Monday 18 April 2022

WASIOJULIKANA WAUA NA KUIBA MAFUTA YA KULA

...


Polisi katika eneo la Uranga kaunti ya Siaya nchini Kenya, wanachunguza mauaji ya kijana mmoja mwenye umri wa miaka 19, baada ya watu wasiojulikana kumvamia dukani na kumuua kisha kuondoka na mafuta ya kula.

Tukio hilo limetokea Jumatano, Aprili 13, 2022, ambapo kwa mujibu wa polisi wameeleza kwamba mwili wa kijana huyo uliokuwa umekatwakatwa vibaya, ulipatikana kando ya barabara, karibu na duka hilo, siku tatu baada ya kuripotiwa kutoweka.

Taarifa zimeeleza kwamba kijana huyo alikuwa amemaliza mtihani wake wa kidato cha nne (KCSE) 2021, akisubiri matokeo.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger