Wednesday 26 June 2019

Wananchi 13,234 Wapatiwa Elimu Ya Madhara Ya Mimba Za Utotoni

...
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma
Jumla ya wananchi 13,234  wamefikiwa na elimu ya madhara ya mimba za utotoni hapa nchini .

Hayo yamesemwa leo bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya  jamii,jinsia wazee na watoto Dokta Faustine Ndugulie  wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum Fatma Tafiq aliyehoji,ndoa  za utotoni ni tatizo kubwa katika jamii zetu  hususan katika jamii zenye umasikini ,je ,serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kutoa elimu kwa umma hasa katika maeneo ya vijijini ili wananchi wafahamu athari za kuozesha watoto katika umri mdogo.
 
Katika majibu yake,Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia,Wazee na watoto Dokta Ndugulile amesema serikali ina tambua umuhimu wa elimu kwa umma katika kupambana na ndoa za utotoni ambazo zina madhara makubwa kwa watoto wa kike .
 
Hivyo amesema kupitia mbalimbali za mawasiliano ikiwemo TV,Radio,Magazeti na Majarida serikali imekuwa  ikitoa elimu kwa  kuandaa jumbe mbalimbali kuhusu madhara  ya mimba za utotoni sambamba na kusisitiza wazazi na walezi  na jamii kwa ujumla kutoozesha  watoto Mapema.
 
Aidha,Dokta Ndugulile ,amesema, Kwa kipindi cha Januari hadi Disemba mwaka  ,2018,Jumla ya Wananchi 13,234  wamefikiwa na Elimu ya Madhara ya Mimba za utotoni .
 
Kati ya hao,wanafunzi  8,546,walimu  476,viongozi wa dini 110,wazee wa mila na watu Mashuhuri 90,ngariba 38,waendesha bodaboda 261,wazazi/walezi  3600 na watendaji wa vijiji 113.
 
Kampeni ya  kutokomeza mimba za utotoni ijulikanayo’mimi Msichana Najitambua ilizinduliwa mkoani  Mara mwaka 2017 ambayo tayari imefanyika katika mikoa ya Shinyanga,Mara,Tabora,Lindi,Dodoma,Tanga,Dar   es  Salaam na Katavi.
 
Mikoa 6 yenye  kiwango kikubwa cha mimba za utotoni hapa nchini Tanzania ni Shinyanga,Dodoma,Tabora,Mara,Katavi na Singida  na takwimu zinaonesha kuwa asilimia 27% ya mabinti walio chini ya miaka 18 wana  mimba au wamezaa.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger