Saturday 8 March 2014

AFISA ELIMU AWAPA SOMO WALIMU WAKUU

...


WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI MASWA” WAFUNDWA”NA AFISA ELIMU SEKONDORI –NTAGAYE

Waalimu wa shule za Sekondari katika Halimashauri ya Wilaya ya Maswa wameagizwa kuhakikisha na wanafuatilia kwa ukaribu ufundashaji wa Wanafunzi katika Shule zao ili kuinua kiwango cha ufaulu Wanafunzi

Kauli hiyo alitolewa hivi karibuni na Afisa Elimu Sekondari wa Halimashauri ya Wilaya ya Maswa  Paulina Ntagaye wakati alipokuta na  Waalimu Wakuu wa Shule za Sekondari katika Ukumbi wa Halimashauri ya Maswa kwa lengo la kuwekeana mikakati ya kuboresha elimu ya Sekondari kwa mwaka 2014

Ntagaye pamoja na mambo mengine alisema kufuatia tamko la Serikali kuwa na mpango wa matokeo makubwa sasa[BRN] ni wajibu wa Waalimu wakuu kwa kila shule kusimamia kwa dhati kazi ya ufundishaji na kila Mwalimu wa Somo ahakikishe anawajibika kadri anavyoweza ili tupate matokeo makubwa

Hata hivyo Mkuu wa Shule ya Sekondari ya kutwa ya Binza Focus Nchiyiki alisema kuwa ili elimu yapatikane matokeo makubwa sasa ni wajibu wa Serikali kuhakikisha ina sambaza vitabu vya kianda na ziada vya kutosheleza kwa Wanafunzi  sambamba na ujenzi wa maabara kama ilivyo kwa Shirika la Umeme[TANESCO]wanavyo sambaza umeme vijijini

“Tunaona karibu kila siku maroli ya nguzo za Umeme na nyaya zinazambazwa katika vijiji mbalimbali vilivyo pendekezwa kupata nishati ya Umeme lakini Wizara ya Elimu na mafunzo Wanafunzi wana uhaba wa vitabu hakuna maabara za kutosha pia na Waalimu ni nwachache katika baadhi ya shule za Sekondari”alisema

Afisa Elimu wa Sekondari  katika Halimashauri ya Maswa Paulina Ntagaye alizipongeza shule kumi bora zilizo fanya vizuri katika mtihani wa kidato cha Pili 2013  ambazo ni Lalago Sekondari,Ipililo Sekondari,Kulimi Sekondari,Senani Sekondari,Mwabayanda Sekondari, shule zingine ni Nyabubinza,Kadoto Sekondari,Ng’wanza Sekondari na Salagi

 Wakati huo huo Ntagaye hakusita kuwanyoshea vidole  Wakuu wa Shule kumi duni ambazo matokea yake ni mabaya mtihani wa kidato cha pili kuwa Ofisi yake hata sita kuwa chukulia hatua kali endepo shule hizo zitaendea kufanya vibaya katika mitihani yake mbalimbali ya ndani na kitaifa alisema kwa msisitizo Afisa Elimu huyo

Shule ya Sekondari ya Kata ya Ipililo imeshika na nafasi ya kwanza kwa shule za Serikali kati ya shule 36 za Serikali    ingawa shule ya Sekondari ya Wazazi ya Lalago imeshika nafasi ya kwanza kati shule 38 za Serikali na binafsi wakati za binafsi  ni Ng’wanza Sekondari na Lalago Sekondari

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger