Sunday 28 January 2024

MANYARA WASHEREKEA KUMBUKIZI YA KUZALIWA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN

...

 Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga ameongoza zoezi la upandaji wa miti lililoendana na ukataji wa keki kwa ajili kusherekea miaka 64 ya kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. 

Akiongoza zoezi hilo la upandaji na kukata keki lililofanyika Januari 27, 2024 katika Shule ya Sekondari ya Katesh - Hanang, Mhe. Sendiga amesema Miti zaidi ya 3,000 imepandwa katika maeneo yaliyoathiriwa na maporomoko ya tope, mawe na magogo ikiwa ni njia mojawapo ya kurejesha uoto wa asili uliopotea kufuatia uharibifu mkubwa wa mazingira uliosababishwa na mafuriko yaliyotokea mwishoni mwaka mwaka jana.

Zoezi hilo lilihudhuriwa na Viongozi mbali mbali wakiwemo Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye, Wakuu wa Wilaya wote wa Mkoa wa Manyara, wananchi pamoja na watoto walioadhirika katika maporomoko hayo.

Mkoa wa Manyara umejipanga kupanda miti milioni 10 kwa mwaka 2024.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger