Wednesday 31 January 2024

WANANCHI WAFUNGA BARBARA YA MWANZAA - SHINYANGA KUKITHIRI MATUKIO YA AJALI UGWETO , WATU WAWILI WAMEGONGWA LEO

...
Wakazi wa kata ya Bugweto manispaa ya Shinyanga wamelazimika kufunga barabara kuu ya Shinyanga - Mwanza baada ya leo watu wawili kugongwa na gari na kusababisha kifo cha mtu mmoja na mwingine kujeruhiwa wakidai ajali nyingi zinazotokea kwenye barabara hiyo zikisababishwa na mwendokasi unaosababishwa na baadhi ya madereva wa magari.

Baadhi ya wananchi wamedai kuwa ukosefu wa kizuia mwendo (matuta) kwenye barabara hiyo na baadhi ya madereva kutofuata sheria za usalama barabarani  imekuwa chanzo cha kusababisha vifo vitokanavyo na ajali.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga ACP Janeth Magomi amefika eneo la tukio na kuzungumza na wananchi hao ambapo amesema wataendelea kuimarisha doria za usalama barabarani katika eneo huku katibu tawala wilaya ya Shinyanga Said Kitinga amefika na kuchukuwa hatua kwa kuzielekeza mamlaka husika.

Msafara wa magari yakiwa yamezuiwa.









Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger