Sunday 21 August 2022

MREMBO AFARIKI KWA KUZAMA SWIMMING POOL AKIJIREKODI LIVE FACEBOOK

...


Mrembo Hellen Wendy aliyefia kwenye swimming pool nchini Canada
**
MREMBO raia wa Kenya aliyekuwa akifanya kazi ya uuguzi nchini Canada, Hellen Wendy amefariki dunia baada ya kuzama wakati akiwa anaogelea kwenye ‘swimming pool’.


Kabla hajafikwa na umauti, Hellen alikuwa akijirekodi ‘live video’ kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook, ambapo anaonekana kwenye video hiyo, akiwa anazungumza na marafiki zake kwenye mtandao huo.


Akiwa anaendelea kufurahi na marafiki zake huku akiogelea, ghafla Hellen alionekana akianza kutapatapa kwenye maji na akasikika akipiga mayowe ya kuomba msaada, kisha akazama.



Video aliyokuwa ameianzisha Facebook, iliendelea kuwa kwa takribani saa 3, huku ikionesha kwamba alifariki dunia dakika 10 au dakika ya 11 tangu alipoanza kurekodi video hiyo.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger