Friday 19 January 2024

TANESCO DODOMA YATOA SEMINA KWA MADIWANI HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA

...

Madiwani wa kata zote 41 za jijini Dodoma wakifatilia Mkutano ulioandaliwa na Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA

SHIRIKA la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma limetoa semina kwa madiwani wa kata zote 41 za jiji la Dodoma lengo likiwa ni kueleza mikakati ya shirika hilo pamoja na miradi inayotekelezwa katika mkoa wa Dodoma.

Akitoa elimu leo Januari 18, 2024 jijini Dodoma, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Dodoma Mhandisi Donasiano Shamba amesema kikao hicho kimejumuisha Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa halmashauri ya jiji la Dodoma.

“Kikao hiki kimehusisha madiwani kutoka kata zote 41 za jiji la Dodoma pamoja na Polisi kata lengo ni kueleza mikakati yetu lakini pia kueleza changamoto zinazotukabili sisi kama shirika hasa suala la uharibifu wa miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme”amesema Mhandisi Shamba

Aidha Mhandisi Shamba amesema kwa kuwashirikisha madiwani hao kwenye kikao hicho watakuwa wamewafikia watu zaidi ya 700,000 wa halmashauri ya jiji la Dodoma.

Mhandisi Shamba ameeleza kuwa Dodoma hakuna uhaba wa umeme bali shida iliyopo ni ubovu wa miundombinu ambayo inachangia kukatika kwa umeme mara kwa mara.

Ameelezea kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/24 Shirika la Umeme (TANESCO) mkoa wa Dodoma, limetengewa kiasi cha Sh. bilioni 14, kwa ajili ya kupeleka nishati hiyo kwa wananchi na kukarabati miundombinu ili kumaliza tatizo la kukatika kwa umeme.

“Katika mwaka huu wa fedha tumepatiwa kiasi cha Sh. bilioni 14 na kati ya hizo bilioni sita ni kwa ajili ya kuboresha miundombinu yetu na kiasi kingine ni kwa ajili ya kupeleka umeme maeneo ya karibu na wananchi.” Amesema Mhandisi Shamba

Awali Afisa Usalama wa TANESCO mkoa wa Dodoma Bw. Madega Dudu, amesema shida inayowakabili hivi sasa ni pamoja na uharibifu wa miundombinu ya kusafirishia na kusambazia umeme.

"Hivi sasa kumekuwepo na shida ya wizi wa vyuma kwenye miundombinu ya kusafirishia (Grid) umeme, mafuta ya transfoma, nyaya za kopa pamoja na miundombinu ya usalama kwenye mashine umba (Transfoma).

“Tunaomba wananchi kutoa taarifa dhidi ya watu hawa ambao wanajihusisha na uharibifu wa miundombinu hii, tafiti zinaonyesha mafuta ya transfoma wanayoiba kwa kiasi yanachanganywa na mafuta ya kukaangia chipsi lakini pia mikoa ya kanda ya ziwa na bahari yanatumika kukaangia samaki.

“Na wengine wanayatumia kwa ajili ya vipodozi na kiasi kikubwa yanatumika kutengenezea vilainishi vya mitambo.” Amesema Dudu.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma Prof. Davis Mwamfupe ,ameipongeza TANESCO Mkoa wa Dodoma kwa kuboresha huduma ya nishati katika mkoa huo na kuendelea kuwafikia wateja kwa wakati pindi inapotokea changamoto yoyote.

"Sisi kama Madiwani tunawapongeza TANESCO Mkoa wa Dodoma kwa kuendelea kutoa huduma bora ya nishati Mkoa wa Dodoma hakuna changamoto kubwa ya umeme hata inapotokea mnatatua kwa wakati na kuwafikia wateja wenu kwa wakati kwa hilo tunawapongeza sana." Amesema Prof.Mwamfupe.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma Ndugu Charles Mamba aliyekuwa mgeni rasmi akifunga semina hiyo amewataka madiwani kwenda kuwa mabalozi wazuri katika kusimamia miundombimu ya umeme kwa kutoa Elimu kwa wananchi wa maeneo Yao.

"Serikali ya Chama Cha Mapinduzi ikiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DKt.Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwajali wananchi wake kwa kuwaletea huduma Bora za Nishati na kwa mikakati ya TANESCO hapa Makao Makuu ya nchi, shida ya umeme inaenda kuwa historia." Amesema Ndg Mamba


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma Mjini Ndugu Charles Mamba,akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa halmashauri ya jiji la Dodoma ulioandaliwa na Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma leo Januari 18,2024 jijini Dodoma.


Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma Prof. Davis Mwamfupe,akizungumza wakati wa Mkutano wa Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa halmashauri ya jiji la Dodoma ulioandaliwa na Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma leo Januari 18,2024 jijini Dodoma.


Meneja wa Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma Mhandisi Donasiano Shamba,akiwasilisha taarifa ya TANESCO halmashauri ya jiji la Dodoma wakati wa Mkutano wa Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa halmashauri ya jiji la Dodoma leo Januari 18,2024 jijini Dodoma.



Meneja wa Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma Mhandisi Donasiano Shamba,akisisitiza jambo zaidi wakati akiwasilisha taarifa ya TANESCO halmashauri ya jiji la Dodoma wakati wa Mkutano wa Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa halmashauri ya jiji la Dodoma leo Januari 18,2024 jijini Dodoma.



Madiwani wa kata zote 41 za jijini Dodoma wakifatilia Mkutano ulioandaliwa na Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma.



Sehemu ya kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa halmashauri ya jiji la Dodoma wakifatilia Mkutano ulioandaliwa na Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma.


Afisa Uhusiano na Huduma kwa wateja TANESCO Mkoa wa Dodoma Sarah Libogoma,akitoa elimu wakati wa Mkutano wa Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa halmashauri ya jiji la Dodoma leo Januari 18,2024 jijini Dodoma.


Afisa Usalama wa TANESCO mkoa wa Dodoma Bw. Madega Dudu,akitoa elimu kuhusu uharibifu wa miundombinu ya kusafirishia na kusambazia umeme wakati wa Mkutano wa Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa halmashauri ya jiji la Dodoma leo Januari 18,2024 jijini Dodoma.


Baadhi ya Waheshimiwa Madiwani wakitoa maoni yao wakati wa Mkutano wa Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa halmashauri ya jiji la Dodoma ulioandaliwa na Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma leo Januari 18,2024 jijini Dodoma.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma Mjini Ndugu Charles Mamba,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Mkutano wa Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa halmashauri ya jiji la Dodoma ulioandaliwa na Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma leo Januari 18,2024 jijini Dodoma.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger