Vyombo vya habari nchini Syria vinasema vikosi vya serikali vimepiga hatua muhimu na kuyateka maeneo mengi yaliyokuwa chini ya udhibiti wa waasi katika mkoa wa Aleppo ulioko kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
Mafanikio haya ya serikali yametangazwa siku moja kabla mazungumzo mapya kati ya Urusi na Uturuki kuhusiana na kuongezeka kwa mapigano katika eneo hilo.
Hatua hii ya serikali ya Syria imeutatiza ushirikiano kati ya Uturuki na Urusi, ambazo wanaunga mkono pande tofauti katika mzozo huo wa miaka tisa, ingawa zinashirikiana katika kutafuta suluhisho la kisiasa.
Kulingana na wanaharakati, hapo jana ndege za kivita za Urusi ziliishambulia miji kadhaa ukiwemo wa Anadan ambao baadaye ulitekwa na vikosi vya Syria vinavyoungwa mkono na wanamgambo wa Iran.
Duru za kijeshi zimearifu kwamba wapiganaji wa upinzani wameondoka kutoka Anadan na mji wa Haritan.
0 comments:
Post a Comment