Monday 6 February 2017

Uporaji kwenye maduka, bodaboda wazua hofu

...

Mbeya. Wamiliki wa maduka, bodaboda na glosari jijini hapa wameingiwa hofu baada ya kuibuka kundi la watu wanaodaiwa kuwa majambazi wanaopora fedha na pikipiki tangu mwishoni mwa Januari.

Mitaa iliyoonja adha ya wavamizi hao ni ya Mafiati, Mwanjelwa, Mabatini, Soweto na Mabanzini ambako vikundi hicho vilivunja maduka matano.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari alisema  wanawashikilia watu watatu wakituhumiwa kuhusika na matukio hayo.

Kidavashari alisema upelelezi wa awali unaonyesha kundi hilo la watu hutoka Tunduma mkoani Songwe na hupokewa na wenyeji ambao huwaongoza katika uporaji.

 Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Bodaboda Kanda ya Soweto, Joseph Patrick alisema hivi karibuni kuna watu waliofika eneo hilo saa 3:00 usiku waliowavamia madereva na kuwapora fedha na baadaye walivamia Mtaa wa Block Q walikopora pikipiki mbili.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger