Friday 28 March 2014

Siri ya CCM kung’ang’ania Serikali mbili kikatiba

Siri ya CCM kung’ang’ania Serikali mbili kikatiba

 

  • Msimamo huo ni kinyume na mapendekezo au matakwa ya wengi kama ilivyoainishwa kwenye Rasimu ya Pili ya Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba


Katika maisha ya kawaida, binadamu ana msimamo wake na hata uamuzi  asiopenda ubadilike.
Katika medani ya siasa nchini msimamo wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) kuhusu Muungano na muundo  unafahamika. Ni muundo wa kutaka  Serikali mbili ambao chama hicho unakipigania kwa udi na uvumba.
Hata hivyo, msimamo huo ni kinyume na mapendekezo au matakwa ya wengi kama ilivyoainishwa kwenye Rasimu ya Pili ya Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
 Tume hiyo iliyokuwa chini ya Jaji Joseph Warioba ilikusanya maoni ya wananchi na ilipendekeza muundo wa Muungano wa Serikali tatu.
Hivi karibuni akifungua Bunge Maalumu la Katiba, Rais Jakaya Kikwete akaunga mkono msimamo wa chama chake, jambo lililoibua mjadala unaoendelea hadi sasa.
Hoja ya Serikali mbili
Kwanini CCM wanataka Serikali mbili na siyo tatu au moja kama ilivyo maoni ya wananchi walio wengi kwa mujibu wa maelezo ya Tume ya Warioba? Makala haya yanachambua hoja hiyo.
 Profesa Bakar Mohammed ni Mhadhiri Mwandamizi na Mkuu wa Idara ya Siasa na Utawala ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anayesema msimamo wa CCM wa kudai Serikali mbili unatokana na hofu ya uhafidhina wa kuogopa mabadiliko.
Anasema viongozi wengi wa CCM wanasumbuliwa na hofu na woga wa mabadiliko na kwamba wanakuwa wagumu kuyakubali  yanapotaka kutokea.
“Kama mtu unaangalia madaraka zaidi, lazima kunakuwa na woga, na hii ni hulka ya binadamu kuwa na woga wa kuacha kile ulichokizoea… Lakini ukiangalia masilahi ya nchi na kuacha yale yanayokusukuma kusingekuwa na wasiwasi huu unaoonekana sasa,” anasema.
Anasema CCM inachofanya ni kuhakikisha haking’oki madarakani, huku viongozi wake wakiamini kuwa wana sifa za kuongoza na siyo wengineo.
Profesa Bakari anailinganisha hofu ya sasa ya CCM na ile waliyokuwa nayo viongozi wa chama hicho miaka ya 1990 zilipoanza vuguvugu za mabadiliko ya siasa za vyama vingi. Anasema CCM kiliendesha propaganda kuwa mfumo wa vyama vingi haukuwa na tija na ungeleta vita.
Share:

VIDEO:SPKA AKIONYA VURUGU NDANI YA BUNGE LA KATIBA


Share:

Seif: Hatuko tayari kujadili serikali mbili


Zanzibar. Makamu wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amesema chama chake cha CUF hakiko tayari kujadili mfumo wa Muungano wa serikali mbili kama inavyotetewa na wabunge wa CCM na Rais Jakaya Kikwete.

Amesema tayari amewaandikia barua Rais Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kuwaeleza juu ya msimamo huo.
Maalim Seif alitoa msimamo huo jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kibandamaiti mjini Unguja.
Isitoshe, alisema CUF imebaini kuwa kuna njama za kufuta kipengele katika Katiba ya Zanzibar kinachosema; “Zanzibar ni nchi” na kwamba hiyo ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu kwa kuwa Wazanzibari kamwe hawatakubali kufanya hivyo.
Maalim Seif alisema haikuwa mwafaka kwa Rais Kikwete kukosoa mapendekezo ya Rasimu ya Katiba yanayotaka mfumo wa Muungano kuwa wa serikali tatu.
Alisema Jaji Warioba aliweka kando itikadi yake ya CCM katika utendaji wake kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kuja na uamuzi huo kwa vile ndiyo tiba ya kero za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
“Mapendekezo yaliyowasilishwa na Jaji Warioba hayakuwa maoni yake, yale ni maoni ya wananchi, Tanganyika imevaa koti la Muungano, ametoa ushahidi wake ili kujenga mwafaka katika kuendeleza Muungano wenye mfumo wa serikali tatu,” alisema Maalim Seif.
Alisema Muungano wa serikali mbili hauvumiliki na kama kuna watu wanaendelea kuutetea mfumo huo, Zanzibar inaweza kutumia sheria yake ya kura ya maoni kuwauliza wananchi wanaotaka na wasiotaka jambo hilo.
“Nimemwandikia barua Rais Kikwete, nakala nimempelekea Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, Tanzania Bara wanataka Zanzibar iondoe kifungu cha Katiba kinachosema Zanzibar ni nchi, jambo hilo halitapita...tutafanya kampeni wananchi walikatae,” alieleza Katibu Mkuu huyo wa CUF.
Alisema ni jambo la kusikitisha katika hotuba yake alijisahau kama ni mkuu wa nchi na analihutubia Bunge Maalumu badala yake akaegemea kuwa mwenyekiti wa CCM.
Alisema haikuwa sahihi kutoa vitisho na kutaja ikiwa Serikali ya Muungano chini ya Serikali tatu italegalega, jeshi litachukua madaraka ya nchi.
“Rafiki na ndugu yangu Kikwete, usifikiri huu ni wakati ule wa Julius Nyerere, akisema yeye hakuna wa kumpinga. Mambo yamebadilika, usijifanye ni Nyerere mpya, hakuna atakayekusikiliza na kubabaika,” alisisitiza Maalim Seif.
Share:

ROSE NDAUKA ADAIWA KUMTIBULIA DILI BATULI

ROSE NDAUKA ADAIWA KUMTIBULIA DILI BATULI


Akizungumza na Ijumaa kwa sharti la kutotajwa jina lake, chanzo kilisema, wazo la project ile alikuwa nalo Batuli lakini Rose akaingilia kati, hali iliyosababisha Batuli amnunie mwenzake.…


Mastaa wawili, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ na Rose Ndauka wamedaiwa kuwa kwenye bifu chanzo kikidaiwa ni Rose kumtibulia mwenzake dili la ile project ya kusafisha jiji iliyofanyika hivi karibuni.
Malkia wa filamu za kibongo, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’.
Akizungumza na Ijumaa kwa sharti la kutotajwa jina lake, chanzo kilisema, wazo la project ile alikuwa nalo Batuli lakini Rose akaingilia kati, hali iliyosababisha Batuli amnunie mwenzake.
Staa wa filamu za kibongo Rose Ndauka
Alipopigiwa Batuli kwanza aling’aka lakini akasema hapendi kuzungumzia mambo hayo kwani yameshapita huku Rose akieleza kuwa, wazo la project hiyo alikuwa nalo kabla hajajifungua hivyo haoni kama kamtibulia Batuli dili lake.

Share:

HIVI NDIVYO MVUA ILIVYOHARIBU MAZINGIRA JIJINI DAR

HIVI NDIVYO MVUA ILIVYOHARIBU MAZINGIRA JIJINI DAR

    Mwavuli unaotumiwa na wafanyabiashara wadogowadogo  ukiwa umechukuliwa na maji na kutumbukia kwenye shimo eneo la stendi ya mabasi Ubungo.
         Maji yakiwa yametuhama…
    Mwavuli unaotumiwa na wafanyabiashara wadogowadogo  ukiwa umechukuliwa na maji na kutumbukia kwenye shimo eneo la stendi ya mabasi Ubungo.
         Maji yakiwa yametuhama kwenye shimo stendi ya mabasi Ubungo.
Mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia jana na leo imesababisha maafa kwenye baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es Salaam ambapo katika mizunguko ya  kamera yetu  imenasa  eneo la nje ya stendi ya Mkoa, Ubungo maji yakiwa yamejaa kila  pande huku wafanyabiashara wadogo wanaofanyia kazi eneo hilo, miavuli yao na vitendea kazi vikisombwa na maji huku mashimo yaliyokuwa yamechibwa katika utengenezaji wa barabara yakizidi kuporomoka.

Share:

Friday 21 March 2014

RAIS KIKWETE AKIHUTUBIA BUNGE HII LEO


Hii ni kutokana na mwaliko wa mwenyekiti wa bunge Samwel sitta
Share:

RAIS KIKWETE AKIHUTUBIA BUNGE HII LEO


Hii ni kutokana na mwaliko wa mwenyekiti wa bunge Samwel sitta
Share:

WAALIMU BINZA SHULE YA MSINGI,WAKANA KUWAZOMEA WALIMU WA SHANWA SHULE YA MSINGI


WAALIMU  BINZA SHULE YA MSINGI, WAKANA KUWAZOMEA WAALIMU WA SHULE YA MSINGI SHANWA KATIKA WILAYA YA MASWA

Waalimu wa shule ya Msingi katika Wilaya ya Maswa wamekanusha vikali juu kudaiwa kuwazomea  Waalimu wenzao wa shule ya Msingi Shanwa zote zikiwa katika Mji mdogo wa Maswa

Kwa mujibu wa Mwalimu mkuu msaidizi Shule ya msingi Binza Bibi Iviri Swai alisema kuwa Ofisi yake pamoja na Walimu wenzake wamesikitishwa mno na taarifa zilizo andikwa na gazeti la Tanzainia daima la Feburuari 12,2014 toleo Namba 3357 kuwa si za kweli hata kidogo jambo hilo halipo shuleni kwake

Mwalimu Swai katika maelezo yake kwa mwandishi habari hizi alisema kuwa anachofahamu ujio wa Afisa Elimu msingi kufika katika shuleni yake  alikuwa na ujumbe wa kuwaeleza Walimu wa Shule ya Binza na Shanwa juu ya ujio wa Rais Jakaya Kikwete katika Wilaya Maswa wala hapakuwa na maelekezo mengine

Aidha alipo ulizwa mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Shanwa Gilda Gogadi yeye kwa upande wake alisema amesikitishwa na taarifa hizo zilizo andikwa  na gazetii la Tanzania daima kuwa zilikuwa na lengo la kuwachonganisha kati uongozi wa shule ya msingi Binza na Shule yake ya Shanwa

“Inawezekana mwadishi huyu hana madili ya uandishi wa habari na si dhani kama ni Mwandishi wa habari anaye fahamu wajibu wake huyu ni mzushi na kama ameshindwa kazi ya uandishi wa habari atafute kazi ingine au akandikie magazeti ya udaku hayo ndiyo kazi yake umbeya na uzushi tu”alisema Mwalimu Gogadi

“Hata hivyo pamoja na kuandika habari za uongo na kumchafua Afisa Elimu wetu ambaye kimsingi bado ni mgeni katika Wilaya Maswa si kwamba ametuchafua sisi hiyo amewachafua Walimu wote wa Halimashauri ya Maswa na Jamii nzima”alisema Gogadi

Kwa upande wake Afisa Elimu katika Halimashauri ya Wilaya ya Maswa  Mabeyo Bujimu  aliyehamia kutoka Halimashauri ya Kibondo mkoani Kigoma alisema kuwa kazi yake ni kusimamia taaluma na Waalimu wote wa Shule za Msingi katika Halimashauri ya Wilaya ya Maswa na Si vingenevyo

Bujimu alibainisha zaidi kwamba kitendo cha kuandikwa na baadhi ya vyombo vya habari hususani gazeti la Tanzania Daima ni kitendo cha kutaka kumdalisha na kudalisha  taaluma ya elimu kwa ujumla “sisi Wataalamu[Walimu]hatuko katika majukwa ya kisiasa kazi yetu ni moja kuelimisha watoto basi”alisisitiza Bujimu

“ Hivi mwandishi kwa uelewa wako mimiDEO mzima] nitoe magizo kwa Walimu wa  Binza wakazomee Walimu wa Shanwa nimeanza jana kazi ya ualimu?huyu mwandishi  ana elimu ndogo yupo yupo tu nenda katika shule zote mbili Binza na Shanwa ukweli utaupata huko”alisema kwa kujiamini  Bujimu.


                       
Share:


WAALIMU  BINZA SHULE YA MSINGI, WAKANA KUWAZOMEA WAALIMU WA SHULE YA MSINGI SHANWA KATIKA WILAYA YA MASWA

Waalimu wa shule ya Msingi katika Wilaya ya Maswa wamekanusha vikali juu kudaiwa kuwazomea  Waalimu wenzao wa shule ya Msingi Shanwa zote zikiwa katika Mji mdogo wa Maswa

Kwa mujibu wa Mwalimu mkuu msaidizi Shule ya msingi Binza Bibi Iviri Swai alisema kuwa Ofisi yake pamoja na Walimu wenzake wamesikitishwa mno na taarifa zilizo andikwa na gazeti la Tanzainia daima la Feburuari 12,2014 toleo Namba 3357 kuwa si za kweli hata kidogo jambo hilo halipo shuleni kwake

Mwalimu Swai katika maelezo yake kwa mwandishi habari hizi alisema kuwa anachofahamu ujio wa Afisa Elimu msingi kufika katika shuleni yake  alikuwa na ujumbe wa kuwaeleza Walimu wa Shule ya Binza na Shanwa juu ya ujio wa Rais Jakaya Kikwete katika Wilaya Maswa wala hapakuwa na maelekezo mengine

Aidha alipo ulizwa mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Shanwa Gilda Gogadi yeye kwa upande wake alisema amesikitishwa na taarifa hizo zilizo andikwa  na gazetii la Tanzania daima kuwa zilikuwa na lengo la kuwachonganisha kati uongozi wa shule ya msingi Binza na Shule yake ya Shanwa

“Inawezekana mwadishi huyu hana madili ya uandishi wa habari na si dhani kama ni Mwandishi wa habari anaye fahamu wajibu wake huyu ni mzushi na kama ameshindwa kazi ya uandishi wa habari atafute kazi ingine au akandikie magazeti ya udaku hayo ndiyo kazi yake umbeya na uzushi tu”alisema Mwalimu Gogadi

“Hata hivyo pamoja na kuandika habari za uongo na kumchafua Afisa Elimu wetu ambaye kimsingi bado ni mgeni katika Wilaya Maswa si kwamba ametuchafua sisi hiyo amewachafua Walimu wote wa Halimashauri ya Maswa na Jamii nzima”alisema Gogadi

Kwa upande wake Afisa Elimu katika Halimashauri ya Wilaya ya Maswa  Mabeyo Bujimu  aliyehamia kutoka Halimashauri ya Kibondo mkoani Kigoma alisema kuwa kazi yake ni kusimamia taaluma na Waalimu wote wa Shule za Msingi katika Halimashauri ya Wilaya ya Maswa na Si vingenevyo

Bujimu alibainisha zaidi kwamba kitendo cha kuandikwa na baadhi ya vyombo vya habari hususani gazeti la Tanzania Daima ni kitendo cha kutaka kumdalisha na kudalisha  taaluma ya elimu kwa ujumla “sisi Wataalamu[Walimu]hatuko katika majukwa ya kisiasa kazi yetu ni moja kuelimisha watoto basi”alisisitiza Bujimu

“ Hivi mwandishi kwa uelewa wako mimiDEO mzima] nitoe magizo kwa Walimu wa  Binza wakazomee Walimu wa Shanwa nimeanza jana kazi ya ualimu?huyu mwandishi  ana elimu ndogo yupo yupo tu nenda katika shule zote mbili Binza na Shanwa ukweli utaupata huko”alisema kwa kujiamini  Bujimu

Mwandishi wa habari hizi alipo hojiana na baadhi ya Waalimu kutoka Shule ya msingi Binza na Shanwa ambao  majina yao yame[ hifadhiwa] kwa kwa sasa kwa nyakati tofauti walisema wanatarajia kuitisha kikao kwa shule zote mbili [Shanwa na Binza] ili kutoa tamko lao hatua za kuchukua dhidi ya Mwandishi wa habari na na chombo anacho andikia.

                       
Share:

Thursday 13 March 2014

DOGO JANJA WAVUNJA UCHUMBA WA MTU MTWARA

DOGO JANJA, ASLAY WAVUNJA UCHUMBA WA MTU MTWARA

Na Chande Abdallah na Nyemo Chilongani
MADOGO wanaotikisa katika ulimwengu wa muziki Bongo, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ na Asilahi Isihaka ‘Aslay’ wamedaiwa kuvunja uchumba wa jamaa aliyefahamika kwa jina la Fikiri Chodas na Farida.
Asilahi Isihaka ‘Aslay’.
Tukio hilo lilitokea usiku wa Machi 7, mwaka huu, Newala mkoani Mtwara wakati wasanii hao walipokuwa wamekwenda kufanya ziara ya kimuziki.
Kwa mujibu wa chanzo makini, baada ya madogo hao kufanya shoo kali mjini humo, Farida aliwang’ang’ania wasanii hao waliokuwa wakijiandaa kwenda kulala katika hoteli waliyofikia ndipo Fikiri alipokasirika.
Uvumilivu ulimshinda Fikiri, akamvaa Dogo Janja na kumtaka aachane na mpenzi wake, mchumba wake huyo naye akaja juu na kuhamia kwa Aslay ndipo vurugu ilipotokea ambapo Fikiri alihangaika kumkwida ili kumuokoa mpenzi wake asiondoke na wasanii hao.
Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’.
Kuonesha mwanamke huyo alikuwa ‘amekolea’ kwa wasanii hao, alianza kumporomoshea mpenzi wake matusi ya nguoni na kudai amuache kwani ‘wametembea’ naye siku moja tu.
Fikiri alipoona mpenzi wake huyo anamkana, aliamua kutangaza kummwaga papo hapo.
Jitihada za mapaparazi wetu kufuatilia sakata hilo kwa undani zilizaa matunda baada ya kufanikiwa kunasa video ya timbwili hilo (litarushwa hewani kupitia Global Online TV).
Mapaparazi wetu walimtafuta Dogo Janja kwa njia ya simu, alipopatikana alifunguka:
“Kweli siku ile tulipomaliza shoo tu tulimuona huyo demu (Farida) anakuja kwetu. Ghafla jamaa akatokea na kuanza kugombana. Sisi tuliondoka sasa kama jamaa kamuacha mpenzi wake ni yeye mwenyewe, sisi hatukuondoka naye,” alisema Dogo Janja.
Share:

ALI KIBA KUTISHIWA KUUAWA, DIAMOND KUHOJIWA POLISI

ALI KIBA KUTISHIWA KUUAWA, DIAMOND KUHOJIWA POLISI


SAKATA la staa wa Bongo Fleva, Ally Saleh ‘Ali Kiba’ kunusurika kuuawa na watu wasiojulikana kwa kutumia bastola limechukua sura mpya, safari hii, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amefunguka kuwa amejiandaa kuhojiwa na polisi.
Ally Saleh ‘Ali Kiba’.
Kwa mujibu wa chanzo chetu katika jeshi hilo jijini Dar, Diamond ambaye amekuwa akitajwa sana katika sakata hilo kupitia mitandao ya kijamii ataitwa kuhojiwa.
“Unajua ile kesi ipo hapa Central, awali ilitokea Polisi Msimbazi, sasa mpelelezi wake amekuwa akifikiria kumwita Diamond ili amhoji maana anatajwa sana,” kilisema chanzo hicho.
Hivi karibuni, Ali Kiba alivamiwa usiku na watu zaidi ya watano nyumbani kwao, Kariakoo jijini Dar ambapo waliruka ukuta na kuingia ndani huku kila mmoja akiwa na bastola.
Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Ilidaiwa kuwa, mmoja kati ya watu hao ambao ilisemekana walitumwa kumuua msanii huyo, aliibua mzozo wa makusudi kwa wenzake ili kumpa mwanya Kiba kutoroka kwa vile hakufurahishwa na kitendo hicho.
Habari zinasema walipoingia ndani huku kelele za mbwa zikasaidia kumshtua staa huyo, ule mzozo ulioanzishwa na wavamizi hao ulimsaidia Kiba kutoroka ingawa walimkosakosa risasi.
Ikasemekana baada ya msanii huyo kukimbia, jamaa ambaye alimkingia kifua alimpigia simu na kumfungukia watu waliohusika huku ikidaiwa kuwa baadhi yao ni mastaa wenzake.
“Alinitajia tu majina lakini nilishindwa kuthibitisha moja kwa moja hivyo nikayafikisha Kituo Kikuu cha  Polisi (Central) kwa ajili ya uchunguzi,” alisema Ali Kiba huku akikataa kutaja hata jina moja.
Hata hivyo, mengine yaliibuka hasa kwenye mitandao ya kijamii kuwa, miongoni mwa wasanii waliohusika katika tukio hilo eti ni na Diamond.
Amani lilimsaka afande mmoja ambaye anajua mwenendo wa kesi hiyo ambaye alikiri kesi hiyo kuwepo Central lakini alisema mambo yote ni siri ya kazi.
“Nani atahojiwa, nani hatahojiwa ni siri ya kazi yetu,” alisema.
Juzi, paparazi wetu walimtafuta staa huyo wa Wimbo wa Number One ili kusikia anazungumziaje manenomaneno hayo ya kwenye mitandao na vinywa vya watu.
“Nimeshasikia nikitajwa katika hilo, kimsingi ni madai mazito lakini mimi nipo tayari kuhojiwa ili sheria ichukue mkondo wake kwani najua si kweli na sijui lolote,” alisema Diamond.
Akandelea: “Mimi na Kiba kuna ugomvi gani hadi nifikie hatua hiyo. Kwanza sina moyo wala uwezo wa kufanya hivyo.”
Share:

AUNT ,WEMA WALA KICHAPO


KIMEWAKA! Habari zilizothibitishwa zinaeleza kuwa, sura mbili za mauzo kwenye sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu na Aunt Ezekiel Grayson wanadaiwa kula kichapo kutoka kwa msanii mwenzao, Adam Kuambiana, Amani limeinyaka.
Wema Sepetu.
Tukio hilo lililoshuhudiwa na ‘shushushu’ wetu lilijiri mchana kweupe maeneo ya Mikocheni, Dar, hivi karibuni baada ya kuibuka timbwili lenye ujazo wa kilo kadhaa baina ya mastaa hao.
ALIANZA WEMA
Kwa mujibu wa chanzo, Wema ndiye aliyeanza kummwagia Kuambiana maneno ya shombo akimwambia kuwa ahakikishe siku hiyo haipiti bila kukata kucha za miguuni kwani ni ndefu na zinatisha.
“Mwanzoni ilikuwa kama utani tu. Wema alimwambia Kuambiana akate kucha, tena itabidi atumie mkasi wa kukatia michongoma maana kwa wembe hazikatiki.
Aunt Ezekiel.
“Pia Wema alimwambia yeye hawezi kumwacha mpenzi wake na kucha ndefu kama hizo za Kuambiana,” kilisema chanzo chetu.
Ilizidi kudaiwa kwamba wakati Wema akiendelea ‘kumpaka’ Kuambiana, Aunt aliyekuwa amejilaza chini alidakia na kusikika akisema kuwa ni kweli msanii huyo mwenye uwezo wa juu katika fani anatakiwa kukata kucha hizo huku akizungumza maneno ya shombo kwa jamaa huyo.
HASIRA
“Baada ya kuona imekuwa ‘too much’, Kuambiana alipandwa na hasira, akanyanyuka kwenye kochi na kumfuata Wema kwa lengo la kumpa kipigo,” kilisema chanzo hicho.
Martin Kadinda.
MARTIN KADINDA AMUOKOA
Habari zilidai kwamba, Kuambiana alipomfikia Wema alianza kumpiga vibao hadi meneja wake, Martin Kadinda akaingilia kati kumuokoa mwanadada huyo ambaye pia ni meneja wake.
KIBAO CHAMGEUKIA AUNT
Chanzo kilieleza kwamba baada ya kuachana na Wema, msaanii huyo ambaye pia ni ‘dairekta’ wa sinema mbalimbali za Bongo alimfuata Aunt na kuanza kumlamba makofi ya kutosha.
Tukio hilo lilizua tafrani na kuwafanya wasanii wengine waliokuwa eneo hilo wakimbie na kushindwa kuwatetea Aunt na Wema kwa kuogopa kugeuziwa kibao.
Adam Kuambiana.
KUAMBIANA ANASEMAJE?
Baada ya kuinyaka ishu hiyo, mapaparazi wetu walimtafuta Kuambiana na kumuuliza kulikoni kugeuka bondia na kuwapiga warembo hao ambapo alikiri kutokea kwa ishu huyo.
Alisema kuwa, Wema na Aunt ni kama wadogo zake, tena yeye kama dairekta wao walipaswa kumheshimu na siyo kumvunjia heshima.
“Akina Wema ni wadogo zangu, wanahitaji kuniheshimu na mimi ndiye mwongozaji wa filamu yao, kwa nini wanikosee heshima? Hata kama wamekasirika lakini nimewashikisha adabu,” alisema Kuambiana kwa ile sauti yake nzito.
WEMA & AUNT
Kwa upande wao, walipoulizwa Aunt na Wema kuhusiana na kichapo walichopewa walisema walishamzoea jamaa huyo, lakini kwa alilolifanya la kuwapiga makofi  aliwakwaza kwa sababu hata kama ni mwongozaji wa filamu yao lakini alikuwa pale kwa ajili yao.
HISTORIA YA KUAMBIANA
Ukiachana na tuki hilo, Kuambiana anadaiwa kuwa na mkono mwepesi hasa anapokuwa ‘lokesheni’ ambapo mwaka jana, aliwahi kumtia mikononi staa mwingine wa filamu za Bongo, Rose Ndauka walipokuwa wakirekodi filamu visiwani Zanzibar.
Siku ya tukio hilo, Kuambiana alikuwa akidairekti Filamu ya Distress in Zanzibar. Alimshutumu Rose kuvaa mavazi tofauti na maagizo yake, katika kujibishana akamuwasha makofi.
HATA MITAANI!
Juni, mwaka jana, Kuambiana alimshushia kipigo Fadhili Joseph ambaye alimdai fedha za bia alizokunywa kwenye baa yake, Sinza, Dar es Salaam.
Kuambiana aliposhindwa kulipa aliacha laptop (kompyuta mpakato), siku iliyofuata alirudi na kushusha kichapo huku akiitaka laptop hiyo.
Kuambiana alikamatwa na Polisi Kawe, Dar kwa faili la malalamiko KW/RB/5761/2012 SHAMBULIO. Kesi hiyo ikahamishiwa Kituo cha Polisi Kijitonyama ‘Mabatini’ kwa vile ndiyo kituo cha karibu na eneo la tukio.
MADAIREKTA WAKOJE?
Mbali na Kuambiana, staa mwingine ambaye pia ni dairekta wa muvi za Bongo, Issa Musa ‘Cloud’ naye aliwahi kutoa kipigo cha bakora kwa msanii Blandina Chagula ‘Johari’ kwa kosa la kuchelewa kufika sehemu ya kurekodia filamu.
Share:

PINGAMIZI LA MGOMBEA UBUNGE CHADEMA CHALINZE

TAARIFA YA PINGAMIZI LA MGOMBEA WA UBUNGE JIMBO LA CHALINZE FABIAN LEONARD SKAUKI – MGOMBEA CHAMA CHA WANANCHI –CUF

                                                            DHIDI YA
MATHAYO MANG’UNDA TORONGEY – MGOMBEA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO - CHADEMA
                                                            13.03.2014
Mimi  FABIAN L. SKAUKI, Mgombea Ubunge wa Uchaguzi mdogo Jimbo la CHALINZE kwa tiketi ya THE CIVIC UNITED FRONT (CUF) ninamwekea Pingamizi mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwamba amepoteza sifa za kuwa mgombea kwa sababu zifuatazo:
1.    Ndugu MATHAYO M. TORONGEY amejaza taarifa za uongo kwenye fomu yake kwamba kazi anayoifanya ni BIASHARA. Sio kweli, kwa sababu hajaweka vielelezo vya yeye kufanya hiyo kazi. Hajulikani anafanya kazi gani.
2.    Ndugu MATHAYO M. TORONGEY amejaza  katika fomu kwamba anajua kusoma na kuandika Kiswahili na kiingereza. Taarifa hizi ni za uongo, mgombea huyu hajui kusoma wala kuandika Kiswahili wala kiingereza, na kwamba amedanganya na amepoteza sifa za kuwa mgombea.
3.    Ndugu MATHAYO M. TORONGEY  amedanganya kwa kughushi/kufoji sahihi za wadhamini, ambao amewaorodhesha kwenye fomu ya kuomba kuthibitishwa kuwa mgombea. Ambapo katika fomu hizo wadhamini wote sahihi zao zimefojiwa na hazifanani na zile zilizokuwepo kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na kwamba sahihi zote hizi zimesainiwa na mtu mmoja ambaye sio muhusika. Hivyo anapoteza sifa ya kuendelea kuwa mgombea.
4.    Ndugu MATHAYO M. TORONGEY ameshindwa kutimiza mahitaji ya kisheria ya kuwa na wadhamini wasiopungua 25, badala yake amedhaminiwa na wadhamini 28 ambao kati yao wadhamini 7 sio wapiga kura halali wa Jimbo la CHALINZE, na kwamba Taarifa zao na namba zilizojazwa hazifanani.
Hivyo anabakiwa na wadhamini halali 21 ambao kisheria hawatoshi kutimiza matakwa ya kisheria.
Majina ya wadhamini hao ambao hawakidhi matakwa ya kisheria na namba zao ni:
JINA LA MDHAMINI                                                            NAMBA YA KADI KURA

1.    HABIBU ALLY SAIDI                                                     *16886275*
2.    MOHAMMED RAMADHANI                                       *30376567*
3.    ABDULKADIR ALLY                                                      *49264905*
4.    SHABANI SULEYMAN                                                  *16984045*
5.    JUMA MRISHO                                                            *48759563*
6.    RAJABU ALLY                                                              *16872368*
7.    MANENO MIRAJI                                                        *16872059*
Wananchi wenye namba na majina hayo hapo juu waliojazwa kama wadhamini kuanzia namba 1 hadi 7 kwenye fomu yake hawana sifa za kupiga kura kwenye maeneo ambayo wamejazwa wanatokea.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba idadi halali ya wadhamini wanaobaki ukiwaondoa hao saba watabaki 21, hawakizi vigezo vya kuwa wadhamini.
5.    Ndugu MATHAYO M. TORONGEY  amedanganya uraia wake na  kwamba yeye si Mtanzania wa kuzaliwa ndio maana hana vielelezo halali vinavyohusu uraia wake. Hivyo anakosa sifa ya kuwa mgombea.
Hivyo ninaomba Tume ya Uchaguzi kutengua uteuzi wa mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ndugu MATHAYO M. TORONGEY  kwa kuwa anakosa sifa za yeye kuendelea kuwa mgombea.
Wako katika ujenzi wa taifa,
FABIAN LEONARD SKAUKI
……………………………………………………..
MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA CHALINZE.
THE CIVIC UNITED FRONT
Share:

Wednesday 12 March 2014

BWAWA LA MAGEREZA MASWA



Magugu maji katika lambo la mwantonja Maswa
MAGUGU MAJI YAVAMIA LAMBO LA MWANTONJA MASWA

Na Isaack Mbwaga  Maswa  Machi 11,2014   Mhariri Habari Mwananchi

Mimea aina ya magugu maji yanatishia kufunika kabisa Lambo la maji  la Mwantonja mini Maswa Lambo linalo hudumia vitongoji 10 vinavyo zunguka lambo hilo  maji yake yatumika kwa kiwango kikubwa wakati wa kiangazi shughuli za kibinadmu kama vile umwagiliaji katika bustania,kujengea na kunyweshea Mifugo

Wakiongea na gazeti hili kwa nyakati tofauti lilipo tembelea eneo la Lambo la Mwantonja na kujionea hali halisi jinsi mimea hiyo ilivyo stawi na kufunika karibu eneo lote la Lambo kwa ktishia uhai wa Lambo

Mkazi wa kitongoji cha Unyanyembe  Njile Washa alisema magugumaji hayo yamezidi kuongeka kadiri siku zinavyo songa mbele na suala la kufurika kwa magugumaji  katika Lambo siyo geni  viongozi wa vitongoji karibu vyote vinavyo lizunguka Lambo wanayo taarifa na wanaona lakini hakuna hatua zinazo chukuliwa kuyaondoa magugu hayo

Njile aliongeza kusema kuwa endapo juhudi hazitafanyika kuanzia sasa kuyatoa huenda magugu hayo yakanza kusafiri hadi mto simiyu ambayo maji yake yanasafiri hadi ziwa Victori mkoani Mwanza

Naye Mwenyekiti wa Kitongoji cha Unyanyembe katika mji mdogo wa Maswa Nkuba Shimi alipo ongea na gazeti hili alisema kuwa taarifa za kuwepo kwa magugu maji   katika lambo la Mwantonja  Ofisi ya Idara ya mifugo na Uvuvi wanazo taarifa tatizo ni ukosefu wa nyenzo za kuvunia magugu hayo

Alizitaja nyenzo hizo kuwa ni pamoja rasimali fedha kwa ajili ya kuajiri watu, mitumbwi mitatu na visu vya kutosha ili watu watakao fanya kazi ya kuyaondoa magugumaji  kazi iwe rahisi kwao na bila kuhatarisha maisha yao ama kuzama endapo italetwa mitumbwi mibovu

Aidha uchunguzi  uliofanywa na gazeti hili umebaini katika baadhi ya visima vya maiji na malambo kadhaa ya maji kuwepo kwa mimea hiyo ambo inatishia uhai wa viumbe wengine kama vile samaki

Endapo mamlaka hazita chukua hatua za haraka kulikabili na kuyaondosha magugumaji hayo katika malambo na visima vilivyo vamiwa na mimea aina ya magugu maji  iko hatari ya kukosa maji kabisa kiangazi kwa ajili shughuli za kibinadamu kama vile Kilimo cha mbogamboga,kunyweshea Mifugo na matumizi ya Binadamu

Tatizo la kuoneka na kuota kwa magugu maji kwa mara ya kwanza lilianza kuijitokeza  mwaka 1994 ambapo mimea hiyo ilikuwa inasafishwa na wafanya biashara wa samaki kutoka Mwanza kuja kuuza katika Soko kuu la Nyalikungu katika mji wa Maswa

Masalia ya mimea ya magugu maji ambayo yalikuwa yanatumika kufunika Samaki  kutoka ziwa Victoria baada ya kutua mzigo wa Samaki majani ya magugu hayo  yalikuwa yanatupwa ovyo bila ungalizi karibu na Malambo ama visima vya maji wakati wana fanya usafi wa vyombo vyao vilivyo kuwa vinatumika kusafirishia Samaki

Serikali ya Halimashauri ya Wilaya ya Maswa [Idara ya Mifugo na Uvuvi] inao wajibu wa kuhakikisha juhudi zinafanyika haraka za kuyavuna magugu hayo kabla hajasambaa na kuenea maeneo mengi katika Halimashauri yote ya Wilaya ya Maswa na Wilaya Jirani zinazo pitiwa na mto Simiyu

Kufutia kuwepo kwa Mradi wa LIVEMP II kwa Halimashauri tano za Itilima,Magu,Kwimba,Meatu na Maswa ambapo Halimashauri ya Maswa ina wahamasisha Watu binafsi,Taasisi na Vikundi mbalimbali kuchimba mabwawa ya kufugia Samaki  kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na biashara


 
Share:

Saturday 8 March 2014

AFISA ELIMU AWAPA SOMO WALIMU WAKUU



WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI MASWA” WAFUNDWA”NA AFISA ELIMU SEKONDORI –NTAGAYE

Waalimu wa shule za Sekondari katika Halimashauri ya Wilaya ya Maswa wameagizwa kuhakikisha na wanafuatilia kwa ukaribu ufundashaji wa Wanafunzi katika Shule zao ili kuinua kiwango cha ufaulu Wanafunzi

Kauli hiyo alitolewa hivi karibuni na Afisa Elimu Sekondari wa Halimashauri ya Wilaya ya Maswa  Paulina Ntagaye wakati alipokuta na  Waalimu Wakuu wa Shule za Sekondari katika Ukumbi wa Halimashauri ya Maswa kwa lengo la kuwekeana mikakati ya kuboresha elimu ya Sekondari kwa mwaka 2014

Ntagaye pamoja na mambo mengine alisema kufuatia tamko la Serikali kuwa na mpango wa matokeo makubwa sasa[BRN] ni wajibu wa Waalimu wakuu kwa kila shule kusimamia kwa dhati kazi ya ufundishaji na kila Mwalimu wa Somo ahakikishe anawajibika kadri anavyoweza ili tupate matokeo makubwa

Hata hivyo Mkuu wa Shule ya Sekondari ya kutwa ya Binza Focus Nchiyiki alisema kuwa ili elimu yapatikane matokeo makubwa sasa ni wajibu wa Serikali kuhakikisha ina sambaza vitabu vya kianda na ziada vya kutosheleza kwa Wanafunzi  sambamba na ujenzi wa maabara kama ilivyo kwa Shirika la Umeme[TANESCO]wanavyo sambaza umeme vijijini

“Tunaona karibu kila siku maroli ya nguzo za Umeme na nyaya zinazambazwa katika vijiji mbalimbali vilivyo pendekezwa kupata nishati ya Umeme lakini Wizara ya Elimu na mafunzo Wanafunzi wana uhaba wa vitabu hakuna maabara za kutosha pia na Waalimu ni nwachache katika baadhi ya shule za Sekondari”alisema

Afisa Elimu wa Sekondari  katika Halimashauri ya Maswa Paulina Ntagaye alizipongeza shule kumi bora zilizo fanya vizuri katika mtihani wa kidato cha Pili 2013  ambazo ni Lalago Sekondari,Ipililo Sekondari,Kulimi Sekondari,Senani Sekondari,Mwabayanda Sekondari, shule zingine ni Nyabubinza,Kadoto Sekondari,Ng’wanza Sekondari na Salagi

 Wakati huo huo Ntagaye hakusita kuwanyoshea vidole  Wakuu wa Shule kumi duni ambazo matokea yake ni mabaya mtihani wa kidato cha pili kuwa Ofisi yake hata sita kuwa chukulia hatua kali endepo shule hizo zitaendea kufanya vibaya katika mitihani yake mbalimbali ya ndani na kitaifa alisema kwa msisitizo Afisa Elimu huyo

Shule ya Sekondari ya Kata ya Ipililo imeshika na nafasi ya kwanza kwa shule za Serikali kati ya shule 36 za Serikali    ingawa shule ya Sekondari ya Wazazi ya Lalago imeshika nafasi ya kwanza kati shule 38 za Serikali na binafsi wakati za binafsi  ni Ng’wanza Sekondari na Lalago Sekondari

Share:

CCM MASWA, YAONYWA


CCM MASWA  YAWEKA MSIMAMO KWA WAJUMBE WAKE KATIKA UTOAJI WA      MAONI KATIBA MPYA

Wakati muda wa  Wajumbe wa Mabaraza ya katiba ngazi ya Wilaya kuanza mchakato wa kutoa maoni kutoka Kata mbalimbali za Wilaya ya  Maswa Chama cha Mapinduzi katika Wilaya ya Maswa tayari kimeweka msimamo kwa  Wajumbe wanachama wake ambao ni Wajumbe wa Baraza la katiba  liloanza kikao chake  jana

Wakiongea kwa nyakati  tofauti jana na Mwandishi wa habari hizi juzi mara baada ya  kikao chao kilicho itishwa kwa lengo kuweka simamo wa chama kwa sharti ya kuto tajwa majina yao katika vyombo vya habari kwa kuhofia kuchukuliwa hatua za kinidhamu na Chama

 Walisema kitendo cha  viongozi wa Chama cha Mapinduzi ngazi ya Wilaya ya Maswa  kuwa wekea msimamo wa chama kwa madai  wasiukosoe ni kuwanyima haki ya kutoa mawazo yao ya demokrasia  ndani na kuwambia kilichojadiliwa na uongozi wa juu  hakuna mtu wa kuzungumza tofauti watakapo hudhuria kikao cha Baraza la Katiba ngazi ya Wilaya

Kufuatia hali hiyo Mjumbe mmoja ambaye ni Diwani kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi   alisema pamoja na kuhudhuria kikao cha chama  kitendo cha kuwafunga midomo  wajumbe katika kikao kwa kuwa lazimisha wajadili kilicho letwa na chama ngazi Taifa siyo kitendo kizuri kwa kweli  kina wanyima fursa  watu wengine kutoa mawazo yao ambayo huenda yanaweza  kusaidia kupata Katiba bora

Hata hivyo alipo uliziwa katibu  Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi katika Wilaya Maswa ambaye ni Katibu Mwenezi wa Mkoa wa Simiyu Jeremiah Mange[Makondeko]kuelezea tuhuma za kuwaziba midomo Wajumbe wa Kikao cha Chama  cha Mapinduzi [CCM]

Kwa upande wake alikanusha uvumi huo na kudai kuwa kikkao kilendeshwa kwa uhuru na kila mjumbe aliruhusiwa kutoa maoni yake bila woga ama vitisho”sikiliza Mwandishi  CCM ndiyo inayo ongoza Serikali  na mawazo ya kuandika katiba mpya ni wazo la Mwenyekiti wetu wa Chama Taifa Jakaya Kikwete kwa nini tuwazuie Wanachama wetu kuzungumza katika kikao hayo ni majungu”alisema Mange

 Mkutano wa Baraza la kutoa maoni ya Rasimu ya Katiba ya Tanzania umeanza jana kwa kuwa shirikisha Wajumbe Mbalimbali kutoka katika Kata zas Wilaya ya Maswa
Share:

Thursday 6 March 2014

MKURUGENZI WILAYA YA MASWA ACHA UBABE


MKURUGEZI MTENDAJI WA HALIMASHAURI YA MASWA, AACHE UBABE KWA WANDISHI WA HABARI

Mkurugenzi Mtendaji wa Halimashuri ya Maswa bibi Hilda Lauwo anataka kuongoza Halimashuri ya Maswa kwa ubabe jambo ambalo halita msaidia kwa namna yoyote katika mustakabali wa Halimashauri hiyo iwapo ataendelea kujenga mazingira hasi kwa wandishi wa Habari

Katika hali isiyo ya kawida hivi karibuni alilibeza Gazeti moja linalo tolewa mara moja kwa wiki Jijini mwanza jina la gazeti hilo kwa sasa lina hifadhiwa akidai kuwa kazi yake kuandika umbeya tu na ni balaa

Akionesha kuwa anataka kufanya kazi kwa woga wa kuto kusogelewa na vyombo vya habari na Wandishi wa Habari amejikuta kila mara lugha yake ni ya kibabe na kejeli kana kwamba nafasi aliyo pewa ya Ukurugenzi ni mali binafsi na wala si dhamana ya Umma tena

Aidha baadhi ya matukio alio yaonesha katika siku za hivi karibuni tangu alipo hamia Halimashuri ya Maswa akitokea Halimashuri ya Ludewa MKoa Mpya Wa Njombe

 Ni wakati ilipo kosolewa baadhi ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halimashauri ya Maswa kutokana taarifa ya  Afisa Mipango wa Halimashauri ya Maswa Jeremia Kikonge kutokidhi sifa za ujenzi mradi wa maabara shule ya Sekondari ya Kata ya Masela

 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Bibi Mwamvua Jilumbi hakuridhishwa kabisa na maelezo ya taarifa hiyo na kuamua kumweleza mkurugenzi mtendaji kina ubaga asimamia kwa karibu miradi hiyo kwa kuwa Serikali na Wafadhili maendeleo wamekuwa wakitoa fedha nyingi za kugharimia miradi hiyo 

Bibi Mwamvua Jilumbi alifanya ziara ya kutembelea Halimashauri ya Maswa miezi mitatu iliopita[Juni,2013 kwa  lengo la kukagua shughuli za maendeleo akiwa ameongozana na Timu ya Wataalamu wa ngazi ya  Mkoa wa Simiyu  Mkurugenzi wa Halimashuri ya Wilaya Maswa akiwa na Wataalaamu wake

Wakati zoezi linaendelea la kukagua mradi wa Jengo la kisasa la upasuaji katika eneo la Hospitali ya Wilaya ya Maswa katika hali isiyo tarajiwa na kiongozi wa umma ambaye ni Mkurugenzi wa Halimashauri ya Maswa Bibi Hilda Lauwo

 Mkurugenzi Mtendaji wa Maswa aliamua kujifunika uso kwa mikono ili asipigwe picha na kamera ya mwandishi wa Habari hizi hiyo ilikuwa wakati akipewa maelezo mafupi na mzabuni juu ya maendeleo ya mradi na changamoto zinazokwamisha kukamilika kwa mradi mzima kwa wakati[ jina la mzabuni limehifadhiwa] kwa sasa

Mkurugenzi huyo akiwa hajiamini na utendaji wake alisikika akisema ninyi andikeni chochote tu hamuni babaishi na uandishi wenu kauli zake hizo inazo ashiria ubabe na kejeli  ni pale aliposikika kwa mara ingine wakati wa kikao cha Sekta ndogo ya zao la Pamba kilichofanyika Mjini Bariadi

 Akisema hawapendi Wandishi wa habari, hawapendi kwa nini? Huyu ni mtumishi wa Umma vyombo vya habari ni rafiki wa maendeleo ya kweli na si vinginevyo anaogopa nini kuumbuka?kuwa karibu nao.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger