Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi amevutiwa na Kijiji cha Mazingira katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Dkt. Muyungi amesema kilichomvutia zaidi ni kuona namna ambavyo vijana wabunifu wamepewa nafasi ya kuonesha ujuzi wao katika kutumia fursa zinazopatikana kwenye Mazingira kupitia kampeni ya Taka ni Fursa.
Dkt. Muyungi amesema kuna haja ya kuwawezesha vijana wenye mitaji midogo ili waweze kufanya mambo makubwa kupitia ubunifu wao kwenye kutumia fursa mbalimbali za urejelezaji na uchakataji taka ili kujipatia kipato na kusafisha Mazingira.
Dkt. Muyungi aliambatana na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi alipotembelea Kijiji cha Mazingira mara baada ya kushiriki hafla ya ufunguzi waaonesho hayo Julai 3,2026.

0 comments:
Post a Comment