Saturday 8 March 2014

CCM MASWA, YAONYWA

...

CCM MASWA  YAWEKA MSIMAMO KWA WAJUMBE WAKE KATIKA UTOAJI WA      MAONI KATIBA MPYA

Wakati muda wa  Wajumbe wa Mabaraza ya katiba ngazi ya Wilaya kuanza mchakato wa kutoa maoni kutoka Kata mbalimbali za Wilaya ya  Maswa Chama cha Mapinduzi katika Wilaya ya Maswa tayari kimeweka msimamo kwa  Wajumbe wanachama wake ambao ni Wajumbe wa Baraza la katiba  liloanza kikao chake  jana

Wakiongea kwa nyakati  tofauti jana na Mwandishi wa habari hizi juzi mara baada ya  kikao chao kilicho itishwa kwa lengo kuweka simamo wa chama kwa sharti ya kuto tajwa majina yao katika vyombo vya habari kwa kuhofia kuchukuliwa hatua za kinidhamu na Chama

 Walisema kitendo cha  viongozi wa Chama cha Mapinduzi ngazi ya Wilaya ya Maswa  kuwa wekea msimamo wa chama kwa madai  wasiukosoe ni kuwanyima haki ya kutoa mawazo yao ya demokrasia  ndani na kuwambia kilichojadiliwa na uongozi wa juu  hakuna mtu wa kuzungumza tofauti watakapo hudhuria kikao cha Baraza la Katiba ngazi ya Wilaya

Kufuatia hali hiyo Mjumbe mmoja ambaye ni Diwani kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi   alisema pamoja na kuhudhuria kikao cha chama  kitendo cha kuwafunga midomo  wajumbe katika kikao kwa kuwa lazimisha wajadili kilicho letwa na chama ngazi Taifa siyo kitendo kizuri kwa kweli  kina wanyima fursa  watu wengine kutoa mawazo yao ambayo huenda yanaweza  kusaidia kupata Katiba bora

Hata hivyo alipo uliziwa katibu  Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi katika Wilaya Maswa ambaye ni Katibu Mwenezi wa Mkoa wa Simiyu Jeremiah Mange[Makondeko]kuelezea tuhuma za kuwaziba midomo Wajumbe wa Kikao cha Chama  cha Mapinduzi [CCM]

Kwa upande wake alikanusha uvumi huo na kudai kuwa kikkao kilendeshwa kwa uhuru na kila mjumbe aliruhusiwa kutoa maoni yake bila woga ama vitisho”sikiliza Mwandishi  CCM ndiyo inayo ongoza Serikali  na mawazo ya kuandika katiba mpya ni wazo la Mwenyekiti wetu wa Chama Taifa Jakaya Kikwete kwa nini tuwazuie Wanachama wetu kuzungumza katika kikao hayo ni majungu”alisema Mange

 Mkutano wa Baraza la kutoa maoni ya Rasimu ya Katiba ya Tanzania umeanza jana kwa kuwa shirikisha Wajumbe Mbalimbali kutoka katika Kata zas Wilaya ya Maswa
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger