Wednesday, 6 November 2019

Sekta Ya Ngozi, Nyama Na Maziwa Zaundiwa Kozi Fupi Vyuoni

Na. Edward Kondela
Serikali imewataka wadau kwenye sekta ya ngozi, nyama na maziwa wanaoandaa mitaala kwa ajili ya vyuo kufundisha kozi fupi katika sekta hizo ngazi ya cheti na diploma kupitisha mitaala bora itakayohakikisha wanafunzi watakaohitimu mafunzo wanaleta matokeo chanya katika sekta hizo kwa wananchi na taifa kwa ujumla.

Akizungumza Jijini Dodoma wakati akifungua kikao kilichowahusisha wadau katika sekta za ngozi, nyama na maziwa kutoka serikalini na taasisi binafsi Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amesema ili kupata malighafi bora zinazotokana na sekta ya ngozi, nyama na maziwa ni lazima wataalam ambao wamesomea sekta hizo ngazi ya cheti na diploma wawekewe mazingira ya kuhakikisha wanatumia utaalam watakaoupata kupitia vyuo mbalimbali baada ya kupitishwa kwa mitaala hiyo ili iwe na tija kwa taifa.

“Mitaala mnayokwenda kupitia na kuzungumzia lazima ijibu mahitaji ya wadau katika sekta tatu yaani ngozi, nyama na maziwa isiwe kuwa na cheti baada ya kuhitimu mafunzo ngazi ya cheti au diploma hawa wataalamu wa ngazi ya kati ndiyo wanaotegemewa kwenda kufanya kazi za vitendo, hakikisheni mnapata mitaala ambayo itakuwa na manufaa.” Amesema Prof. Gabriel

Aidha Prof. Gabriel amewataka wadau hao kubainisha njia bora za kufundishia mara baada ya kupitishwa kwa mitaala hiyo ili kuhakikisha wanafunzi watakaodahiliwa wanaelewa vizuri pamoja na kuwa na utaratibu mzuri wa kuwapata watu ambao wanafundishika na wawe tayari kupokea mafunzo hayo.

Akibainisha juu ya jamii kuwa na ufugaji wenye tija, katibu mkuu huyo amewaasa wadau wa mifugo wajenge utamaduni wa kuwatumia wataalam hususan wa ngazi ya kati ili waweze kufuga kisasa na kunufaika kupitia mifugo yao badala ya kufuga kwa mazoea na hatimaye kupata hasara.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utafiti, Ugani na Mafunzo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Angello Mwilawa amesema mjadala wa kuandaa mitaala kwa ajili ya kufundisha vyuoni kozi fupi katika ngazi ya cheti na diploma kwenye kwenye sekta ya ngozi, nyama na maziwa umetoka kwa wadau, hivyo wizara ikashirikisha taasisi mbalimbali likiwemo Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) ili kukamilisha mitaala hiyo.

Dkt. Mwilawa amefafanua kuwa mara baada ya kukamilika kwa taratibu za kuandaa mitaala hiyo vyuo vya serikali kwa kushirikiana na binafsi vitaanza kutekeleza kwa kutoa mafunzo ya tasnia ya ngozi, nyama na maziwa katika ngazi ya cheti na diploma.

Akielezea umuhimu wa serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuandaa mitaala hiyo, Katibu wa Chama cha Wafugaji Tanzania Bw. Magembe Makoye ameipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuhakikisha sekta ya mifugo inasimamiwa vyema kupitia mambo ya kisera na kisheria ambayo ndiyo yamekuwa yakisimamia pamoja na kutunga kanuni mpya zenye lengo la kuhakikisha sekta ya mifugo inathaminiwa zaidi.

Bw. Makoye amesema sekta ya mifugo ambayo inaajiri watu wengi kote nchini kupitia mafunzo yatakayoanza kutolewa vyuoni mara baada ya kupitishwa kwa mitaala hiyo kutachangia kwa kiasi kikubwa kuongeza thamani ya sekta ya ngozi, nyama na maziwa kwa kuwa wafugaji sasa wataongezewa taarifa na maarifa kupitia kwa wataalamu watakaohitimu mafunzo hayo.

Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya ngozi, nyama na maziwa pamoja na taasisi mbalimbali likiwemo Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) inapitia mitaala kwa ajili ya kuanzishwa kwa kozi fupi ngazi ya cheti na diploma katika sekta hizo kwenye vyuo vya serikali na binafsi ili kuyaongezea thamani zaidi mazao ya ngozi, nyama na maziwa kwa kuwa na waatalamu wengi zaidi ngazi ya kati walipobobea katika sekta za ngozi, nyama na maziwa.


Share:

Serikali Yapiga Marufuku Walengwa Wa Tasaf Kulazimishwa Kuchangia Bima Za Afya Na Michango Ya Kijamii

Na. Aaron Mrikaria-Dodoma
Serikali imewaagiza Viongozi wa Vijiji kutowalazimisha walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kukatwa ruzuku kwa ajili ya kuchangia bima za afya na michango mbalimbali ya kijamii kwani ruzuku hiyo hutolewa na Serikali kwa ajili ya kuziwezesha kaya maskini kujikwamua kiuchumi.

Agizo hilo limetolewa Bungeni leo na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Kapt.

(Mst) Mhe. George H. Mkuchika (Mb), wakati akijibu swali la Mbunge wa Bahi, Mhe. Omary Ahmed Badwel aliyetaka kujua Utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika vijiji vyote nchini.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema, ruzuku inayotolewa na Serikali kwa walengwa ni kwa ajili ya kuwawezesha kupata mahitaji ya msingi kama vile chakula, gharama za elimu na Afya na kuwekeza katika kuanzisha miradi itakayowaongezea kipato na hatimaye kujikwamua na umaskini, hivyo ni maamuzi ya kaya husika kupanga matumizi ya ruzuku wanayoipata.

“Katika baadhi ya maeneo, Viongozi wa Vijiji wamekuwa wakiwalazimisha walengwa kukatwa ruzuku ili kulipia bima za afya na michango mbalimbali jambo ambalo si sahihi na halikubaliki”, Mhe. Dkt. Mwanjelwa amefafanua.

Aidha, Dkt. Mwanjelwa ameelekeza walengwa kutokatwa ruzuku moja kwa moja bila ridhaa yao bali wapewe stahiki zao na kama kuna michango ya shughuli za maendeleo ya kijiji inapaswa kutozwa kwa wananchi wote wa kijiji husika.

Dkt. Mwanjelwa amewataka viongozi wote waliokuwa wanatoa amri ya kukatwa kwa ruzuku za walengwa wa TASAF moja kwa moja bila ridhaa yao, waache mara moja kwani ni kinyume cha utaratibu na iwapo wataendelea, Serikali itawachukulia hatua za kali za kinidhamu na kisheria.

Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini tangu uanze kutekelezwa na Serikali mwaka 2013 umezinufaisha kaya maskini kwa asilimia 70, na hivi sasa Serikali inajiandaa kuanza utekelezaji wa Awamu ya Tatu sehemu ya pili mwishoni mwa mwaka huu baada ya Serikali kupata fedha lengo likiwa ni kuzifikia kaya zote maskini nchini


Share:

Serikali Yasema Haitaingilia Kupanga Bei Msimu Ujao Wa Pamba

Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema kuelekea msimu ujao wa pamba serikali itajitahidi kupunguza gharama na kwamba haitaingilia kupanga bei bali watatafuta njia nyingine za kumlinda mkulima na kuhakikisha hapati hasara.

Ametoa kauli hiyo bungeni leo Jumatano Novemba 6, alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Busega (CCM), Dk. Raphael Chegeni aliyetaka kupata tamko la serikali kuhusu wakulima wa pamba ambao waliuza pamba tangu Mei mwaka huu lakini hawajalipwa fedha zao.

“Wakulima wa pamba ambao mwaka hadi mwaka wamekuwa wakifanya kazi ya kulima wamekuwa wakipata hasara kwa mfano leo hii wakulima wa Mkoa wa Simiyu hasa wa Wilaya ya Busega wameuza pamba tangu mwezi Mei mpaka leo hawajaliwa fedha zao sasa hauoni kwamba hii ni kuwakatisha tamaa wakulima wasiweze kufanya kilimo kizuri zaidi na nini tamkola serikali juu ya hili,” amehoji.

“Ninakiri kuwa baadhi ya wakulima wa pamba hawajalipwa fedha zao, kwa mwaka huu mpaka sasa hivi jumla ya bilioni 417 zimeshalipwa kwa wakulima wa nchi nzima, ambao hawajalipwa wanadai bilioni 50 kufikia sasa hivi na sababu ya msingi ni lazima tufahamu kwamba asilimia zaidi ya 80 ya pamba inakwenda nje ya nchi, wanunuzi wetu wanakabiliwa na mtikisiko wa bei ambao umewakabili katika soko la dunia na sisi kama nchi tulitoa maelekezo ya bei ya kununulia na haya yalikuwa maamuzi ya serikali kwaajili ya kumlinda mkulima asipate hasara.

“Pamba yote iliyokuwa kwa wakulima imeshakusanywa sasa hivi kilichobaki mikononi mwa wakulima ni tani 5,000 tu ambayo tunaamini msimu unapoanza pamba yote ya wakulima itakuwa imeondoka, tunajitahidi kupunguza gharama msimu huu unaokuja na hatutaingilia kupanga bei, jukumu letu litakuwa ni kuhakikisha mkulima hapati hasara kwa kutafuta njia nyingine za kumlinda kuliko kumuathiri mnunuzi,” amesema Bashe.


Share:

Waziri wa Nishati, Medard Kalemani Atoa ONYO Kwa mameneja na wakandarasi wanaotoza Wananchi Gharama ya nguzo za umeme

Waziri wa Nishati, Medard Kalemani ametoa onyo kwa mameneja na wakandarasi wanaotoza nguzo za umeme wananchi na kuwataka waachane na tabia hiyo mara moja kwakua serikali imegharimia nguzo hizo kwa asilimia 100.

Waziri Kalemani ametoa kauli hiyo bungeni leo Jumatano Novemba 6, katika kipindi cha maswali na majibu alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Halima Bulembo aliyetaka kujua serikali inazungumzia vipi kadhia ya kulipishwa nguzo za umeme ambayo wananchi wa Mkoa wa Kagera wamekuwa wakikumbana nayo

Akijibu hoja hiyo Waziri Kalemani amesema serikali haitaendeleakufumbia macho suala hilo na kwamba yeyote atakaekamatwa atachukuliwa hatua za kisheria bila kujali cheo chake.

“Yapo maeneo bado wakandarasi na mameneja wa Tanesco wanaendelea kutoza nguzo wateja, ninaomba nitoe tamko kali sana kwamba ni marufuku kutoza nguzo kwa wateja wote, awe mkandarasi, Meneja wa Tanesco au kibarua na hii ni kwasababu serikali imegharamia kwa asilimia 100,” amesema Dk. Kalemani.

Aidha amesema serikali imekuwa ikipeleka umeme katika maeneo yote hasa vijijini lakini baadhi ya taasisi zimekuwa hazilipiwi na hivyo amewataka wamiliki wa taasisi hizo kuhakikisha wanalipa kiasi cha Sh 27,000 ili taasisi zote zipelekewe umeme.


Share:

Je, Una Hofu na Usalama wa Namba Yako ya Simu?? | Tazama Hapa Jinsi ya Kujitoa au Kufuta namba yako Kwenye App ya TrueCaller

Kabla ya kuangalia namna ya kujitoa kwenye huduma hii, kwanza ningependa tuanze kwa kutoa ufafanuzi Truecaller ni nini?

TrueCaller ni app maarufu duniani inayowawezesha watumiaji wake kutambua majina ya watu au makampuni wanayotaka kuwasiliana nayo au yanayowapigia simu wao.

Kwa kifupi, mtumiaji wa TrueCaller anaweza kufahamu jina la mtu au kampuni  hata kama hajam save kwenye simu yake kabla ya kupiga au kupokea simu.

Mfumo wa data wa TrueCaller ni mfumo ambao  watumiaji wake wanasaidiana kupeana taarifa za data za watu walio kwenye simu zao.

Unapopakua programu hiyo kutoka kwenye Playstore/App Store kisha ukaingia ndani kwa kuweka email na password yako, basi utakuwa umeruhusu wahusika kuona namba za watu ulionao kwenye kifaa husika na kuhifadhi taarifa hizo  kwenye kompyuta zao za kutunza kumbukumbu (servers).

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬   

Pamoja na uzuri wa TrueCaller, yaweza kuwa imefika mahali sasa unawaza usalama wa namba yako ya simu au data zako na taarifa zako binafsi  na hivyo unatamani kujitoa au kufuta kabisa namba yako kwenye Mfumo wa TrueCaller

Leo tutakuelekeza namna ya kujitoa maana yawezekana hata kama   bado haujajiunga na app hiyo ila namba yako tayari imeunganishwa kwenye mfumo wa TrueCaller kupitia mtu mwingine mwenye number yako ya simu.

Kuna njia mbili za  kuiondoa namba yako kwenye mfumo wa TrueCaller, hii inategemea kama tayari ulijiandikisha kwenye huduma hii au haujajiandikisha lakini kumbuka kama kuna  mtu anayetumia app hii ya TrueCaller  na  ana namba yako basi  taarifa zako zimeingizwa pia kama alitoa 'access/Kibali' ya contacts list

Jinsi ya kujitoa au kutoa namba yako kutoka kwenye app ya TrueCaller

Kwa wale wenye akaunti za TrueCaller
1.Fungua app ya TrueCaller, nenda kwenye alama ya nukta tatu upande wa kushoto juu.
2.Kisha nenda Settings, kisha About, na hapo utaona chaguo la ‘Deactivate Account’ yaani futa akaunti…
3.Ata ukishafuta akaunti yako, yaani ‘deactivate account’ bado namba yako inaweza kuwa kwenye data za TrueCaller. Na hapa ndio inabidi uchukue hatua inayofanana na wale ambao hawana akaunti ya TrueCaller.
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬   

Kwa wale wasio na akaunti ya TrueCaller au wamefuta/deactivate akaunti zao

1.Hatua inayofuata ni kuondoa namba kwenye mfumo wa kompyuta (servers) za huduma ya TrueCaller.
2.Nenda kwenye tovuti ya TrueCaller huduma ya kuondoa namba (Unlist)
3,Ukifika hapa andika namba yako ya simu, chukua hatua za kuonesha ya kwamba wewe ni binadamu (captcha) na kisha bofya ‘Unlist’

==>>Kama Bado Hujaelewa <<BOFYA HAPA>> Kusoma maelezo Kwa Kina Zaidi


Share:

Katibu Mkuu TAMISEMI Ataka Sheria, Kanuni na Miongozo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2019 Zifuatwe

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhandisi Joseph Nyamhanga amewataka viongozi na wasimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika ngazi za Mikoa, Wilaya na Halmashauri kuhakikisha kuwa wanasimamia kwa karibu Kanuni, Sheria, na Miongozo mbalimbali iliyowekwa ili uchaguzi huo ufanyike katika mazingira ya amani na uwe huru na haki.

Katibu Mkuu ameyasema hayo leo Jijini Dodoma wakati akielezea hatua inayofuata baada ya zoezi la uchukuaji na urejeshwaji wa fomu za kugombea nafasi mbalimbali katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kukamilika hapo jana ambapo amesema zoezi linaloendelea kwa tarehe 5 Novemba, 2019 ni Uteuzi wa Wagombea katika nafasi za Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa na nafasi ya Wajumbe wa Halmashauri za Vijiji na Wajumbe wa Kamati za Mitaa.

Amesema kuwa kuanzia tarehe 5 hadi 6 Novemba, 2019 ni kipindi cha watu walioomba kuteuliwa kuwa wagombea au wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi ambao hawajaridhika na uteuzi uliofanywa na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi kuwasilisha pingamizi kuhusu uteuzi wa wagombea.

 “Nitoe maelekezo kwa Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi kusimamia kwa weledi zoezi la uwasilishaji wa pingamizi na kutoa uamuzi wa haki kuhusu pingamizi hizo za uteuzi wa wagombea” amesisitiza Katibu mkuu.

Mhandisi Nyamhanga ameseama kwamba baada ya Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi kupokea pingamizi na kutoa uamuzi, waombaji au wagombea ambao hawataridhika na uamuzi wa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi watakuwa na haki ya kukata rufaa kati ya tarehe 5 hadi 8 Novemba,  2019 kwenye Kamati za Rufani zilizoanzishwa katika kila Wilaya nchini.

Aidha, Kamati za Rufani zitatoa uamuzi kuhusu rufaa mbalimbali zilizowasilishwa kwake kati ya tarehe 5 na 9 Novemba, 2019.  Vilevile, mtu yeyote ambaye ameomba kuteuliwa kuwa mgombea au mgombea ambaye hajaridhika na uamuzi wa Kamati ya Rufani atakuwa na haki ya kufungua kesi katika Mahakama ya Wilaya ndani ya muda wa siku 30 baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa.

Mhandisi Nyamhanga amevikumbusha Vyama vya Siasa ambavyo vitashiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2019 kuhakikisha vinawasilisha ratiba za mikutano ya kampeni kwa Wasimamizi wa Uchaguzi tarehe 10 Novemba, 2019 kama ilivyooneshwa kwenye ratiba ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.


Share:

Mbwana Samatta Avunja Rekodi....Ni Baada ya kuifunga timu kubwa duniani ambao ni mabingwa wa Ulaya, Liverpool.

Mshambuliaji kinara wa klabu bingwa ya Ubelgiji KRC Genk na nahodha wa Tanzania, Mbwana Samatta jana usiku ametimiza ndoto yake ya kuifunga timu kubwa duniani ambao ni mabingwa wa Ulaya, Liverpool.

Goli hilo lilikuwa likisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa mpira wa miguu nchini Tanzania.

Hata hivyo, matokeo ya mwisho ya mchezo huo wa Klabu Bingwa Ulaya yalikuwa mabaya kwa Genk kwa kulazwa kwa goli 2-1.

Samatta, aliunganisha kwa kichwa mpira wa kona mpaka wavuni katika dakika ya 40 ya mchezo.

Mshambuliaji huyo ambaye ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza michuano hiyo mikubwa zaidi ya vilabu barani Ulaya tayari ameshapachika magoli mawili katika mechi nne. 


Share:

Makubaliano yafikiwa kati ya serikali na waasi wa Yemen

Serikali ya Yemen inayotambulika kimataifa na wapiganaji wanaotaka kujitenga upande wa kusini wametia saini makubaliano ya kugawana madaraka na kumaliza mapigano baina ya makundi hayo. 

Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman alitangaza kufikiwa makubaliano hayo katika televisheni ya taifa jana, akisema ilikuwa hatua muhimu kufikisha mwisho vita vya miaka minne nchini Yemen. 

Makubaliano yanayoitwa ya Riyadh , yanakamilisha mwezi mmoja wa mazungumzo ya moja kwa moja ya amani kati ya serikali hiyo inayotambuliwa kimataifa, ikiongozwa na rais Abed Rabbo Mansour Hadi na wapiganaji wanaotaka kujitenga wakiungwa mkono na Umoja wa Falme za Kiarabu wanofahamika kama baraza la mpito la kusini mwa Yemen STC. 

Pande hizo mbili zimekuwa zikipigana licha ya kuungana dhidi ya majeshi ya wahouthi yanayoungwa mkono na Iran, ambayo yanashikilia mji mkuu Sanaa, pamoja na miji mingine mingi nchini Yemen.

-DW


Share:

TAKUKURU Mkoa Wa Dodoma Yamnasa Afisa Mtendaji Kwa Kosa La Kushawishi Kupokea Rushwa Kutoka Kwa Mfugaji

Na.Faustine  Gimu Galafoni,Dodoma.
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini [TAKUKURU]  mkoa wa Dodoma inamshikilia  Bw.David Daud Tengeneza mwenye umri wa  miaka 50 ambaye ni afisa mtendaji katika kijiji cha Mapanga kata ya Itiso wilaya ya Chamwino  kwa kosa la kushawishi na kujaribu kupokea rushwa   kinyume na kifungu cha sheria Na.15[1]a cha sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa  Sura ya 329 marejeo ya mwaka 2018.
 
Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini Kwake jijini Dodoma  Nov.5,2019,Mkuu wa TAKUKURU mkoani hapa Bw.Sosthenes Kibwengo amesemaTAKUKURU imekuwa ikipokea tuhuma kadhaa juu ya afisa mtendaji huyo kujihusisha na vitendo vya rushwa .
 
“Mtendaji huyu amekuwa na tuhuma mbalimbali za rushwa ambapo TAKUKURU Mkoa wa Dodoma imekuwa ikifuatilia kwa kina na safari hii arobaini yake imewadia”amesema.
 
Bw.Kibwengo amefafanua kuwa “,baada ya kupokea taarifa mbili tofauti dhidi ya mtuhumiwa  wiki iliyopita tuliamua kufuatilia  mojawapo ambapo uchunguzi ulithibitisha kwamba ameomba rushwa ya shilingi laki tatu[300,000/=]kutoka kwa mtoa taarifa wetu ambaye ni mfugaji.
 
Tarehe 30 Oktoba ,2019 afisa wetu aliambatana na mtoa taarifa  hadi ofisini kwamtuhumiwa ambapo alielekeza apelekewe fedha hizo ndipo ampatie barua  ya kumruhusu  kuingiza kijijini Mapanga  ng’ombe arobaini na nane[48] aliowatoa kijiji jirani cha Segala  la sivyo angemchukulia hatua za kisheria  kwa kutokuwa na kibali.”
 
Mkuu huyo wa TAKUKURU ameendelea kusema kuwa,kutokana na uzoefu wa Mtuhumiwa katika vitendo vya rushwa ,mtuhumiwa alipomwona mtoa taarifa akiwa na mtu mwingine alianza kumhoji huku akisisitiza kuwa yeye ni mzoefu  na mara kadhaa amekoswa na TAKUKURU,hivyo kumtaka akaweke fedha hizo nje ya chooni lakini hakuacha fedha hiyo ya Rushwa na walipoondoka ,mtuhumiwa akaenda chooni kuangalia  na akagundua kuwa hongo yake haipo.
 
Mtuhumiwa aliamua kumfuata mtoa taarifa na kumtaka arudi na akahojiiweje hongo haipo  naye akamweleza hawezi kuacha fedha  bila kupewa barua,ndipo akaelekezwa aiweke chini ya jiwe  lililo chini ya mti  nje ya Ofisi ya mtuhumiwa na aingie ndani kuandikiwa barua.
 
Bw.Kibwengo ameendelea kusema,baada ya kuweka fedha hiyo chini ya jiwe,mtoa taarifa  aliingia ndani ya ofisi lakini mtuhumiwa hakumwandikia barua kwa kisingizio  cha kuisahau mihuri nyumbani na TAKUKURU imemkamata na atafikishwa mahakamani.
 
Hivyo ,Bw.Kibwengo amewakumbusha wananchi wote kuwa ni kosa la jinai kushawishi  na kujaribu kuchukua rushwa  na wananchi wanapokutana na hali hizo watoe taarifa mapema kwa TAKUKURU.
 
Pia,Bw.Kibwengo amewakumbusha watumishi wa Umma kwamba mkono wa sheria ni Mrefu  hivyo ukijihusisha na uhalifu ipo siku ya arobaini itafika na fedheha itakuja ni vyema kuzingatia Maadili ya kazi kwani Rushwa hailipi.


Share:

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo Yabainisha Mkakati Wa Kudhibiti Maradhi Yanayoikumba Mimea Ya Mipapai Nchini

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imefanya utafiti na kugundua kuwa ugonjwa wa Ubwili unga ndio unaoathiri mipapai kwa kiwango kikubwa.

Baada ya kugundulika ugonjwa huo, Wizara ya kilimo imechukua hatua za kuudhibiti kwa kutumia viuatilifu vyenye viambata vya croripynfos (udhibiti wa kwenye udongo), Profenophos na Dichlorovosch (udhibiti kwenye majani).

Aidha, njia nyingine ya uthibiti ni kwa kutumia mbinu bora za kilimo (Cultural Control) kwa kupanda miche wakati wa kiangazi ili mimea isishambuliwe ikiwa michanga, kupalilia shamba kwa wakati na kug’olea miche iliyoathirika na utumiaji wa wadudu marafiki (Biological Control).

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba ameyasema hayo jana tarehe 5 Novemba 2019  bungeni Jijini Dodoma Wakati akijibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum Zainabu Mussa Bakari aliyetaka kufahamu serikali imechukua hatua gani kudhibiti maradhi katika mimea ya mipapai nchini ambayo yanahatarisha kupotea kwa mimea hiyo.

Amesema kuwa Serikali inaendelea kutoa elimu kwa wakulima kuhusu kufuata kanuni bora za kilimo ili kuepuka magonjwa mbalimbali yanayoweza kuathiri mimea ukiwemo mpapai.

Serikali kupitia Kituo cha Utafiti cha TARI-Horti TENGERU imeendelea kufanya utafiti magonjwa na wadudu wanaoathiri mazao ya bustani ikiwemo mipapai. Utafiti huo umegundua kuwa ugonjwa wa Ubwili unga unaoathiri mipapai unaosababishwa na vimelea vya kuvu (fungus) vijulikanavyo kitaalam kama Oidium caricae papaya.

Ameongeza kuwa Mipapai haiwezi kupotea nchini kwa kuwa tayari njia za kudhibiti      magonjwa na wadudu wanaoshambulia mimea hiyo zipo.

kadhalika, Wizara itaendelea kuwaelimisha wakulima na wadau mbalimbali juu ya udhibiti wa ugonjwa na wadudu wanashambulia mimea na mazao ikiwemo mipapai ili kuongeza uzaliahaji na tija.

 MWISHO


Share:

HATUA ILIPOFIKIA MIRADI YA MELI JIJINI MWANZA

Tazama Video hapa chini
Share:

Job Opportunity at ActionAid, TOR- Inspirator Kilwa

TOR- Inspirator Kilwa   ActionAid is an international anti-poverty agency working in over 47 countries, taking sides with poor people to end poverty and injustice together. Whilst all applicants will be assessed strictly on their individual merits, qualified women are especially encouraged to apply. ActionAid started its operations in Tanzania in 1998. ActionAid Tanzania (AATZ) envisions seeing Tanzania without… Read More »

The post Job Opportunity at ActionAid, TOR- Inspirator Kilwa appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at ActionAid, TOR- Inspirator Unguja

TOR- Inspirator Unguja  ActionAid is an international anti-poverty agency working in over 47 countries, taking sides with poor people to end poverty and injustice together. Whilst all applicants will be assessed strictly on their individual merits, qualified women are especially encouraged to apply. ActionAid started its operations in Tanzania in 1998. ActionAid Tanzania (AATZ) envisions seeing Tanzania without… Read More »

The post Job Opportunity at ActionAid, TOR- Inspirator Unguja appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

2 Jobs Opportunities at INADES-Formation Tanzania

Job Title: Project Officer Agroforestry Job Reports to: Project Coordinator Duty Station: Kondoa Town, with project activities in villages of Kondoa and Chemba Districts Education: Bachelor’s degree in agroforestry or related fields Experience: 3 years’ experience in mobilizing rural communities in field work with an ability to work under pressure, tight deadlines with less supervision. Fluency in Swahili… Read More »

The post 2 Jobs Opportunities at INADES-Formation Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MKUTANO WA 18 WA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA NCHI ZA AFRIKA 29 NA NCHI 5 ZA NORDIC KUFANYIKA DAR ES SALAAM


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano November 6























Share:

Tuesday, 5 November 2019

Procurement Officer – Goods & Services Job Opportunity at IRC Dar es Salaam

Procurement Officer – Goods & Services Job Opportunity at IRC Dar es Salaam Job Title: Procurement Officer – Goods & Services Requisition ID: req7060 Sector: Supply Chain Employment Category: Fixed Term Employment Type: Full-Time Open to Expatriates: No Location: Dar es Salaam, Tanzania Job Description The International Rescue Committee (IRC) is an International Non-Governmental Organization working in 40… Read More »

The post Procurement Officer – Goods & Services Job Opportunity at IRC Dar es Salaam appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger