Tuesday 26 July 2022

BASI LA SHULE LAUA WATU 10 WAKIWEMO WANAFUNZI 8 ..RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA POLE

...
Ajali ya basi
Rais Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za pole kufuatia basi la wanafunzi wa Shule ya King David Mtwara lenye namba za usajili T 207 CTS lililopata ajali asubuhi ya leo Jumanne, Julai 26, 2022 eneo la Mikindani Mtwara likiwa na wanafunzi na kuua watu 10 wakiwemo wanafunzi nane wa shule hiyo.


Kamanda wa Polisi Mtwara Nicodemus Katembo amesema Wanafunzi waliofariki dunia ni wanane, Dereva mmoja na Mwangalizi mmoja, majeruhi ni 19.


Kupitia akaunti yake ya Twitter, Rais Samia ameandika: “Nimesikitishwa na vifo vya wanafunzi 8 wa Shule ya Msingi ya King David na watu wazima 2 vilivyotokea leo asubuhi huko Mtwara Mikindani baada ya gari la shule kutumbukia shimoni. Nawapa pole wafiwa, mkuu wa mkoa na jamaa. Mwenyezi Mungu awarehemu marehemu na kuwaponya majeruhi.


Taarifa zaidi kuhusu ajali hiyo zitakujia hivi punde.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger