Friday 15 July 2022

JUMUIYA YA WAZAZI CCM YAJIPANGA KUBORESHA USHINDANI KIELIMU

...
Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo amesema hayo jana Jijini Dodoma wakati akiongea kwenye kikao cha Wakuu wa shule za Umoja wa Wazazi jijini Dodoma. 
Na Dotto Kwilasa,DODOMA

JUMUIYA ya Umoja  wa wazazi ,
 Chama  cha Mapinduzi (CCM) imeazimia kuboresha shule zote zinazomilikiwa na Jumuiya hiyo kuwa zenye viwango,vigezo, vipimo  na utofauti ili kuingia kwenye ubora wa ushindani sawa na shule nyingine.

Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo amesema hayo leo Jijini Dodoma wakati akiongea kwenye kikao cha Wakuu wa shule za Umoja wa Jumuiya ya wazazi Tanzania na kutaka maboresho hayo kuhusisha makundi  kundi yote ikiwemo wanafunzi wenye ufaulu mzuri,ufaulu wa kati na wale wasiojiweza kabisa .

Amesema ili kuendana na malengo ya kuanzisha shule hizo inatakiwa  kila kundi lipewe dozi kulingana na hali halisi
ya madaraja yao na kwamba kila jambo linahitaji msukumu zaidi wa mafanikio .

"Sasa hivi hatupo tena kwenye giza, 
tunatakiwa kuongeza bidii kwenye haya mafanikio tuliyoyaleta wenyewe
na lazima mfahamu kuwa hakuna muujiza kwenye mafanikio,"ameeleza

Katibu Mkuu huyo pia amesema kulingana na mwenendo  wanaoenda nao shule hizo zinahitaji mabweni hivyo kuweka wazi kuwa yeye kwa nafasi yake atahakikisha anatekeleza jambo hilo ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira ya walimu na wale wanafunzi wanaodhaniwa kuwa hawafundishiki.

"Ahadi yangu ipo  palepele kuhakikisha walimu wanakuwa na mazingira mazuri zaidi ili kuendana na hadhi ya Jumuiya hii ikiwa ni apamoja na kuongeza madarasa mawili mawili,tutaangalia pia uhitaji wa shule husika hali itakayoongeza ufanisi na  kupekelea shule zetu kuwa kimbilio kwa kila mtu,"amesisitiza Chongolo 

Sambamba na hayo Chongolo ameeleza malengo ya kuanzisha Shule za Jumuiya hiyo kuwa ni pamoja na kuongeza wigo wa elimu kwa wananchi waliokosa fusra kwenye machaguo mbalimbali ya serikali,kupanua wigo na kupata wasomi wengi kwenye nchi na kuongeza kiwango chenye elimu yenye tija nchini.

"Kazi bado haijaisha,tuna kazi nyingine ya ziada,bado lengo kuu la elimu bora na kufanikisha kuendelea liko pale pale 
kufanikisha misingi ya uanzishaji wa shue zetu kwa kuwaandaa na kuwajengea msingi wanafunzi walioshindwa na wale wanaodhaniwa kuwa hawafundishiki,"amesema Katibu huyo

"Tumewapa jukumu hili la kuboresha mazingira ya elimu,nendeni  mkalifanye kwa dhamira ya dhati,mengi mmefanya kwa kujitolea,mafanikio yanatafutwa na ili kufanikiwa lazima uweke juhudi zako ninyi ni watu wa msukuko tambueni heshima ya Mwalimu ni matokea,ukitaka kuheshimiwa tengeneza matokeo yako vizuri,"amesema na kuongeza;

Heshima ni gharama,na ninyi mmeonesha namna mnavyodhamiria kuitafuta heshima kwa gharama yoyote,sina shaka dhamira yenu ni kujaza kibaba"amesisitiza

Katibu huyo pia alitoa wito kwa Wakuu wa Shule  hizo za Jumuiya ya wazazi kuwapa motisha walimu na wanafunzi ili kufanya vizuri zaidi na kwamba awamu ijayo hawatatoa zawadi kwa usawa bali  watatoa kutokana na ushindi wa matokeo 

"Tutatumia ushindani wa vigezo,vipimo, viwango na utofauti,tusilazimishe mambo makubwa tuendelee kuweka msukumo na viwango vyetu  ili tupate ubora tunautaka,"amesisitiza

Pamoja na hayo Katibu huyo Mkuu wa CCM ametumia nafasi hiyo kuwataka Wakuu hao kupenda kufanya kazi kwenye mazingira yanayohitaji mafanikio na kukemea tabia ya baadhi ya walimu kutamani shule zilizofanikiwa.

"Mwalimu mwenye uwezo apelekwe kwenye shule inayohitaji mafanikio,hali hiyo itawaheshimisha walimu,kila mtu atafute mafanikio ya shule yake nisione mtu anataka kuhamia shule yenye mafanikio waliyoyaanzisha wenzie  wakati yeye ameshindwa huo ni ubinafsi mkubwa,"amesema

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi taifa Dkt.Edmund Mndolwa ametumia  nafasi hiyo kuwataka Wakuu wa Shule hizo kuacha kuingiza siasa kwenye Jumuiya hiyo huku akiwataka kufanya kazi kwa kufuata misingi ya maadali na uzalendo.

"Siasa ina mahali pake hatupaswi kuiingiza kwenye utendaji,lazima tujue kutofautisha vitu hivi,najua kuna wakati mnafanyia kazi katika mazingira magumu lakini msikate tamaa ili muendelee kuijenga heshima yenu,"amesema

Amesema shule za wazazi nchini kwa sasa zina utulivu wa kutosha tofauti na ilivyokuwa mwanzo na kueleza kuwa hali hiyo imetokana na maelekezo ya uongozi uliopo na kufanya matokeo mazuri 
kwa shule zote za wazazi licha ya wanafunzi waliopo ni wale wanaodhaniwa kuwa hawafundishiki.


Mwishoo



 Kwilasa ,DODOMA

JUMUIYA ya Umoja  wa wazazi ,
 Chama  cha Mapinduzi (CCM) imeazimia kuboresha shule zote zinazomilikiwa na Jumuiya hiyo kuwa zenye viwango,vigezo, vipimo  na utofauti ili kuingia kwenye ubora wa ushindani sawa na shule nyingine.

Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo amesema hayo jana Jijini Dodoma wakati akiongea kwenye kikao cha Wakuu wa shule za Umoja wa Jumuiya ya wazazi Tanzania na kutaka maboresho hayo kuhusisha makundi  kundi yote ikiwemo wanafunzi wenye ufaulu mzuri,ufaulu wa kati na wale wasiojiweza kabisa .

Alisema ili kuendana na malengo ya kuanzisha shule hizo inatakiwa  kila kundi lipewe dozi kulingana na hali halisi
ya madaraja yao na kwamba kila jambo linahitaji msukumu zaidi wa mafanikio .

"Sasa hivi hatupo tena kwenye giza, 
tunatakiwa kuongeza bidii kwenye haya mafanikio tuliyoyaleta wenyewe
na lazima mfahamu kuwa hakuna muujiza kwenye mafanikio,"ameeleza

Katibu Mkuu huyo pia alisema kulingana na mwenendo  wanaoenda nao shule hizo zinahitaji mabweni hivyo kuweka wazi kuwa yeye kwa nafasi yake atahakikisha anatekeleza jambo hilo ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira ya walimu na wale wanafunzi wanaodhaniwa kuwa hawafundishiki.

"Ahadi yangu ipo  palepele kuhakikisha walimu wanakuwa na mazingira mazuri zaidi ili kuendana na hadhi ya Jumuiya hii ikiwa ni apamoja na kuongeza madarasa mawili mawili,tutaangalia pia uhitaji wa shule husika hali itakayoongeza ufanisi na  kupekelea shule zetu kuwa kimbilio kwa kila mtu,"amesisitiza Chongolo 

Sambamba na hayo Chongolo ameeleza malengo ya kuanzisha Shule za Jumuiya hiyo kuwa ni pamoja na kuongeza wigo wa elimu kwa wananchi waliokosa fusra kwenye machaguo mbalimbali ya serikali,kupanua wigo na kupata wasomi wengi kwenye nchi na kuongeza kiwango chenye elimu yenye tija nchini.

"Kazi bado haijaisha,tuna kazi nyingine ya ziada,bado lengo kuu la elimu bora na kufanikisha kuendelea liko pale pale 
kufanikisha misingi ya uanzishaji wa shue zetu kwa kuwaandaa na kuwajengea msingi wanafunzi walioshindwa na wale wanaodhaniwa kuwa hawafundishiki,"amesema Katibu huyo

"Tumewapa jukumu hili la kuboresha mazingira ya elimu,nendeni  mkalifanye kwa dhamira ya dhati,mengi mmefanya kwa kujitolea,mafanikio yanatafutwa na ili kufanikiwa lazima uweke juhudi zako ninyi ni watu wa msukuko tambueni heshima ya Mwalimu ni matokea,ukitaka kuheshimiwa tengeneza matokeo yako vizuri,"amesema na kuongeza;

Heshima ni gharama,na ninyi mmeonesha namna mnavyodhamiria kuitafuta heshima kwa gharama yoyote,sina shaka dhamira yenu ni kujaza kibaba"amesisitiza

Katibu huyo pia alitoa wito kwa Wakuu wa Shule  hizo za Jumuiya ya wazazi kuwapa motisha walimu na wanafunzi ili kufanya vizuri zaidi na kwamba awamu ijayo hawatatoa zawadi kwa usawa bali  watatoa kutokana na ushindi wa matokeo 

"Tutatumia ushindani wa vigezo,vipimo, viwango na utofauti,tusilazimishe mambo makubwa tuendelee kuweka msukumo na viwango vyetu  ili tupate ubora tunautaka,"amesisitiza

Pamoja na hayo Katibu huyo Mkuu wa CCM ametumia nafasi hiyo kuwataka Wakuu hao kupenda kufanya kazi kwenye mazingira yanayohitaji mafanikio na kukemea tabia ya baadhi ya walimu kutamani shule zilizofanikiwa.

"Mwalimu mwenye uwezo apelekwe kwenye shule inayohitaji mafanikio,hali hiyo itawaheshimisha walimu,kila mtu atafute mafanikio ya shule yake nisione mtu anataka kuhamia shule yenye mafanikio waliyoyaanzisha wenzie  wakati yeye ameshindwa huo ni ubinafsi mkubwa,"amesema

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi taifa Dkt.Edmund Mndolwa ametumia  nafasi hiyo kuwataka Wakuu wa Shule hizo kuacha kuingiza siasa kwenye Jumuiya hiyo huku akiwataka kufanya kazi kwa kufuata misingi ya maadali na uzalendo.

"Siasa ina mahali pake hatupaswi kuiingiza kwenye utendaji,lazima tujue kutofautisha vitu hivi,najua kuna wakati mnafanyia kazi katika mazingira magumu lakini msikate tamaa ili muendelee kuijenga heshima yenu,"amesema

Amesema shule za wazazi nchini kwa sasa zina utulivu wa kutosha tofauti na ilivyokuwa mwanzo na kueleza kuwa hali hiyo imetokana na maelekezo ya uongozi uliopo na kufanya matokeo mazuri 
kwa shule zote za wazazi licha ya wanafunzi waliopo ni wale wanaodhaniwa kuwa hawafundishika.



Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger