Monday, 15 September 2025

MAMLAKA YA DAWA NA VIFAA TIBA YASHIRIKI MAONESHO YA BIASHARA MBEYA, YAWASHAURI WANANCHI KUTUMIA DAWA KWA SAHIHI

...

 

















Meneja wa TMDA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Anitha Mshighati
akitoa maelezo  kwa mkuu wa mkoa wa mbeya Beno Malisa alipotembelea Katika banda lao  lililopo Katika maonyesho ya biashara Ya kimataifa  ya kanda ya nyanda za juu kusini 

Na Woinde Shizza ,Mbeya
Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imeshiriki maonesho ya pili ya biashara ya kimataifa yaliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, ikitoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanatumia dawa za binadamu na mifugo zilizosajiliwa na zilizo salama.

Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa TMDA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Anitha Mshighati alisema kuwa lengo la ushiriki wao ni kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuhakikisha watumia sawa kwa usahihi ilikuondokana na usugu wa vimelea dhidi ya dawa pamoja na kuhakikisha wananunua dawa katika maeneo rasmi.

“Tumeona ni nafasi nzuri ya kutoa elimu kwa wakazi wa Mbeya na wageni wanaoshiriki maonesho haya kuhusu matumizi sahihi ya dawa na vifaa tiba tunasisitiza wananchi kununua dawa katika maduka ya dawa yaliyoidhinishwa na kuacha kutumia dawa kiholela bila ushauri wa kitaalamu,” alisema.

Maonesho hayo yamekusanya wafanyabiashara, wawekezaji na wadau mbalimbali wa maendeleo kutoka ndani na nje ya nchi, yakilenga kukuza biashara na uwekezaji katika Mkoa wa Mbeya na ukanda wa Nyanda za Juu Kusini.

TMDA imesisitiza itaendelea kushirikiana na wananchi, wafanyabiashara na wadau wa afya ili kuhakikisha dawa na vifaa tiba vinavyotumika nchini ni salama, bora na fanisi.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger