Tuesday, 6 December 2016

Kipindupindu charejea kwa kasi, chatikisa mikoa 6

Share:

Mbunge wa Ukonga apinga amri iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam


Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) amepinga amri iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ya wafanyabiashara kufunga maduka yao kila siku ya Jumamosi kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa nne ili wafanye usafi.

Amesema amri hiyo ni batili na haitekelezeki kwa sababu inarudisha nyuma uchumi wa wananchi hususani wafanyabiashara ndogondogo ambao wanategemea kipato chao cha siku kuendesha maisha yao.

Akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Kivule mwishoni mwa wiki, Waitara alisema yeye hapingani na watu kufanya usafi katika maeneo yao, lakini amri ya kufunga maduka kila Jumamosi inaathiri uchumi wa wananchi hivyo ni batili na haipaswi kuendelea kuwapo.

Siku chache baada ya kuteuliwa kuongoza Mkoa wa Dar es Salaam, Makonda alipiga marufuku kufungua maduka na biashara zingine kabla ya saa nne asubuhi ili muda huo utumike kufanya usafi na anayekaidi agizo hilo hutozwa faini isiyopungua Sh 50,000.

Mbunge huyo wa Ukonga alisema uchumi wa watu masikini hususani wa mjini unategemea kile wanachokizalisha kila siku, hivyo amri ya kufunga biashara kila wiki ni kurudisha nyuma juhudi za wananchi kujiletea maendeleo yao.

Katika mkutano huo aliwaambia wananchi hao kujiwekea utaratibu kuhakikisha maeneo yao yanakuwa safi wakati wote na kila Jumamosi wafungue biashara zao asubuhi kama kawaida na wasibughudhiwe na mtu yeyote.

“Mimi naunga mkono utaratibu wa kufanya usafi kila mwezi uliotangazwa na Rais Dk. John Magufuli ambao upo kwa mujibu wa taratibu, lakini huu wa kila Jumamosi mimi sina mwongozo nao na hizo faini za kila wiki sizitambui na ni batili.

“Ninachotaka kila mtu afanye usafi kwenye eneo lake, hizi faini zinatozwa bila utaratibu hata kama eneo la mtu ni safi sitaki kuzisikia, wananchi hawa si wanyama, waelimishwe waachwe wajiwekee utaraibu wao.

“Hivi mama, baba ntilie anayepika  maandazi, vitumbua, chapati afunge biashara tangu asubuhi mpaka saa nne halafu hiyo chai itanywewa na nani, huyu mtu unamwambia afunge biashara ili akaibe mtaani?” alihoji mbunge huyo na kuongeza:

“Watendaji lazima muwasikilize watu, nasikia kinachofanyika ni mwendo wa kuviziana, waacheni watu wafanye kazi, hapa ni kazi tu sio faini tu” alisema Waitara.

Katika hatua nyingine, Waitara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kivule alivunja kikundi cha ulinzi kilichokuwa katika ofisi hiyo kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa pamoja na kuwanyanaysa wananchi.

Badala yake, alisema uitishwe mkutano wa hadhara watu wote wanaohitaji kazi hiyo walete maombi katika ofisi hiyo na baadaye wajadiliwe na wananchi katika mkutano wa hadhara ili kuepuka kuwapa kazi watu wasiokuwa waaminifu katika jamii.
Share:

Fundi Pancha Atupwa Jela Miaka 30 Kwa Kukutwa na Misokoto 601 ya Bangi

Share:

TANZIA: Aliyekuwa mbunge wa Rufiji na daktari bingwa wa moyo, Prof. Mtulia afariki dunia

Share:

PICHA: Ajali ya Lori na Hiace Yaua Watu 9 na Kujeruhi 18

Share:

Monday, 5 December 2016

Bilioni 2.7 Zayeyuka Mradi Wa Ujenzi Hospitali Ya Wilaya Ya Monduli,Waziri Mkuu Aagiza Ufanyike Uchunguzi

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Arus
Share:

Waziri Mkuu Majaliwa Aitembelea Familia Ya Marehemu Sokoine Monduli Juu

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na  Napono Sokoine (wapili kulia) na  Nekiteto Sokoine (kulia) ambao ni  wajane wa aliyekuwa Waziri Mkuu, Marehemu Edward Sokoine wakati aipokwenda nyumbani kwa marehemu, Monduli Juu kuisalimia familia akiwa katika ziara ya wilaya  ya Monduli Desemba 4, 2016.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka shada la maua kwenye kaburi la aliekuwa Waziri Mkuu, Edward Sokoine wakati alipokwenda nyumbani kwa marehemu, Monduli Juu akiwa katika ziara ya wilaya ya Monduli
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipokwenda nyumbani kwa  aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Sokoine, Monduli Juu kuisalimia familia akiwa aktika ziara ya wilaya  ya Monduli Desemba 4, 20, 16.  Kushoto kwake  wajane wa marehemu, Napono Sokoine (wpili kulia) na kulia ni  Nekiteto Sokoine . Kulia kwake  ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipokwenda nyumbani kwa  aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Sokoine, Monduli Juu kuisalimia familia akiwa aktika ziara ya wilaya  ya Monduli Desemba 4, 20, 16.  Kushoto kwake  wajane wa marehemu, Napono Sokoine (wpili kulia) na kulia ni  Nekiteto Sokoine . Kulia kwake  ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.(Picha na Ofisi ya Wziri Mkuu)
Share:

Waziri Mkuu Majaliwa aagiza uchunguzi ufanyike kwanini mbolea ya minjingu hazitumiki nchini

Share:

Mchezaji wa Mbao FC afariki baada ya kugongana na mchezaji wa Mwadui FC

Share:

Rais Shein aagiza Mitaala ya ujasiriamali Shule za sekondari ili Kuwasaidia Vijana Kujiajiri

Share:

Lowassa: Fidel Castro ni shujaa wangu wa dunia


Share:

Mzee wa Upako: Tajeni nilikunywa pombe gani na Katika Baa Gani

Share:

Yusuf Manji Atii Sheria Bila Shuruti,Alipewa saa 24 kuondoka kwenye jengo la PSPF Plaza (Quality Plaza)

Mfanyabiashara Yusuph Manji jana alitii sheria bila shuruti kwa kuhama kwenye jengo la Quality Plaza akitekeleza amri ya Mahakama ya kumtaka kurejesha jengo hilo ambalo ni mali ya Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF). 
Mbali na kutekeleza amri ya kuhama baada ya kupewa notisi ya saa 24 iliyomalizika juzi, pia anatakiwa kulipa malimbikizo ya deni la pango la Dola za Marekani 6.1 milioni (zaidi ya Sh13 bilioni), ambazo kama asipozilipa mali zake zitakamatwa. 
Hatua hiyo imekuja baada ya Mahakama Kitengo cha Ardhi kutoa hukumu ya kumtaka Manji kuondoka kwenye jengo hilo pamoja na kuilipa deni la pango. 
Alipotakiwa kuzungumzia suala hilo, Manji ambaye ni Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga hakupatikana kupitia simu yake ya mkononi. 
Viongozi wa kampuni za Manji waliokuwa wakisimamia uondoaji wa vifaa uliomalizika jana asubuhi, walikataa kuzungumza na waandishi wa habari waliofika kufuatilia tukio hilo. 
Tangu juzi chini ya usimamizi wa kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart, Manji na kampuni zake walikuwa wanaondoa vifaa mbalimbali vilivyopo kwenye jengo hilo na kuhitimisha shughuli hiyo jana.

Meneja Uendeshaji wa Yono Auction Mart, Atukuzwe Mhugo alisema kampuni ambazo walikuwa wakizisimamia kuondoa vifaa ni Quality Group Co Ltd, Gaming Managemeti Ltd, Q Consult Ltd na Quality Logistics Co Ltd.

Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo ya Yono, Scholastica Kenyela alisema tayari wameshaziondoa kampuni za Manji kwenye jengo hilo. 
Kenyela alisema mteja wao ambaye ni PSPF alichukua uamuzi huo baada ya Manji kushindwa kulipa kodi ya pango ya zaidi ya Sh13 bilioni. 
“Sisi tumetimiza wajibu wetu, ukienda pale utaona tayari tumeshafanya kazi yetu kwa sababu alipewa notisi ya saa 24 awe ameondoka,” alisema.
Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi alisema masuala yote yanayohusiana na jengo hilo kwa sasa yako chini ya Yono Auction Mart. “Sipo Dar es Salaam na sitazung- umzia chochote kuhusu jengo hilo wenye mamlaka ni Yono naomba uwatafute wao,” alisema.
Share:

Waziri Mkuu afanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Mount Meru,Akerwa na Msongamano Katika Wodi ya Wazazi

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa jana alifanya ziara ya kushtukiza katika hospitali ya Mkoa ya Mount Meru ambako kulikuwa na tuhuma za kuibwa watoto, lakini alishuhudia wazazi watatu wakilala kitanda kimoja. 

Ziara hiyo ilitokana na taarifa alizolalamikiwa na wananchi juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, kwamba hospitali hiyo ina matukio ya wizi wa watoto wachanga. 

Hata hivyo, jana baada ya kufika katika hospitali hiyo, Majaliwa alishuhudia msongamano katika wodi ya wazazi na kuagiza kuboreshwa hospitali za pembezoni. 

Majaliwa aliagiza uongozi wa hospitali hiyo kuhakikisha wanaondoa changamoto za ongezeko la wagonjwa na kuboresha huduma katika hospitali hiyo. 
Akizungumzia sakata ya kupotea kwa watoto katika hospitali ya mkoa alivitaka vyombo husika kuendelea na uchunguzi kwa kuwa suala hilo tayari lipo mikononi mwa vyombo vya dola. 

Wiki mbili zilizopita mzazi, Walda Mussa alisema kuwa alijifungua mtoto katika hospitali hiyo lakini hadi alipotoka hakumpata.
“Nilikuja hapa hospitali Oktoba 4 na Oktoba 7 nikajifungua kwa upasuaji wakamchukua mtoto na kumpeleka chumba cha joto, akaja mume wangu akaenda kumuona mtoto mzima, siku ya pili alienda kumuona mtoto pia akiwa mzima lakini siku ya tatu, tulipokwenda wote mimi na mume wangu tuliambiwa mtoto alifariki na hatujawahi kuona mwili wake,” alisema mwanamke huyo hivi karibuni. 
Mganga Mkuu mfadhiwi wa hospitali ya Mkoa Mount Meru, Dk Jackline Urio alipotakiwa kuelezea sakata hilo, alisema kuwa mtoto huyo baada ya kuzaliwa alifariki dunia na baadaye mwili ulipelekwa chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali hiyo. 
Share:

MWANAFUNZI WA DARASA LA 5 AJINYONGA HADI KUFA

Share:

Magazeti ya Leo Jumatatu Tarehe 5.12.2016

Share:

KURASA ZA NDANI ZA MAGAZETI YA LEO JUMATATU DEC 05 2016

TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE HABARI ZA MICHEZO LEO..


TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE KATUNI ZA LEO..


KUMI BORA ZA MASWAYETU BLOG KURASA ZA NDANI MAGAZETINI LEO


1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger