Friday 22 July 2022

SIMBA WASAJILI BEKI MPYA

...


Beki mpya wa Simba Mohamed Ouattara

KLABU ya Simba imekamilisha usajili wa mlinzi wa kati kutoka klabu ya Al Hilal ya nchini Sudan Mohamed Ouattara.

Ouattara amesaini kandarasi ya miaka miwili kuwatumikia wekundu wa msimbazi na anaingia moja kwa moja kuziba pengo la Pascal Wawa aliyemaliza mkataba wake na tayari ameshatimka klabuni hapo.


Ouattara ametambulishwa rasmi kupitia ukurasa wa klabu hiyo wa mtandao wa kijamii wa Instagram.


Beki huyo raia wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 29 amewahi pia kukipiga katika Ligi Kuu nchini Morocco akiwa na moja ya miamba ya soka Barani Afrika Klabu ya Wydad Casablanca.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger