Wednesday 26 June 2019

Mbunge Jaguar wa Kenya Aliyetishia Kuwatimua Watanzania Ndani ya Masaa 24 Akamatwa Mchana Huu

...
Maafisa wa polisi nchini Kenya wamemkamata mbunge wa jimbo la Starehe anayedaiwa kutoa kauli za chuki dhidi ya wafanyabiashara wa Tanzania na Uganda waliopo jijini Nairobi.

Vyombo vya habari vya nchi hiyo vinaripoti kuwa Charles Kanyi maarufu kama Jaguar amekamatwa mchana huu akiwa anatoka kwenye viwanja vya bunge.

Jana, June 25 Serikali ya Kenya ilitoa taarifa ya kuwahakikishia wafanyabiashara wa kigeni nchini humo usalama wakati wote huku ikisema Serikali haipo upande wa Mbunge wa Starehe, Charles Njagua maarufu Jaguar kuhusu kauli alizozitoa.

Mbunge huyo ambaye pia ni mwanamuziki kupitia mitandao ya kijamii jana Jumanne ilisambaa video yake akieleza kuwafukuza wafanyabiashara wa kigeni wakiwemo Watanzania ndani ya masaa 24 kurudi kwao la sivyo watawapiga na kuwarudisha nchini mwao..




Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger