Monday, 19 January 2026

WANA SANTA RC BUNJU WAPIGWA MSASA MATUMIZI SAHIHI YA MITANDAO

...


Wanakwaya wa Mt. Joseph, Parokia ya Mlima Karmeli Bunju, Jimbo la Bagamoyo wakiwa Zanzibar kushiriki moja ya matamasha makubwa nchini kwa mwaliko.

**
Wanakwaya wa Mt. Joseph, Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmel Bunju, jimbo la Bagamoyo wameaswa kutumia vema mitandao ya kijamii kutangaza kwaya yao na ujasiriamali ili kujiongezea kipato.

Wito huo umetolewa Januari 18,2026 Parokiani hapo na Msemaji wa kwaya hiyo Bi. Rose Ngunangwa wakati wa mafunzo kwa wanakwaya hao ambapo amesisitiza pia umuhimu wa kuwa na nidhamu na kuheshimu utu mitandaoni.

“Kama vijana wa kikatoliki na wanakwaya ninawaasa kuheshimu utu wa watu mitandaoni na kutochangia kutweza, kudhalilisha au kutusi mtu. Tumieni mitandao kunadi kazi zenu ili kuongeza kipato. Naomba msiwe watumwa wa historia hata kama hukubahatika kufanya vema kwenye masomo tumia karama ulizonazo kutengeneza kipato,” amesisitiza.

Katika miaka ya hivi karibuni, kwaya ya Mt. Joseph Bunju imejipatia umaarufu mkubwa katika uimbaji huku baadhi wakiita Tanzania 2 kutokana na uimbaji wenye sauti zilizopangiliwa.

Kwa sasa kwaya hiyo inatamba na nyimbo zake mpya kama Ishara ya Msalaba na Nia Yangu, nyimbo ambazo zinafanya vema kwenye majukwaa mbalimbali ya kidijitali.

Kwaya hiyo imeweza kushiriki matamasha makubwa ya kitaifa kama Mkatoliki Concert, Tamasha la Yesu ni Mwema na lile la Jubilei ya Miaka 25 ya Uaskofu  wa Mhashamu Augustine Shao wa Zanzibar ambapo ilijizolea mashabiki lukuki visiwani humo.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger