Saturday 29 June 2019

Makonda Amuomba Radhi Rais Magufuli

...
Mwenyekiti wa Kamati ya Hamasa ya Taifa Stars, Paul Makonda amemuomba radhi Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, John Pombe Magufuli kufuatia Stars kupoteza mechi ya pili mfululizo.

Makonda ameomba radhi hiyo jijini Cairo kwamba kila Mtanzania alikuwa na imani ya kupata ushindi katika mchezo dhidi ya Harambee Stars ambapo Stars ilifungwa bao 3-2.

Makonda amesema Watanzania wanapaswa kuendelea kuiombea timu yao na kuiunga mkono kwani matokeo hayo ni sehemu ya mchezo.

Mkuu huyo alisema licha ya Stars kupoteza ameridhika na jinsi kikosi hicho kilivyocheza kwa nguvu ikiwa ni tofauti na mchezo wa kwanza waliofunga na Senegal bao 2-0.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger