Monday 31 March 2014

Bunge livunjwe tukawaombe radhi wananchi- Mjumbe

...

Bunge livunjwe tukawaombe radhi wananchi- Mjumbe

Laizer pia amewataka wajumbe wenzake kurudi katika maeneo yao ili wakaombe radhi kwa Watanzania kutokana na ufujaji wa fedha unaotokana na kuwepo kwao kwenye vikao vya Bunge.


Dodoma. Mivutano katika Bunge la Katiba imemchukiza mmoja wa wajumbe wa chombo hicho, Michael Laizer ambaye amemshauri mwenyekiti wake, Samuel Sitta amwombe Rais kuvunja Bunge.
Laizer pia amewataka wajumbe wenzake kurudi katika maeneo yao ili wakaombe radhi kwa Watanzania kutokana na ufujaji wa fedha unaotokana na kuwepo kwao kwenye vikao vya Bunge.
“Mwenyekiti narudia tena kama watu hawataki uamuzi huu, nakushauri andika barua kwa Mheshimiwa Rais ili aje alivunje Bunge na twende makwetu,” alisema Laizer.
Laizer alilishutumu Bunge hilo kuendelea kutafuna fedha wakati watu wengine wanaishi maisha magumu zaidi kiasi cha kushindwa kupata hata mlo mmoja kwa siku.
Alipinga muda ambao wametumia wajumbe hao kwa ajili ya kujadili masuala ya kanuni pekee bila hata ya kufikia uamuzi, akisema ndoto yake ni kuwa hadi wiki hii waanze kuchambua vifungu vya katiba.
Aidha alisema watu wenye umri mkubwa kama yeye (Laizer) wanaogopa kuchangia hoja kutokana na tabia ya kuzomeana.
Aliwataka wajumbe kuwa wavumilivu ili kuruhusu wajumbe kuchangia mijadala kwa uhuru.
michango kwa uhuru.
na kuheshimiana kama ilivyotokea kwa baraza la Wawakilishi Zanzibar ambako CCM ilikubali kugawa madaraka hata pale ambapo hawakutaka kufanya hivyo.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger