Baadhi ya mitambo katika jengo karibu na Ziwa Victoria,hii inatumika kusukuma maji hadi katika kituo cha Kutibu Maji cha Ihelele kilomita chache kutoka Ziwani




Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi kutoka Mamlaka ya Maji Arusha (AUWSA) Jackline Mkindi, akizungumza mara baada ya kuhitimisha ziara yao Mkoani Shinyanga kwa kutembelea KASHWASA.






























Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza katika mkutano na wananchi wa kijiji cha Nyachoka wilayani Serengeti mkoani Mara wakati wa zoezi la kukabidhi hati miliki za kimila tarehe 12 Julai 2022
Sehemu ya wananchi wa kijiji cha Nyachoka wilayani Serengeti mkoa wa Mara wakimsikiliza Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alipokwenda kutoa hatimiliki za kimila tarehe 12 Julai 2022
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akimkabidhi kitabu cha mpango wa matumizi ya ardhi Mwenyekiti wa kijiji cha Nyichoka wilayani Serengeti mkoa wa Mara Imanuel Cairo Sochora wakati wa zoezi la kukabidhi hati miliki za kimila tarehe 12 Julai 2022.
Mkuu wa wilaya ya Serengeti mkoani Mara Vicent Mashinji akizungumza wakati wa zoezi la kugawa hatimiliki za kimila tarehe 12 Julai 2022. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi akizungumza na uongozi wa wilaya ya Serengeti na watendaji wa sekta ya ardhi tarehe 12 Julai 2022
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Serengeti (aliyevaa Kaunda) Ayoub Mwita akimuonesha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi eneo la kijiji cha Nyichoka katika ramani ya Sereneti wakati wa ziara ya siku moja katika wilaya hiyo tarehe 12 Julai 2022.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi akiangalia moja ya hati za kimila alizozikuta katika ofisi ya halmashauri ya wilaya ya Serengeti wakati wa ziara yake ya siku moja tarehe 12 Julai 2022. (PICHA NA WIZARA YA ARDHI)


Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba (kushoto) akizungumza na Bi.Tereza Stephano wa Kijiji cha Kisamwene wilayani Butiama kuhusu athari za matumizi ya kuni na mkaa katika mfumo wa upumuaji pamoja na faida za kutumia nishati safi ya kupikia. Waziri wa Nishati aligawa mtungi wa Gesi kwa kaya ya Bi. Tereza Stephano ili iweze kutumia kwa matumizi ya kupikia.
Waziri wa Nishati, January Makamba akizindua mradi wa umeme wa BUTUGURI wilayani Butiama mkoani Mara ambao utasambaza umeme katika Nyumba 287 na utagharimu Shilingi milioni 385. Mradi huu utawasaidia wananchi kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kufunga mashine za kusaga na kukoboa nafaka, uchomeleaji na upatikanaji wa huduma bora za kijamii ikiwemo maji baada ya umeme kufika katika miradi ya maji.
Bi.Tereza Stephano kutoka Kijiji cha Kisamwene wilayani Butiama mkoani Mara akimshukuru Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba baada ya kumkabidhi mtungi wa gesi utakaomwezesha kuachana na matumizi ya kuni na mkaa ambayo yanaleta athari katika mfumo wa upumuaji. Kulia kwa Waziri wa Nishati ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini ambaye pia ni Mbunge wa Butiama.
Dkt. Mary Mahenge kutoka Hospitali ya Mkoa wa Mara iliyopo wilayani Musoma akimweleza Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba ( wa Pili kutoka kushoto) kuhusu magonjwa ya mfumo wa hewa ni yanayotokana na kuchomwa kwa kuni na mkaa wakati Waziri wa Nishati alipofanya ziara mkoani Mara kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.