Thursday 28 April 2022

HAYA NDIYO MAHARAGE YANAYOONGEZA NGUVU ZA KIUME

...

Maharage aina ya Jesca

KUTOKANA na kuwa na ongezeko kubwa la wanaume wenye upungufu wa nguvu za kiume tafiti zimeonesha kuwa kuna aina ya maharage yanayopatikana jijini Arusha na Tanzania kwa ujumla ambayo ni suluhisho la tatizo hilo.


Maharage hayo yanafahamika kwa jina la Jesca ambalo kimsingi limetokana na muunganiko wa herufi za kwanza za majina ya vijana wanne ambao waliamua kuungana na kufanya utafiti pamoja na kufanya uzalishaji wa maharage hayo ambayo wanadai yanapatikana kote nchini tena kwa bei ambayo ni rafiki kwa mteja.
Maharage aina hii yanaongeza nguvu za kiume

Vijana hao ni John, Elizabeth, Sostenes, Clement na Alex.

Maharage hayo yameongezwa viini lishe vya madini ya zinki na chuma ambavyo vinasaidia kuongeza uzalishaji wa homoni aina ya testosteroni pamoja na kuongeza damu mwilini,


Licha ya kwamba maharage hayo yamekuwa yakipewa majina mbalimbali kutokana na maeneo husika mathalani majina kama Iringa au Punda, lakini jina halisi ambalo watafiti hao wameliweka wazi kama jina la Kampuni ni JESCA.


Naye mtaalamu kutoka Taasisi ya Lishe Celestin Mgoba amesema maharage ya Jesca yameongezewa kwa wingi madini chuma na madini ya zinki kwa njia ya kilimo ambayo amedai kwa madini chuma ni lazima iwe miligramu 74 hadi 92 kwa kilo moja na zinki iwe miligramu 26 hadi 43 kwa kilo moja.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger