Saturday, 26 November 2016

Muuguzi anayedaiwa kumwambia mama wa mgonjwa ‘ataisoma namba kumchagua Magufuli’ atambuliwa

Mbeya. Muuguzi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya anayedaiwa kumkamshifu Junes Elias, mkazi wa Mbozi mkoani Songwe na Rais John Magufuli ametambuliwa.

Mganga mkuu wa hospitali hiyo, Dk Gloria Mbwille alisema muuguzi huyo ametambuliwa na kwamba tume imeundwa kuchunguza tuhuma zinazomkabili.

Hata hivyo, alikataa kuzungumzia zaidi kuhusu muuguzi huyo wala kumtaja jina akisema taarifa zaidi zitatolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla baada ya tume kukamilisha uchunguzi huo. Juzi mchana, Junes alimueleza Makalla kwamba alifika hospitalini hapo Novemba 22 asubuhi akitokea wilayani Mbozi.

Alisema baada alifuata taratibu za kufungua kadi kwa gharama ya Sh5,000 kwa ajili ya kutaka matibabu ya mtoto wake, Joyce Asifiwe (9), lakini alikashfiwa kwenye dirisha la dawa akiambiwa ataisoma namba kwa kumchagua Rais Magufuli.

Alisema baada ya kumuona daktari aliandikiwa dawa za kwenda kuchukua kwenye dirisha ambako ndiko alikotolewa maneno ya kashfa.

“Kwenye dirisha hilo nilimkuta muuguzi mmoja ambaye aliniambia kwamba dawa zote zinauzwa. Hapa hakuna dawa za bure, si mlimchagua Magufuli, sasa mtaisoma namba,’’ alisema akidai kumnukuu aliyemtaja kuwa ni muuguzi.


Baada ya kumsikiliza malalamiko hayo, Makalla aliagiza mganga mkuu aitwe, lakini ilielezwa alikuwa safarini, hivyo kaimu wake, Dk Ismail Macha alifika.

Makalla alimueleza Dk Macha kwa kifupi yaliyojiri kutoka kwa mlalamikaji huyo na kumtaka waongozane hadi hospitalini na kuwaita wauguzi waliokuwa zamu Novemba 22 dirisha la dawa ili amtambue mhusika na achukuliwe hatua jambo ambalo limefanyika.
Share:

Rais wa Zamani wa Cuba, Fidel Castro Afariki Dunia

CUBA: Rais wa zamani wa Cuba, na kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha nchini humo, Fidel Alejandro Castro Ruz amefariki dunia leo akiwa na umri wa miaka 90.
Share:

Magazeti ya Leo Jumamosi november tarehe 26.11.2016

Share:

Friday, 25 November 2016

official VIDEO | MwanaFA Ft. Vanessa Mdee – Dume Suruali | Watch/Download


dume
Share:

Rais Magufuli amualika Rais wa Zambia kwa ziara ya siku 3

Share:

Ripoti ya uchunguzi wa mali za BAKWATA yakabidhiwa

Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zuber  jana amekabidhiwa ripoti ya awali iliyoandaliwa na tume ambayo ameiunda  kwa ajili ya kufanya uchunguzi  na kuzibainisha  mali zote za  Baraza kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).

Akizungumza wakati wa kumkabidhi ripoti hiyo, Mwenyekiti wa tume hiyo Sheikh Abubakari Khalid Hajj alisema kuwa  ripoti hiyo imefanyika kwa muda wa miezi mitatu licha ya kukumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ufinyu wa muda.

Aidha aliwambia wanahabari kuwa uchunguzi huo umehusisha ufuatiliaji wa mali za Bakwata katika Mkoa wa Dar es salaam pekee,ikiwemo majengo,viwanja, pamoja na kupitia mikataba mbalimbali ili  kujiridhisha kama imefuata taratibu za kisheria.

Akizungumza mbele ya wanahabari mara baadi ya kupokea ripoti hiyo Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zuber alisema kuwa ataipitia ripoti hiyo  ili kujua yale yaliyobainishwa na tume yake, na kuahidi kuyafanyia kazi mapema iwezekanavyo.

Hata hivyo Mufti huyo ameiongezea muda wa miezi mitatu tume hiyo ambayo ina jumla ya  wajumbe wanane kwa ajili ya kukamilisha kuandaa ripoti ya mkoa wa Dar es salaam kabla ya kuhamia mikoa mingine kwani zoezi hilo litafanyika nchi nzima.
Share:

Magazeti ya Leo Ijumaa Ya Novemba 25 2016

Share:

Thursday, 24 November 2016

RC Makonda Aamuru Mwenyekiti wa Mtuu Akamtwe na Kuwekwa Rumande Hadi Upelelezi Utapokamilika

Share:

Wataalam wa afya kuanza kusajiliwa na kupewa leseni

Wataalamu mbalimbali wa sekta ya afya, sasa wataanza kusajiliwa na kupewa leseni zitakazowatambulisha na zitakuwa na masharti maalumu.

Hayo yamesema na Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Muhammad Kambi  jana Jumatano  jijini Dar es salaam, wakati akifungua mkutano wa mwaka wa Chama cha Wafiziotherapia (APTA).

Alisema serikali imeanza mchakato wa kuipitia upya Sheria ya Madaktari wa Tanganyika, ambayo itaongezwa sharti hilo pamoja na kuundwa kwa bodi maalumu itakayosimamia maadili ya watumishi hao.

“Lakini hivi sasa kuna taaluma nyingi ndani ya hii fani, kwa mfano ninyi wataalamu wa fiziotherapia. Mpo lakini sheria haiwatambui, kwa maana hiyo inakuwa vigumu hata kuwafuatilia. Ndiyo msingi wa kuipitia upya sheria hii,” alisema.

“Katika sheria mpya itakayoboreshwa, kila mtumishi atatakiwa kukata leseni. Kila mtumishi atatakiwa kujiendeleza kielimu, kuongeza ujuzi ili aendane na wakati uliopo kwa sababu mambo yanabadilika, kile ulichosoma jana unahitaji kujifunza zaidi,” alisema.

Aidha Kambi alisema tayari maboresho ya sheria hiyo yameshawasilishwa katika Kamati ya Baraza la Mawaziri ya Katiba na Sheria na imeshapitiwa.
Share:

Mwanafunzi Apigwa Risasi na Polisi Dar,Askari Wawili Watiwa Mbaroni

Share:

Official VIDEO ,Download Darassa Ft. Ben Pol – Muziki

vlcsnap-2016-11-23-16h23m16s238
Share:

New AUDIO | Darassa Ft. Ben Pol – Muziki | Download


15056726_1788955811344767_5399682663202160640_n
Share:

BONGO MOVIE SHINYANGA NA SWAHILI ARTS WAMEKULETEA TAMTHILIA YA VAISI VESA -TAZAMA HAPA SEHEMU YA KWANZA 'WIVU'



Tamthilia ya Vaisi Vesa- sehemu ya kwanza Wivu,itazame chini ya maelezo yote hapo chini

Amani Masuka(kushoto) na Ibrahim Songoro(kulia) wakiwa katika ofisi ya Bongo Movie Shinyanga Jumatano,Novemba 23,2016 wakiendelea na kazi 

Amani Masuka(kushoto) na Ibrahim Songoro(kulia) wakiwa katika ofisi ya Bongo Movie Shinyanga Jumatano,Novemba 23,2016
Kundi la sanaa ya uigizaji la Swahili Arts la jijini Arusha na Bongo Movie Shinyanga wameamua kuja upya kwa kuunganisha asasi zao na kufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha wanaiwakilisha vyema Shinyanga na kuitambulisha tasnia ya filamu mkoa wa Shinyanga. 
Wakizungumza na Malunde1 blog,wamesema sasa wameamua kuja kwa ujio mpya ambao utakuwa bandika bandua kwa kazi zenye ubora na mafunzo na wameanza kwa tamthiliya ya Vaisa Vesa. 
Hatua hiyo imekuja baada ya mwongozaji wa filamu nchini Amani Masuka anayeongoza kundi la sanaa ya uigizaji la Swahili Arts la jijini Arusha na mmliki wa Eden Media Creation,kumaliza tofauti zilizojitokeza mwanzoni mwa mwaka 2015 na Bongo Movie Shinyanga inayosimamiwa na Ibrahim Songoro ambaye pia anamiliki Songoro Media Production. 
Pamoja na mikakati kibao waliyonayo itakayoanza mwezi Desemba 05 mwaka huu,magwiji hao wa sanaa ya uigizaji na uongozaji wa filamu wameahidi kuja na mkakati utakaotengeneza wasanii wapya na kujenga misingi imara ya kiwanda cha filamu mkoa wa Shinyanga. 
Tayari wameanza na tamthilia fupi inayojulikana kwa jina la 'Vaisi Vesa' itakayokuwa inarushwa kwa njia ya mitandao ya kijamii kama vile youtube,instagram,whatsapp n.k. 
Wahusika wakuu katika tamthilia hiyo ni Ibrahim Songoro na Miss Grace,mwongozaji ni Masuka A.J na mpiga picha ni David Skerah. 
Mwandishi na mwongozaji wa tamthilia ya Vaisi Vesa,Amani Masuka amesema filamu hiyo imejaa visa mbalimbali vinavyotokea katika maisha ya binadamu vinavyotokana na watu wawili kupishana kauli. 
“Tamthilia ya Vaisi Vesa itakuwa inatoa visa vifupi ambavyo wahusika huwa wanatofautiana kauli ‘kauli tata’,itakuwa inahusisha watu wawili”,anaeleza Masuka. 
Amesema sehemu ya kwanza ya tamthiliya hii inaitwa “Wivu”,ambapo utata umeibuka kutokana na kauli ya “Ugonjwa usiokuwa na tiba”,ambapo mhusika mkuu Ibrahim Songoro anatafsiri ugonjwa usio na tiba kuwa ni Ukimwi ilhali binti aliyekuwa anamshawishi awe mpenzi wake akimaanisha ugonjwa usio na tiba kuwa ni wivu. 
“Hapo tunaona unafiki wa Songoro anayewakilisha wanaume walaghai akibadilika ghafla na kumshtumu binti huyo kuwa ni muuaji aliyekusudia kumwambukiza virusi vya Ukimwi”,anaeleza Masuka. 
“Binti anajitahidi kumwelewesha Songoro kuwa alimaanisha wivu,ndipo Songoro anarudi kinafiki na kuanza kujichekesha,hapa tunapata ujumbe kuwa siyo kila neno unaloambiwa unatakiwa kuliamini(wanawake),lakini pia kabla ya kuchukua maamuzi unapaswa kufikiria sana kabla ya kutoa uamuzi ulio sahihi (wanaume)”,ameongeza Masuka.
Akizungumzia tamthilia hiyo, mwenyekiti wa Bongo Movie Shinyanga Ibrahim Songoro “Songoro Gaddafi” amesema tamthiliya ya Vaisi Vesa imelenga kuielimisha,kuiburudisha na kuikosoa jamii katika masuala mbalimbali.
Kwa taarifa zaidi kuhusu tamthilia ya Vaisi Vesa na mambo mengine ya sanaa ya uigizaji wasiliana na Ibrahim Songoro kwa simu namba 0767831036 na Amani Masuka simu namba 0767856192.
Tumia dakika zako chache kutazama Tamthilia ya Vaisi Vesa hapa chini katika sehemu yake ya kwanza inayoitwa “Wivu”.

Share:

HIZI HAPA KURASA ZA NDANI MAGAZETI YA LEO ALHAMISI NOV 24 2016


X

1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
Share:

Magazeti ya Leo Alhamisi tarehe 24.11.2016


Share:

Wednesday, 23 November 2016

TAARIFA KWA UMMA: KUONGEZWA KWA MUDA WA KUFANYA MAOMBI YA UHAMISHO KATIKA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) CHA UALIMU ELIMU YA MSINGI NA AWALI NA STASHAHADA (DIPLOMA) YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017


 
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
TAARIFA KWA UMMA

KUONGEZWA KWA MUDA WA KUFANYA MAOMBI YA UHAMISHO KATIKA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) CHA UALIMU ELIMU YA MSINGI NA AWALI NA STASHAHADA (DIPLOMA) YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017
Share:

FINAL LIST OF GRADUANTS SOKOINE UNIVERSITY OF AGRICULTURE 2015/2016

Taarifa ya Sherehe za Mahafali ya 32 ya Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo.

Uongozi  wa Chuo Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo unayo furaha kuwafahamisha wahitimu wote, wanajumuiya wote wa Chuo na umma kwa ujumla, kuwa sherehe ya Mahafali ya 32 ya Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo, itafanyika Ijumaa tarehe 25 Novemba, 2016  katika  Kampasi ya Solomon Mahlangu “Nelson Mandela Freedom Square” Mazimbu, kuanzia saa 4:00 asubuhi.
Sherehe hiyo itatanguliwa na sherehe ya utoaji zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri sana katika masomo yao “Prize awarding Ceremony” hapo alhamisi tarehe 24 Novemba, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa baraza la Chuo yaani “Council Chamber” uliopo kampasi kuu, kuanzia saa 2:30 hadi saa 4:30 asubuhi.
Aidha, mkutano wa majalisi ya wanataaluma wa SUA yaani “Annual general meeting of SUA convocation” utafanyika siku hiyo ya Alhamisi tarehe 24 Novemba, 2016 “Multipurpose hall” kampasi kuu, kuanzia saa 5:00 asubuhi hadi saa 7:00 mchana.
Wahitimu ˝Graduands˝ wanakumbushwa kushiriki katika mazoezi ˝Rehearsal˝ yatakayofanyika 25 Novemba, 2016 kuanzia saa 2.00 hadi saa 3.00 asubuhi, “Nelson Mandela Freedom Square”, kampasi ya solomon mahlangu, mazimbu.
Wote Mnakaribishwa.
Imetolewa Na:
Kitengo Cha Mawasiliano Na Masoko, SUA

>>KUONA MAJINA YA WAHITIMU BONYEZA HAPA<<
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger