Monday, 6 January 2020

Tanasha Donna avunja kimya kuhusiana na madai ya Diamond Kuwa na Mpenzi Mwingine

...
Mpenzi Mkenya wa msanii Diamond Platinumz, Tanasha Donna hatimaye amevunja kimya chake baada ya kuibuka kwa maneno kuwa mwanamuziki huyo ana uhusiano wa pembeni.

Diamond anadaiwa kuwa katika uhusiano mwingine na mrembo wa Tanzania yapata miezi sita tu baada ya kumkaribisha mwanawe wa kiume Naseeb Junior.

Mama huyo wa mtoto mmoja kupitia ukurasa wake wa Instagram, aliwaomba watu kukoma kueneza habari ambazo macho yao hayajashuhudia kwa kutumia mdomo.

Ni bayana kuwa mrembo huyo alikuwa anajibu madai kuwa mpenziwe ana uhusiano na mwanadada kwa jina Rose.

Katika hali ya kuzima fununu kuhusu uhusiano wake, mtangazaji huyo wa radio ya NRG alisema mapenzi yake na Diamond hayawezi kuvunjika.

Donna alichapisha picha yake na Diamond katika hali ya mahaba na kuonyesha kuwa hawawezi kutengana hivi karibuni.


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger