Friday, 15 July 2022

WAJUMBE AUWSA WATEMBELEA CHANZO CHA MAJI YA ZIWA VICTORIA, WAVUNA MADINI YA KUTOSHA KASHWASA

WAJUMBE wa Bodi ya Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira Jiji la Arusha (AUWSA),wametembelea na kukagua mtambo unaochakata na kusambaza maji ya ziwa Victoria kutoka mkoa wa Mwanza hadi Shinyanga na Tabora kwa kutumia mtambo huo.


Wajumbe hao wa Bodi ya Maji Arusha (AUWSA) wamefanya ziara hiyo Julai 14, 2022, wakiwa wameambatana na Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira Kahama Shinyanga (KASHWASA) mhandishi Patrick Nzamba na wajumbe wa bodi ya Maji Arusha, kwa lengo la kujifunza na kubadilishana mawazo juu ya utendaji kazi na Mamlaka ya Maji (KASHWASA).

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi kutoka Mamlaka hiyo ya Maji Arusha (AUWSA) Dk. Jackline Mkindi, amesema wamefanya ziara katika Mamlaka ya Maji Safi na usafi wa Mazingira Kahama ,Shinyanga (KASHWASA), ili kujifunza jinsi gani wanavyoweza kuendesha mamlaka yao na kupata matokeo chanya kama ilivyo KASHWASA.


Dk. Mkindi amesema katika ziara hiyo wamejifunza vitu vingi vizuri kutoka (KASHWASA), ambapo wao kama Bodi ya Maji Arusha (AUWSA) watakwenda kuvifanyia kazi na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi kwenye Mamlaka hiyo ya Maji Arusha.

“Tunaipongeza KASHWASA) kwa ubunifu wao mkubwa, wakutoa maji mkoa wa Mwanza hadi Shinyanga na kusambza huduma hiyo mikoa jirani ya kiwa safi na salama, huu ni ubunifu wa hali ya juu sana ambao sisi tumejifunza,”amesema Mkindi.

Awali Mkurugenzi mtendaji wa KASHWASA Mhandisi Patrick Nzamba akizungumza na wajumbe wa bodi ya maji kutoka AUWSA ameeleza kuwa lengo la kuanzishwa kwa mamlaka hiyo mwaka 2009 ilikuwa ni kutatua changamoto ya maji katika mji wa Shinyanga na Kahama lakini hivi sasa miji mingi inahitaji maji hayo kama vile (MwanzaNgudu,Shinyanga na Tabora) baadaye Isaka,Kishapu,Kagongwa,Igunga na Tabora.

Amesema wao ni wazalishaji wa maji wala siyo wasambazaji kwani kazi ya kusambaza maji kwa mteja mmoja mmoja inafanywa na mamlaka za maji katika miji husika kama vile KUWASA NA SHUWASA ambao ndiyo wateja wakubwa wa maji pamoja na kamati za maji za vijiji

Hata hivyo Mhandisi Nzamba amesema katika ziara hiyo imekuwa na mafanikio pia kwao, ambapo wamebadilishana mawazo na kupeana ushauri wa kiutendaji kazi hali itakayo saidia kuboresha utendaji kazi wa KASHWASA katika mkoa wa Shinyanga.

Baadhi ya mitambo katika jengo karibu na Ziwa Victoria,hii inatumika kusukuma maji hadi katika kituo cha Kutibu Maji cha Ihelele kilomita chache kutoka Ziwani





Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi kutoka Mamlaka ya Maji Arusha (AUWSA) Jackline Mkindi, akizungumza mara baada ya kuhitimisha ziara yao Mkoani Shinyanga kwa kutembelea KASHWASA.










Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULAI 15, 2022


Magazetini leo Ijumaa Julai 15, 2022


Share:

Wednesday, 13 July 2022

UGONJWA WA AJABU WAIBUKA TANZANIA.. RAIS SAMIA "HATUJUI NI KITU GANI....WATAALAMU WAMEPIGA KAMBI"

 Na Veronica Mrema

Homa kali, mwili kuchoka, shida ya kupumua na kutoka damu puani, ndizo dalili za awali ambazo zimeripotiwa za ugonjwa usiojulikana uliozuka huko Kusini mwa Tanzania.


Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Aifello Sichwale amebainisha dalili hizo alipozungumza na EAST Africa Radio.


"Timu bado ipo 'site', wakija {na ripoti kamili}, tutaeleza Umma sasa bado ni mapema.


"Mkoa wa Lindi wanajaribu kufuatilia hii shida ni nini?


"Dalili tulizoambiwa homa kali, mwili kuchoka, kupata shida ya kupumua na kutoka damu puani, ndizo  wanazosema," amesema.


Dkt. Sichwale ameongeza"Timu yetu ya idara ya magonjwa ya dharura na majanga na nyingine kutoka Idara ya Kinga katika Kitengo cha epidemiolojia.


"Timu ya afya ya Mkoa na halmashauri na idara ya mifugo wanaendelea na ufuatilia, taarifa itatolewa na Waziri wa Afya, tuwe na subra" amesema.


Julai 13, 2022 {jana}, akizungumza katika Maadhimisho ya Mkutano wa 20 wa AMECEA, Rais Samia Suluhu Hassan alisema ugonjwa umeingia huko Kusini mwa Tanzania, watu wengi wanatoka damu puani na kudondoka.


"Ingekuwa mmoja tungesema labda ana 'presha' {Shinikizo la damu} au 'veins' zimepasuka {puani}, Lakini ni wengi wanadondoka kwa mara moja," alisema.


Ingawa hakubainisha takwimu, Rais Samia alithibitisha kwamba tayari wataalamu wa afya wamehamia {wamepiga kambi} huko wakifuatilia kwa kina ugonjwa huo.


Rais Samia ameongeza "Hatujui kitu gani wataalamu na wanasayansi wamehamia huko wanaangalia.


Chanzo : Matukio na Maisha blog

Share:

AJALI YA GARI MCHOMOKO YAUA WATU WATANO SIMIYU.

 

Watu watano wamefariki dunia na wengine 11 wamejeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Magereza nje kidogo ya mji wa Bariadi Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu usiku wa kuamkia leo Julai 13, 2022.


Kamanda wa Polisi Mkoa Simiyu, Blasius Chatanda amesema kuwa ajali hiyo imehusisha magari madogo ya abiria.

"Nimefika eneo la ajali nimeona waliofariki wote ni wanaume. Gari moja mchomoko lilikuwa likitokea Lamadi na lingine Bariadi. Dereva aliyekuwa akitoka Lamadi aliova-take ndipo akakutana na mwenzake. Chanzo ni mwendo kasi. Madereva wamejeruhiwa na wapo chini ya ulinzi,"amesema
Share:

RAIS SAMIA ARIDHIA WADAIWA SUGU KODI YA ARDHI KUSAMEHEWA RIBA


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza katika mkutano na wananchi wa kijiji cha Nyachoka wilayani Serengeti mkoani Mara wakati wa zoezi la kukabidhi hati miliki za kimila tarehe 12 Julai 2022 Sehemu ya wananchi wa kijiji cha Nyachoka wilayani Serengeti mkoa wa Mara wakimsikiliza Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alipokwenda kutoa hatimiliki za kimila tarehe 12 Julai 2022Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akimkabidhi kitabu cha mpango wa matumizi ya ardhi Mwenyekiti wa kijiji cha Nyichoka wilayani Serengeti mkoa wa Mara Imanuel Cairo Sochora wakati wa zoezi la kukabidhi hati miliki za kimila tarehe 12 Julai 2022.

Mkuu wa wilaya ya Serengeti mkoani Mara Vicent Mashinji akizungumza wakati wa zoezi la kugawa hatimiliki za kimila tarehe 12 Julai 2022. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

Na Munir Shemweta, SERENGETI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameridhia kusamehewa riba ya kodi ya pango la ardhi kwa wadaiwa sugu kwa masharti kwamba wadaiwa hao wawe wamelipa madeni yq msingi ndani ya miezi sita kuanzia mwezi julai hadi desemba 2022.

Hayo yamebainishwa tarehe 12 Julai 2022 na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula katika mkutano na wananchi wa kijiji cha Nyachoka wilayani Serengeti mkoani Mara wakati wa zoezi la kukabidhi hati miliki za kimila.

Jumla ya hatimiliki za kimila 6,155 zimekamilika na kutolewa kwa wananchi wa vijiji 22 katika wilaya ya Serengeti ambapo hati 1621 sawa na asilimia 26 zimekamilishwa kwa ajili ya akina mama na hatimiliki 1519 sawa na asilomia 25 ni za umiliki pacha kati ya wanaume na wanawake.

Dkt Mabula alisema yeye pamoja na Waziri wa Fedha ambaye ndiye mwenye dhamana ya kusamehe watakutana na kupanga namna bora ya kutekeleza msamaha huo.

"Najua kuna wengi wanadaiwa madeni ya muda mrefu kwa hiyo kumetokea msamaha kuanzia mwezi julai mpaka desemba mwaka huu, watakaoweza kulipa ndani ya miezi hii sita, wale ambao madeni yao yana miaka mitano kurudi nyuma watalipa bila ile tozo ya riba" alisema Dkta Mabula.

" Mhe mama samia ameridhia kupitia waziri wa fedha kwa kushirikiana na waziri wa ardhi waweke utaratibu mzuri wa ninyi kuondolewa tozo ile na msamaha ni wa miezi sita tu kama una ndugu mpigie simu mwambie serikali ya awamu ya sita chini ya mama samia imetoa msamaha kwa wadiwa sugu ili watoke katika jina baya la wadaiwa sugu kwenda kulipa madeni bila riba" alisema Dkt Mabula

Kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi, mmiliki wa ardhi atakayeshindwa kulipa madeni yake katika kipindi cha miezi hiyo sita basi atadaiwa madeni yake pamoja na riba na akishindwa kufanya hivyo atafikishwa kwenye vyombo vya sheria ambako huko uamuzi wake ni kulipa ama kunyang'anywa ardhi anayoimiliki.

Akigeukia zoezi la utoaji hatimiliki za kimila Dkt Mabula alisema, hatua ya kumilikishwa ardhi kwa nyaraka kuna faida kubwa katika maisha ya kila siku na kutaja baadhi ya faida hizo kuwa ni pamoja na usalama wa ardhi, uhakika wa milki, kupunguza migogoro pamoja na nyaraka hiyo kutumika kama dhamana.

Zaidi ya wananchi 6000 katika vijiji 22 wamepangiwa matumizi bora ya ardhi katika maneo yao na kuwekewa mipaka ya kudumu ili kuepuka migogoro ya mipaka kwenye ardhi zao

Serikali kupitia halmashauri ya wilaya ya Serengeti, Shirika la Hifadhi la Taifa Serengeti (SENAPA) na Shirika la Frankfurt Zoological Society (FZS) kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KFW) kupitia mradi wa utunzaji na uendelezaji wa Ikolojia ya Serengeti waliingia makubaliano ya pamoja kwa ajili ya kuwezesha uandaaji wa mpango wa matumizi ya ardhi ya vijjji vinavyopakana na maeneo yaliyohifadhiwa yanayounda ikolojia ya serengeti inayojumuisha hifadhi za taifa na mapori ya akiba.

Madhumuni ya mradi huo ni pamoja na kupunguza migogoro ya matumizi ya ardhi kati ya vijiji na eneo la hifadjhi , kutatua migogoro ya mipaka kati ya maneo ya kiutawala pamona na kutoa elimu ya uhifadhi na sheria mbalimbambalj zinazosimamia mipango ya matumiZi ya ardhi nchini
Share:

WAZIRI DKT MABULA AIPA WIKI MBILI HALMASHAURI YA SERENGETI


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi akizungumza na uongozi wa wilaya ya Serengeti na watendaji wa sekta ya ardhi tarehe 12 Julai 2022Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Serengeti (aliyevaa Kaunda) Ayoub Mwita akimuonesha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi eneo la kijiji cha Nyichoka katika ramani ya Sereneti wakati wa ziara ya siku moja katika wilaya hiyo tarehe 12 Julai 2022.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi akiangalia moja ya hati za kimila alizozikuta katika ofisi ya halmashauri ya wilaya ya Serengeti wakati wa ziara yake ya siku moja tarehe 12 Julai 2022. (PICHA NA WIZARA YA ARDHI)

***************

Na Munir Shemweta, SERENGETI

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameipa wiki mbili halmashauri ya wilaya ya Serengeti mkoani Mara kumpatia taarifa ya hali ya mashamba 36 yaliyopo katika halmashauri hiyo ili yale mashamba yasiyoendelezwa yaweze kubatilishwa umiliki wake.

Hatua hiyo inafuatia kuelezwa kupitia taarifa ya sekta ardhi ya halmashauri ya wilaya ya Serengeti kuwa wilaya hiyo ina mashamba yaliyopimwa 36 kulingana na taarifa iliyopatikana kutoka wizarani kutokana na kutokuwepo kumbukumbu za kutosha mashamba hayo katika wilaya hiyo.

Taarifa hiyo iliyosomwa na nAfisa Ardhi Mteule wa Halmasahauri hiyo ya Serengeti Orwaka Nyamsusa ilieleza kuwa, mashamba hayo yalipimwa vijijini bila kufuata taratibu za uhaulishaji na ilipotakiwa yamililishwe kwa kupewa hati za kawaida ilishindikana.

"Ninawapa Serengeti wiki mbili nijue status ya mashamba hayo na kama ni suala la kuanza kuyabatilisha, mchakato uanzie katika halmashauri ambayo ni mamlaka ya upangaji ili tuitangaze fursa kwa wawekezaji kama Serengeti tunayo mashamba 36 na kati ya hayo ni matano tu yenye umiliki halali’’. Alisema Dkt Mabula

Akizungumza na uongozi wa wilaya ya serengeti na watendaji wa sekta ya ardhi katika halmashauri hiyo tarehe 12 Juala 2022 wilayani humo, Dkt Mabula alisema haingii akilini mashamba pamoja na ardhi kuwa katika halmashauri hiyo lakini halmashauri husika haina kumbukumbu iwapo imeyapima mashamba hayo na badala yake inaenda kutafuta kumbukumbu wizarani.

Alibainisha kuwa, kama utaratibu wa kuisimamia sekta ya ardhi kwa halmashauri ya Serengeti utakuwa ni wa aina hiyo basi halmashauri hiyo haiwezi kufika popote katika masuala ya ardhi na itaendelea kuwa na changamato.

" Halmashauri ni mamlaka za upangaji kwa mujibu wa sheria namba 8 ya mipango miji ya 2007, ni mamlaka za upangaji zinazotakiwa kupanga miji yao wanataka iwe ya namna gani wizara kazi yake ni kusimamia na kuangalia kama shughuli za ardhi zinaenda kwa utaratibu au shetia zinafuatwa.

Alisema, halmashauri nyingi hazifuati takwa la sheria huku zikifahamu ni mamlaka za upangaji na kueleza kuwa halmashauri zote zinatakiwa kutekeleza takwa hilo na zisipotekekeza migogoro yq ardhi haiwezi kuisha.

Katika taarifa yake, halmashauri ya wilaya ya serengeti ilieleza kuwa wilaya hiyo ina jumla ya vijjji 78 ambapo kato ya hivyo vijjji 61 vimepimwa huku vijiji 10 kati ya hivyo vikitakiwa kufanyiea marejeo kutokana na makosa katika ramani za upimaji.

Aidha, jumla ya vijiji 29 kati ya 78 vina mpango wa matumizj bora ya ardhi ambapo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/ 2023 halmashauri hiyo imetenga kiaai cha shilingi 15,000,000 kwa ajili ya mpango wa matumizi bora ya ardhi kwenye vijiji 3
Share:

Tuesday, 12 July 2022

AJALI YAUA WATU NANE, KUJERUHI WATANO BUHARAMULO


Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera, William Mwampaghale

**
Watu nane wakiwamo watano wa familia moja ambao ni mama na watoto wake wanne, wamefariki dunia baada ya magari mawili kugongana uso kwa uso usiku wa kuamkia Julai 11, 2022, katika eneo la Busiri barabara kuu ya kutoka Lusahunga kuelekea Nyakahura wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera William Mwampaghale, amesema kuwa ajali hiyo imeyahusisha gari la mizigo lililokuwa likitokea nchini Rwanda kwenda Dar es Salaam, likiendeshwa na Vicent Gakuba (52) raia wa Rwanda, na Toyota Succeed lililokuwa likitokea eneo la Nyamalagala wilayani Biharamulo kuelekea Benaco wilayani Ngara likiendeshwa na Nyawenda Bihela (35) ambaye alifariki wakati wa ajali hiyo.

"Uchunguzi wa awali umeonesha ajali hiyo imetokana na uzembe wa dereva wa lori kutokana na kuhama kutoka upande wa kushoto wa barabara na kuendesha gari upande wa kulia, kitendo kilichosababisha magari hayo kugongana uso kwa uso na kusababisha vifo hivyo, miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti, katika kituo cha afya Nyakanazi Biharamulo" amesema Kamanda William.

Kamanda huyo amesema kuwa mbali na dereva pia watu wote waliokuwa katika gari aina ya Toyota Succeed walipoteza maisha, na kutaja majina yao kuwa ni Jesca Leonard (45), Magreth Sekanabo (14), Adidas Sekanabo (12), Zabron Sekanabo (6), Vedastina Sekanabo (8), Michael Charles (28) na Majaliwa Kanundo (32).

Chanzo - EATV
Share:

TEITI YATOA ELIMU KWA WANANCHI NAMNA INAVYOTIMIZA MAJUKUMU YAKE KWA MUJIBU WA SHERIA


Kamishna Msaidizi Tume ya Madini Tanzania na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirikisho la vyama vya wachimbaji wadogo wa madini (FEMATA) Haroun Kinega (kulia) akimsikiliza Afisa Msimamizi wa Fedha wa Taasisi ya Uhamasishaji, Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali madini, Mafuta na Gesi asilia (TEITI) Erick Ketagory (kushoto) alipokuwa katika Banda lao lililopo ndani ya banda kuu la STAMICO katika maonesho ya sabasaba leo Julai 11,2022 Jijini Dar es salaam.

Kamishna Msaidizi Tume ya Madini Tanzania na Afisa Mtendaji Mkuu wa (FEMATA) Haroun Kinega (kulia) akitia saini kwenye kitabu cha wageni mara baada ya kumaliza ziara yake fupi katika Banda hilo.

Afisa Msimamizi wa Fedha wa Taasisi ya Uhamasishaji, Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) Erick Ketagory (wa kwanza kulia) akiwa na afisa habari wa Taasisi hiyo Godwin Masabala 9wa pili kulia) wakizungumza na wageni waliotembelea kwenye banda lao kufahamu jinsi taasisi hiyo inavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria.


Na: Mwandishi wetu Dar.


Afisa Mawasiliano wa Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) Godwin Masabala amesema kuwa Taasisi hiyo imedhamiria kutoa elimu kwa wananchi ili kuwajengea uelewa wa namna inavyotimiza majukumu yake ya Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini,Mafuta na Gesi Asilia kwa mujibu wa Sheria.


Ameyataja majukumu yao wanayoyasimamia kwa mujibu wa sheria ni pamoja na kuweka wazi taarifa za Mapato ya Serikali na malipo ya Kodi yanayotoka kwenye Kampuni za Madini,Mafuta na Gesi Asilia kwa Umma ili kuhamasisha Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali hizo.


Masabala ameyasema hayo katika mahojiano maalum na waandishi wa habari yaliyofanyika Julai 11,2022 katika Banda lao lililopo ndani ya Banda kuu la STAMICO kwenye Maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayofanyika katika Viwanja vya Mwl. Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.


Amefafanua kua Taasisi hiyo imeundwa kwa Sheria namba 23 ya TEITA ya mwaka 2015 ambayo imeunda Kamati ya Uwazi na Uwajibikaji (Kamati ya TEITI) yenye wajumbe nane(8) na inaongozwa na Mwenyekiti ambaye ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mstaafu Ludovick Utouh na kazi za kila siku za TEITI zinatekelezwa na Katibu Mtendaji.


"Taasisi hii ina wajibu mkubwa wa kuhamasisha Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini,Mafuta na Gesi Asilia" amefafanua.


Share:

KUHANI MWAKIBINGA : JITOKEZENI KWA WINGI KUHESABIWA SIKU YA SENSA

 

Kuhani Ayubu Mwakibinga

Na Derick Milton, Bariadi.

Kiongozi wa Kanisa la World Miracle Mission Central (WMCC) kutoka Mkoani Shinyanga Kuhani Ayubu Mwakibinga amewataka wahumini wa kanisa hilo kujitokeza kwa wingi katika zoezi la sensa na makazi.


Amesema kuwa zoezi hilo ambalo litafanyika Agosti 23, 2022 ni muhimu sana kwa nchi ambayo inataka kuwaletea watu wake maendeleo, ambapo ameeleza yeye atakuwa mstari wa mbele siku hiyo kwenda kuhesabiwa.


Kiongozi huyo wa Dini amesema hayo jana mjini Bariadi wakati wa mkutano wake wa injili uliofanyika mjini Bariadi na kuhudhuliwa na mamia ya wananchi wa mji wa Bariadi wakiwemo wahumini wake.


Alisema kuwa zoezi la sensa linatakiwa kuungwa mkono na kila mtanzania mpenda maendeleo, kwani serikali haiwezi kuleta miundombinu mbalimbali kwa wananchi bila ya kujua wako wangapi na wanahitaji nini.


Aliongeza kuwa watu wengi wamekuwa wakilalamikia serikali kwa kushindwa kuwaletea huduma za mbalimbali za kijamii, ambapo ameeleza ili serikali iweze kutimiza jukumu hilo lazima ijue ina watu wangapi.


Amewataka wahumini wake kila mmoja kuhakikisha anamwasisha mwezake kwenda kuhesabiwa Agosti 23, 2022, ili serikali iweze kuweka mipango yake ya kuwaletea watanzania maendeleo.


“ Agosti 23, 2022 ni siku ya sensa kitaifa, na sisi kama raia wa nchi hii, ambayo inaoongoza na mmama yetu mpendwa Samia Suluhu Hassan tunao wajibu wa kumuunga mkono Rais wetu kwa kujitokeza kwa wingi siku hiyo kuhesabiwa, Mimi nitakuwa mstari wa mbele kuhesabiwa.” Alisema Kuhani Mwakibinga…..


“ Nchi lazima iwe na takwimu, tukipanga maendeleao tujue wako wangapi, tunaweka pale kulingana na takwimu na watu wako pale, tusipohesabiwa tutajua watu wako wangapi?....


Katika hatua nyingine Kiongozi huyo wa Dini amewataka wahumini wake kuendelea kumwombea Rais Samia kwani amekuwa kiongozi mwenye maono wa kuletea maendeleo kwa kasi wananchi wake.


“ Tumemwona Rais wetu kwa kipindi hiki kifupi amejenga shule, vituo vya Afya kwa wingi sana, tunao wajibu wa kumlinda kiongozi wetu kwa kumwombea na wale wenye nia mbaya na yeye” ,alisema Kuhani Mwakibinga

Share:

WAZIRI WA NISHATI AANZA UHAMASISHAJI WA MATUMIZI SAFI YA NISHATI NCHINI


Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba (wa Tatu kutoka kulia) akizungumza na Mwakilishi wa Kikundi cha Kusama, Bi.Beatrice Mbaga kuhusu athari za kiafya zinazotokana na matumizi ya mkaa na kuni wakati akiwa wilayani Musoma, mkoani Mara ambapo alikabidhi mitungi Sita ya Gesi na kuahidi kufunga mfumo wa gesi kwa kikundi hicho ambacho kinatumia kuni na mkaa kukaanga dagaa.

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba (kushoto) akizungumza na Bi.Tereza Stephano wa Kijiji cha Kisamwene wilayani Butiama kuhusu athari za matumizi ya kuni na mkaa katika mfumo wa upumuaji pamoja na faida za kutumia nishati safi ya kupikia. Waziri wa Nishati aligawa mtungi wa Gesi kwa kaya ya Bi. Tereza Stephano ili iweze kutumia kwa matumizi ya kupikia.

Waziri wa Nishati, January Makamba akizindua mradi wa umeme wa BUTUGURI wilayani Butiama mkoani Mara ambao utasambaza umeme katika Nyumba 287 na utagharimu Shilingi milioni 385. Mradi huu utawasaidia wananchi kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kufunga mashine za kusaga na kukoboa nafaka, uchomeleaji na upatikanaji wa huduma bora za kijamii ikiwemo maji baada ya umeme kufika katika miradi ya maji.

Bi.Tereza Stephano kutoka Kijiji cha Kisamwene wilayani Butiama mkoani Mara akimshukuru Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba baada ya kumkabidhi mtungi wa gesi utakaomwezesha kuachana na matumizi ya kuni na mkaa ambayo yanaleta athari katika mfumo wa upumuaji. Kulia kwa Waziri wa Nishati ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini ambaye pia ni Mbunge wa Butiama.

Dkt. Mary Mahenge kutoka Hospitali ya Mkoa wa Mara iliyopo wilayani Musoma akimweleza Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba ( wa Pili kutoka kushoto) kuhusu magonjwa ya mfumo wa hewa ni yanayotokana na kuchomwa kwa kuni na mkaa wakati Waziri wa Nishati alipofanya ziara mkoani Mara kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

………………………..

Ikiwa ni utekelezaji wa moja ya vipaumbele vya Wizara ya Nishati katika Bajeti ya mwaka 2022/2023, Waziri wa Nishati, January Makamba ameanza kazi ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia katika mikoa mbalimbali nchini ambapo Awamu ya kwanza ya uhamasishaji inayojumuisha mikoa 14 na Wilaya 38 imeanzia mkoani Mara.

Katika siku ya kwanza ya kazi, Waziri wa Nishati, alizungumza na makundi mbalimbali ya wananchi katika Wilaya za Musoma, Butiama na Bunda na kugawa mitungi ya Gesi kwa vikundi mbalimbali pamoja na kaya maskini.

“Sisi kama Wizara ya Nishati moja ya mambo tunayosimamia ni nishati ya umeme, nishati ya kupikia na ya kwenye magari ila nishati ya kupikia tumekuwa hatuigusi, lakini hii ni nishati ambayo kila mtanzania lazima atumie, hivyo kuanzia mwaka huu, tumeamua kutoa kipaumbele kikubwa katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.” Alisema Makamba

Alieleza kuwa, kwa hapa Tanzania wananchi takriban Elfu 22 wanakufa kwa mwaka kutokana na magonjwa ya njia ya kupumua yanayosababishwa na kutumia mkaa na kuni ambapo kwa Mkoa wa Mara takriban wananchi 400 hadi 600 huugua kwa mwaka kutokana na matumizi hayo hivyo athari hizo pia zinaipa msukumo Serikali katika kuwahamasisha wananchi kutumia nishati safi.

Kuhusu changamoto za bei ya gesi ya mitungi ambayo inafanya wananchi wengi kuendelea kutumia kuni na mkaa, alieleza kuwa Serikali inachukua hatua mbalimbali ikiwemo kupunguza kodi ili familia mbalimbali ziweze kumudu bei ya mitungi ya gesi.

Suala la athari za matumizi ya kuni na mkaa, lilitiliwa mkazo na Dkt. Mary Mahenge kutoka Hospitali ya Mkoa wa Mara iliyopo wilayani Musoma ambaye alieleza kuwa, kwenye nchi zinazoendelea, sababu kubwa ya magonjwa ya mfumo wa hewa ni kuchomwa kwa kuni na mkaa na kwamba kinacholeta madhara kwenye matumizi hayo ni moshi ambao una hewa ya carbonmonoxide ambayo ikiwa nyingi inaweza kusababisha pia vifo vya ghafla.

Akiwa wilayani Musoma alikabidhi mitungi Sita ya Gesi kwa Kikundi cha Kusama ambacho kinakaanga dagaa kwa kutumia kuni na mkaa pamoja kuahidi kufunga mfumo wa gesi ambao utasaidia kikundi hicho kufanya kazi kwa ufanisi.

Mwakilishi wa Kikundi cha Kusama, Bi.Beatrice Mbaga ambaye alisema macho yake yameathirika kutokana na kupikia kuni kwenye biashara hiyo kwa miaka 17, alimshukuru Waziri wa Nishati, January Makamba kwa ahadi aliyoitoa ya kufungiwa mfumo wa gesi ambao utahamasisha pia vikundi vingine vya wajasiriamali kutumia nishati safi kwenye kazi zao.

Aidha, akiwa wilayani Butiama katika Kijiji cha Kisamwene, aligawa mtungi wa Gesi kwa kaya maskini ya Bi. Tereza Stephano ambaye alimshukuru Waziri wa Nishati kwa kupata nishati hiyo safi ya kupikia ambayo itamrahisishia shughuli za upishi huku akiwa na uhakika wa usalama wa afya ya familia yake.

Pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati safi mkoani Mara, akiwa wilayani Butiama, Waziri wa Nishati alizindua mradi wa umeme wa Butuguri ambao utasambaza umeme katika kaya 287 na utagharimu shilingi milioni 385 ambapo mradi huo utawawezesha wananchi wa eneo hilo kuboresha huduma za kijamii na kiuchumi ikiwemo kujiajiri.

Pia, Waziri wa Nishati alizindua huduma ya Ni-Konekt kwa Mkoa wa Mara ambapo huduma hiyo inawawezesha wananchi kupata huduma mbalimbali zinazotolewa na TANESCO kwa njia ya mtandao ikiwemo maombi ya kuunganishiwa umeme.

Ziara ya Waziri wa Nishati iliyoanza tarehe 11 Julai 2022, itakuwa ni ya siku 21 ambapo atahamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na kukagua miradi mbalimbali ya nishati katika Mikoa 14, Wilaya 38 na Majimbo 41.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger