Wednesday 20 July 2022

DIAMOND PLATNUMZ ATHIBITISHA KUNUNUA NDEGE

...

Diamond Platnumz akitumbuiza Jijini Berlin Ujerumani

KAMA ulikuwa unadhani ni stori stori tu za mtandaoni, habari ikufikie Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amethibitisha kununua ndege.


Ndio, kwa kinywa chake Diamond ametamka akiwa nchini Ujerumani akiwa ameshika kipaza sauti cha chombo cha habari cha kimataifa cha DW nchini Ujerumani.
Diamond alikuwa akizungumzia namna msanii unatakiwa kuishi au kuwa ili kupata ile heshima unayostahili na kuingiza mkwanja wa kutosha (msanii unavyotakiwa kujiwekeza mwenyewe).


“Mfano kwa mtu kama mimi ambaye nimetokea mtaani, kwa sasa nanunua gari la kifahari lenye thamani hadi tsh. bilioni 2.3…kwa hiyo itabidi ufanye hivyo kwani usipofanya hivyo hawatakuona wewe ni wa thamani (watakuchukulia poa)… na sasa tayari nimeshanunua ndege binafsi (private jet),” Diamond Platnumz.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger