Sunday 31 July 2022

SIMBA SC YAIBUKA NA SLOGAN MPYA "WE ARE UNSTOPPABLE".....HATUSHIKIKI HATUZUILIKI

...

CEO wa Simba Barbara Gonzalez Kushoto akizindua Slogan mpya kwa msimu huu We Are Unstoppable (Kushoto) ni malkia wa Bongo Fleva Zuchu
 **
Mtendaji Mkuu wa Simba Barbara Gonzalez amesema kuwa msimu huu klabu hiyo imejipanga kurudisha makombe yote ya ndani na kuhakikisha inafika nusu fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika.


Barbara ameyasema hayo leo kwenye uzinduzi wa Simba Week uliofanyika Mbagala Zakheim Dar es salaam ambapo pia ameongeza kuwa usajili bado unaendelea na kuanzia wiki ijayo wataendelea kushusha wachezaji wengine.


“Safari hii hakuna kuteleza tena. Tumejipanga kuhakikisha tunarudisha mataji yote kuanzia Ligi Kuu, FA na kufika Nusu Fainali ya Klabu Bingwa Afrika”


Kuelekea kilele cha Simba Day ambayo itafanyika Agosti 8, 2022 Simba imezindua Slogan Mpya We Are Unstoppable Hatushikiki Hatuzuiliki.

Msimu uliopita Simba ilizisiwa ujanja na watani zao Yanga baada ya kuzoa makombe yote ikiwemo la ligi kuu ya Nbc, pamoja na Kombe la shirikisho la Azam (Azam Sports Federation Cup) na Ngao ya Jamii.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger