Thursday 28 April 2022

POLISI, MAHABUSU WAFARIKI KWA AJALI GEITA

...


Watu wanne ambao ni askari wa Jeshi la Polisi wawili na mahabusu wawili wamefariki dunia, kwenye ajali iliyotokea katika kijiji cha Ibanda mkoani Geita.

Ajali hiyo imetokea April 27 majira ya saa 10:00 jioni ikihusisha gari la Polisi namba PT 3798 Toyota Landcruiser lililokuwa likitokea Geita kusikiliza kesi mahakamani, kugongana na Lori aina ya Scania namba T 691 DBQ mali ya kampuni ya Nyanza lililokuwa likitokea mkoani Mwanza kuelekea mkoani Geita.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita Henry Mwaibambe ameeleza chanzo cha ajali hiyo kuwa ni gari la Polisi kupata hitilafu.

Mganga Mfawidhi hospitali ya rufaa mkoa wa Geita Dkt. Mfaume Salum amesema alipokea majeruhi watatu na wote wamepatiwa matibabu mmoja anaweza kuruhusiwa.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger