Monday 13 February 2017

Dkt. Slaa amtumia ujumbe Gwajima kuhusu Dawa za Kulevya

...
Vita ya kupambana na dawa za kulevya nchini iliyopamba moto zaidi na kuzua mijadala tangu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alipoanza kutaja majina ya watuhumiwa imemuibua Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dkt. Wilbroad Slaa.

Dkt. Slaa ameibuka baada ya kutajwa na kuhojiwa kwa Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ambaye alikuwa rafiki yake na ‘muwezeshaji’ wake kabla siasa za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 hazijawageuza kuwa mahasimu.

Akizungumza jana kanisani kwake wakati akiwasimulia waumini wake mkasa uliompata tangu alipowasili katika kituo cha kati cha polisi jijini Dar es Salaam hadi alipoachiwa, Askofu Gwajima alisema kuwa alipokea ujumbe wa Dk. Slaa ambaye alimtetea dhidi ya tuhuma hizo.

Ujumbe wenyewe umewekwa kwenye ukurasa wa Facebook wa Askofu Gwajima na unasomeka hivi hapa chini
 
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger