa msimu baada ya mkataba wake kumalizika. (Mirror)

Meneja Unai Emery amesema Arsenal bado hawajazungumzia uwezekano wa kumnunua beki wa kati wa Chelsea Gary Cahill, 33, Januari. (Football.London)

Lakini meneja wa Fulham Claudio Ranieri amekuwa wakimtaka Cahill akitumai kumtumia kuimarisha safu yake ya ulinzi Craven Cottage. Anamtaka kwa mkopo wa miezi sita. (The Sun)

Emery amefahamishwa kwamba Arsenal hawataunga mkono mpango wake wa kutaka kuwarejesha Calum Chambers, 23, na Reiss Nelson, 19, mwezi huu. Wawili hao wako nje kwa mkopo. (Metro)Gary Cahill

Chelsea wanakariiba sana kukamilisha usajili wa kiungo wa kati Mmarekani Christian Pulisic, 20, kwa £45m kutoka Borussia Dortmund. (Express)
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger