Friday 28 June 2019

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA

...

Manchester United inafikiria kumnunua beki wa Ufaransa na Barcelona Samuel Umtiti, 25. (Mundo Deportivo - in Spanish)
Mshambuliaji wa Manchester City na Ujerumani Leroy Sane, 23, anasalia kuwa mchezaji anayelengwa sana na mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich msimu huu licha ya mpango huo kusita hapo awali. (Sky Sports)

Mkufunzi wa klabu ya Sporting Marcel Keizer anaamini kwamba nafasi ya kumzuia kiungo wa kati wa Portugal Bruno Fernandez katika klabu hiyo ni ndogo, huku Manchester United ikiwa miongoni mwa klabu ambazo zimevutiwa na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 (Record, via Manchester Evening News)
Mkufunzi wa Celtic Neil Lennon ameambia Arsenal watahitajika kulipa zaidi iwapo watamsajili beki wa kushoto wa Uskochi Kieran Tierney, 22. (Telegraph)

Arsenal inamlenga mshambuliaji wa Monaco Keita Balde, 24, baada ya inter Milan kujiondoa katika harakati za kumsajili mchezaji huyo wa Senegal . (Le 10 Sport, via Metro)

Beki wa Borussia Dortmund na Ufaransa,20 Dan-Axel Zagadou, anataka kuondoka katika klabu hiyo na ananyatiwa na Arsenal. (Bild, via Mirror)

Babake mshambuliaji wa Juventus Moise Kean, 19, ametangaza kwamba raia huyo wa Itali anataka kuhamia Inter Milan". (Mirror)

Atletico Madrid inafikiria kumsajili mchezaji wa Real Madrid na Colombian James Rodriguez, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 akiwa ahitajiki tena Real . (Cadena SER, via AS)

Tottenham iko tayari kumnunua mchezaji anayelengwa na Arsenal William Saliba, huku klabu ya St-Etienne ikisema kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18 ana thamani ya £20m. (RMC, via Star)

Bayern Munich ilijaribu kuteka uhamisho wa beki wa klabu ya PEC Zwolle Sepp van den Berg kuelekea Liverpool wakati ambapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 17 kutoka Uholanzi alikuwa akifanyiwa ukaguzi wa matibabu. (Times)

Naibu mkufunzi wa Chelsea Gianfranco Zola ataondoka Chelsea wikendi hii wakati ambapo kandarasi yake itakuwa inakamilika baada ya kukataa ofa ya kuwa balozi wa klabu hiyo. (Guardian)

Manchester United itafanya uamuzi wa iwapo itamsaini beki wa katikati kufikia mwisho wa wiki hii.. (Manchester Evening News)

Kiungo wa kati wa Ufaransa Adrien Rabiot, anayelengwa na Manchester United, anaonekana kukaribia kuondoka katika klabu ya PSG baada mamake kufichua kwamba hakuna klabu iliowasilisha ofa yoyote kwa mwanawe(Daily Mail)

Mchezaji wa Real Madrid na Norway Martin Odegaard, 20, anatarajiwa kuondoka kwa mkopo kwa kipindi cha misimu mingine miwili (AS)

Kiungo wa kati wa Uingereza Sean Longstaff, 21, anatarajiwa kuripoti kwa mazoezi ya kujiandaa kwa msimu kama kawaida wiki ijayo licha ya kulengwa na Man United. (Chronicle)

Beki wa Arsenal na Poland Krystian Bielik anataka kuondoka katika klabu hiyo mwisho wa msimu huu . (Sun)

Mshambuliaji wa Ujerumani Bassala Sambou, 21, amekataa kandarasi mpya na klabu ya Everton na anatarajiwa kuhamia Ujerumani ama Eredivisie. (Liverpool Echo)

CHANZO.BBC SWAHILI
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger