Tuesday 21 February 2017

SHAMSA FORD AMLILIA MUMEWE ALIEKAMATWA KWA KESI YA MADAWA YA KULEVYA

...
Mwigizaji Shamsa Ford ambaye ni mke wa Mfanyabiashara Chidi Mapenzi aliyeitwa Polisi kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya, ameandika yafuatayo ikiwa ni mara ya kwanza toka aitwe Polisi kuhojiwa.

Shamsa amepost ujumbe huu kupitia Instagram “nilipoolewa nilijua ipo siku nitapitia hivi vitu huzuni,furaha, maudhi, kudharauliwa, kuchekwa na nk.ila pamoja na yote hayo haitabadilisha mapenzi yangu kwa mume wangu kipenzi”

“Nina amini kuwa wewe ni mume aliyenipa Mungu na wala Mungu hakutukutanisha kwa bahati mbaya.Dunia nzima ikuzomee na kuamini kile wanachoamini lakini jua una mke anayekupenda kwa dhati“

“Ninakujua, ninakuamini na kukupenda sana ndomaana niliolewa na wewe kwasababu nilijua utakuwa baba bora kwa mwanangu kama ambavyo ulivyo sasa..Nina amini Mungu anapotaka kukupeleka sehemu anayoitaka yeye lazima akupitishe kwenye mitihani”

“Hii ni mitihani ya Mwenyezi Mungu na nina imani inshaallah yatapita..Nakupenda sana mume Wangu kipenzi Rashidi..“
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger