Friday 26 November 2021

BINTI AMSHTAKI DAKTARI KWA KUZALIWA

...

Picha ya Evie Toombess

Mwanamke anayefahamika kwa jina la Evie Toombess (20) amefungua kesi dhidi ya Daktari aliyemsaidia mama yake kujifungua kwa madai ya kwamba yeye hakustahili kuzaliwa.

Evie alizaliwa na tatizo la 'Spina Bifida' ambalo husababishwa na kutokukua vizuri kwa uti wa mgongo wa mtoto akiwa tumboni, pamoja na kuzaliwa na tatizo hilo Evie ni maarufu katika mchezo wa kuruka na farasi nchini Uingereza.

Evie anasema kama Dkt Phillip Mitchell angemshauri mama yake kutumia virutubisho vya 'Folic Acid' basi mama yake asingebeba ujauzito na yeye asingezaliwa na tatizo la 'Spina Bifida' ambalo humfanya kuvaa mirija masaa 24.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger