Thursday 9 February 2017

Vita dhidi ya dawa za kulevya DSM Watu maarufu wakiwemo wanasiasa waguswa

...

Sakata la dawa za kulevya katika jiji la dsm limeendelea kutikisa watu maarufu,wakiwemo wafanyabiashara na wanasiasa Pamoja na Kiongozi maarufu wa dini ambao wametakiwa kwenda kituo cha polisi cha kati siku ya ijumaa kwa ajili ya mahojiano.
Mkuu wa Mkoa wa dsm Paul Makonda akizungumza na vyombo vya habari ametangaza Orodha mpya ya watu 65 ambao wanadaiwa kujihusisha kwa namna moja au nyingine katika kuuza au kusaidia kuingiza dawa za kulevya hapa nchini au nje ya nchi.
Baadhi ya watu maarufu wanaotakiwa kuripoti kituo cha polisi cha kati Siku ya Ijumaa ni pamoja na Mbunge mstaafu wa kinondoni Iddi Azzan,Mfanyabiashara Yusuph manji,Mbunge wa hai Freeman Mbowe,mchungaji Josephat Gwajima,huku wafanyabiashara maarufu akiwemo Hussein pamba kali ,mwinyi machapta pamoja na boss Chizenga wakazi wa kinondoni.
Aidha makonda amewataka wamiliki wa hotel wakiwemo Cassino sea cliff,Parm beach casino,Sleep way ,Yatch Club pamoja na Viongozi wa makampuni ya mafuta yakiwemo GBP,Tanga Petrolium,na Nas Hauleg nao kujisalimisha Polisi siku ya ijumaa.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger