Saturday 30 May 2020

Donald Trump aiwekea vikwazo China kufuatia sheria yake ya usalama Hong Kong

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuweka vikwazo vipya dhidi ya China, akiituhumu tena kuhusika kwa maelfu ya vifo vilivyoptokana na ugonjwa hatari wa Covid-19.

Ametangaza pia kutokubaliana na sheria ya usalama wa China kwa Hong Kong ambayo imeendelea kuzusha wasiwasi mkubwa katika kimbo hilo linalojitawala.

Donald Trump ametekelza vitisho ambavyo amekuwa akitoa kwa siku kadhaa dhidi ya China.

Rais Trump amesema kuwa China imekiuka makubaliano ya uhuru wa Hong Kong kwa kupitisha sheria ya usalama wa Kitaifa. Nakala ambayo inaruhusu kurudi kwa vyombo vya usalama vya China kwa koloni la zamani la Uingereza na ambayo kwa wengi ni tishio kwa uhuru wa eneo hilo.

"Uchina inadai kulinda usalama wa kitaifa. Lakini ukweli ni kwamba Hong Kong ni eneo huru linalojitawala, lenye usalama na ambalolinaloendelea kuistawi kiuchumi na maendeleo mbalimbali. Uamuzi wa Beijing ni hatua ya kurudi nyuma. Uamuzi ambao unaimarisha uwepo wa China kwa mfumo wa usalama kwa eneo ambalo ni uhuru, "Rais wa Marekani amesema.

Uingereza, Japan, Canada, Australia na Marekani zimeelezea wasiwasi wao kuhusu sheria ya usalama wa China kwa Hong Kong. Uingereza imesema sheria hiyo inaweza kukandamiza mamlaka ya ndani ya Hong Kong.

Hisia mbalimbali zinazidi kutolewa kufuatia hatua ya bunge la China kuidhinisha mipango ya sheria tete ya usalama kwa Hong Kong. Waziri Mkuu wa China Li Keqiang amesema sheria hiyo mpya inalenga kuulinda mji wa Hong Kong, lakini Japan, Marekani, Canada, Australia na hata Marekani zimeikosoa hatua hiyo.

Katika taarifa ya nadra, punde tu baada ya sheria hiyo kupitishwa, wizara ya mambo ya nje ya Japan imeutaja mji wa Hong Kong kama mshirika muhimu zaidi. Yoshihide Suga ambaye ni waziri mwenye hadhi ya juu katika baraza la serikali la Japan amesema.


Share:

Kansela Angela Merkel akataa kuhudhuria mkutano wa G7 Marekani

Kansela Angela Merkel amekataa kuhudhuria mkutano wa kilele wa kundi la nchi 7 zenye uchumi wa juu zaidi duniani, G7, nchini Marekani mnamo mwezi Juni, kama ilivyopendekezwa na rais wa Marekani, Donald Trump.

Angela Merkel amesema hatohodhuria mkutano huo, kwa sababu ya janga la Corona, msemaji wa serikali ya Ujerumani amelithibitishia shirika la habari la AFP leo Jumamosi.

"Kwa leo, ukizingatia hali ya jumla ya janga la Corona, hawezi kukubali kusafari kwenda Washington," amesema msemaji wa serikali ya Ujerumani, akithibitisha habari ya chombo cha habari mtandaoni cha Politico kutoka Marekani.

"Ofisi ya kansela wa Ujerumani inamshukuru rais Trump kwa mwaliko wake kwenye mkutano wa G7," msemaji wa serikali ya Ujerumani ameongeza.

Bi Merkel, ndiye kiongozi wa kwanza wa kundi la G7 (Japan, Canada, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia) kukataa rasmi mwaliko huu.

Umri wa Merkel, 65, ambaye pia ni sawa na ule wa Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe, unamweka katika hatari kubwa ya kuambukizwa haraka janga la Covid-19.

Marekani ni nchi ya kwanza kuathirika zaidi duniani (zaidi ya watu 100,000 wamefariki dunia kwa Covid-19, huku watu Milioni 1.7 wakithibitishwa kuambukizwa virusi hivyo).

Ikulu ya White ilikuwa imetangaza mwanzoni mwa mwezi Machi kuwa inasitisha maandalizi ya mkutano huo, kwa sababu ya janga la Corona, kwa kuwaleta pamoja marais na viongozi wa serikali kutoka n-kundi la G7, ingependelea mkutano huo ufanyike kupitia video.

Lakini wiki iliyopita, Donald Trump alitangaza kwamba mkutano wa kilele wa kundi la G7 utafanyika mwezi wa Juni "katika Ikulu ya White House", ingawa kuna mikutano kadhaa ambayo inaweza kufanyika katika makazi ya rais ya Camp David, katika jimbo jirani la Maryland.


Share:

Baada ya vitisho, hatimaye Trump akata uhusiano na WHO

Rais Donald Trump wa Marekani ametangaza kukata uhusiano na Shirika la Afya Duniani WHO, akidai kuwa taasisi hiyo ya kimataifa ni kikaragosi cha China.

Katika kikao na waandishi wa habari katika Ikulu ya White House jana Ijumaa, Trump alirudia tuhuma zake dhidi ya shirika hilo akidai kwamba linaipendelea China, na eti lilishindwa kushughulikia ipasavyo janga la corona.

Aidha alitumia jukwaa hilo kuituhumu China kwa kusema Dunia inahitaji majibu kutoka kwa China juu ya virusi (vya corona)

Trump amechukua uamuzi huo chini ya wiki mbili baada ya kumuandikia barua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Dunia, Tedros Adhanom Gabrayesus ambapo alidai kuwa, "Marekani itaikatia misaada WHO kikamilifu iwapo haitapiga hatua kubwa za kujiboresha ndani ya siku 30 zijazo."


Share:

PICHA: Rais Magufuli akabidhi zawadi ya Ndege aina ya Tausi kwa Marais Wastaafu Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Hati ya Makabidhiano ya zawadi ya Ndege aina ya Tausi 25 kwa Mama Maria Nyerere mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa ajili ya kuwafuga katika Makazi yake, hafla hiyo fupi ilifanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi hao Wakuu wastaafu mara baada ya kuwakabidhi zawadi ya ndege aina ya Tausi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa.

PICHA NA IKULU


Share:

Simbachawene: Serikali Ipo Katika Mchakato Kuhakikisha Mahabusu Nchini Wanafanya Kazi Magerezani Kama Wafungwa

Na Felix Mwagara, MOHA, Dar.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene amesema Serikali ipo katika mchakato wa kuhakikisha Mahabusu waliopo katika Magereza mbalimbali nchini wanaanza kufanya kazi kama ilivyokuwa kwa wafungwa.

Amesema mchakato huo ambao tayari umeanza, utakapo kamilika utaleta mapendekezo madhubuti ya jinsi gani ya kuwatumia mahabusu hao pamoja na wafungwa katika kufanya kazi za uzalishaji mali na kuhakikisha Jeshi hilo linajitegemea kikamilifu.

Akizungumza na Maafisa na Askari Magereza katika Magereza ya Segerea, Ukonga na Keko jijini Dar es Salaam, leo, kwa nyakati tofauti alipofanya ziara ya siku moja ya kusisitiza magereza yanajitegemea nchini, alisema ili binadamu ale lazima afanye kazi, na pia vitabu vitakatifu vinasisitiza hilo, hivyo mahabusu wanapaswa kufanya kazi kwa kuwa nao wanakula vyakula magerezani.

“Kuna mjadala mkubwa tunaendelea kuchakata kuhusu mahabusu waweze kufanya kazi, lakini lengo letu sio kuwafanyisha kazi za sulubu, au kazi zinazotweza utu wao, hapana, wao pamoja na wafungwa wana adhabu wanayoitumikia, tunataka kuwatumia katika kuzalisha, kwahiyo watafanya kazi kama watu wengine wanavyofanya kazi, hili naomba lieleweke,” alisema Simbachawene.

Aliongeza kuwa, “Mjadala unaendelea na tutakuja na majibu jinsi ya kuwatumia mahabusu na wafungwa, lakini tutakuja na majibu yenye mapendekezo tutashirikiana, lakini tunataka kuwatumia kwa nia njema ya kuzalisha, kama mnavyojua binadamu asipofanya kazi asile na imeandikwa katika vitabu vitakatifu, kama mtu umemfungia ndani alafu hafanyi kazi na anadai chakula na ajue kwamba asipofanya kazi hana haki ya kula, wewe umekuja ni mahabusu ili upeleke tonge hapa lazima uzalishe, huwezi kusema sifanyi kazi kwasababu ni mahabusu, hapana tutakulinda hata kwa bunduki utafanya kazi.”

Alisema lazima kuwepo na mtazamo mpana, mkubwa katika masuala ya kuzalisha na kujitegemea kwa Jeshi la Magereza, kwa ajili ya kuzalisha pamoja na kutatua matatizo mengine ndani ya Jeshi hilo ikiwemo kujenga nyumba, kulipa umeme pamoja na mahaitaji mbalimbali ya Jeshi hilo.

“Kama nilivyosema mjadala bado ni mkubwa kwa wafungwa na tunafahamu wapo chini ya Magereza, lakini hao wengine tumepewa tuwatunze wapo chini ya vyombo vingine, hivyo tunaendelea na mchakato wa kujadiliana kuhusu hilo, na ukikamilika tutawaletea majibu,” alisema Simbachawene.

Aliongeza kuwa, dhana ya Jeshi hilo kuzalisha na kujitegemea ni agizo la Amiri Jeshi Mkuu, Rais Dkt. John Magufuli kulitaka jeshi hilo kuzalisha kwa wingi ili kujitosheleza na kujitegemea.

Aidha, alilitaka Jeshi hilo kuhakikisha Magereza ya Mkoa wa Dar es Salaam yaanze kufanya kilimo cha mboga za majani na matunda pamoja na ubunifu wa uzalishaji mwingine katika mkoa huo, na magereza yaliyopo mikoani yaendelee na kilimo cha mpunga, mahindi, ufugaji pamoja na uzalishaji wa aina nyingine wanaoendelea nao katika maeneo yao.

Alisema kupitia uzalishaji mali huo utawezesha kupata fedha baada ya kuuza na kusaidia majukumu mengine ya Jeshi kuliko kutegemea fedha za matumizi mengine (OC) ambazo utolewa na Serikali kwa Jeshi hilo.

Pia Waziri Simbachawene amelitaka Jeshi hilo kuhakikisha wanahakiki mali zote za Jeshi ikiwemo mashamba yajulikane, na pia ijulikane yana hati au hayana, na mifugo ya Jeshi hilo ipo wapi na idadi yake ikiwa ni lengo la kutambua mali hizo na kuwekwa wazi kwasababu ni mali za umma.

Kwa upande wake Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP), Solomon Urio, alimshukuru Waziri huyo kwa kufanya ziara katika Mkoa huo na kuwaomba viongozi mbalimbali nchini waweze kutembelea magereza ili waweze kujifunza na kujua kazi mbalimbali zinazofanywa na Jeshi mkoani humo.

“Tunakushukuru kwa kututembelea Mheshimiwa Waziri, na maelekezo uliyotaoa tutayafanyia kazi, na pia tunawaomba viongozi mbalimbali waweze kutembelea Magereza na kujua kazi mbalimbali tunazozifanya,” alisema ACP Urio.

Simbachawene amemaliza ziara yake ya siku moja kwa kutembelea magereza hayo, ambayo ni Gereza Kuu la Mahabusu Segerea, Gereza Kuu la Ukonga na Gereza la Mahabusu la Keko, ambapo katika ziara yake alipokua taarifa ya utendaji kazi kutoka kwa Wakuu wa Magereza hayo pamoja na kuahidi changamoto zao kufanyiwa.  


Share:

Picha : RAIS MAGUFULI AWAKABIDHI ZAWADI YA TAUSI MARAIS WASTAAFU WA TANZANIA




Ndege aina ya Tausi (Picha kutoka Maktaba)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Hati ya Makabidhiano ya zawadi ya Ndege aina ya Tausi 25 kwa Mama Maria Nyerere mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa ajili ya kuwafuga katika Makazi yake, hafla hiyo fupi ilifanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi hao Wakuu wastaafu mara baada ya kuwakabidhi zawadi ya ndege aina ya Tausi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza katika hafla hiyo fupi ya Makabidhiano ya zawadi ya ndege aina ya Tausi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete wakati akitoa neno la Shukrani kwa niaba ya Marais wenzake wastaafu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete mara baada ya hafla fupi ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi katika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa. PICHA NA IKULU
Share:

FULL POWER , ZAT 50 NI SULUHISHO LA KUDUMU TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume


⇒Ngiri,

⇒Henia

⇒Kisukari

⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri

⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu

⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi

⇒Msongo wa mawazo 



⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.



FULL POWER



⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.



⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50



⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4


⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

LIVE: Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Ikulu Ya Chamwino

LIVE:  Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Ikulu Ya Chamwino


Share:

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Yatoa Bilioni 122.8

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imetoa Sh. bilioni 122.8 kwa vyuo na taasisi mbalimbali za elimu nchini kwa ajili ya ada, chakula na malazi ya wanafunzi wanaorejea vyuoni kuendelea na masomo Jumatatu.

Mkurugenzi wa HESLB, Abdul Razaq Badru, aliyasema hayo jana jijini Dodoma alipozungumza na waandishi wa habari.

Alibainisha kuwa, kati ya kiasi hicho, Sh. bilioni 63.7 ni kwa ajili ya chakula na malazi kwa wanafunzi 132,119 kupitia vyuo na taasisi za elimu 81 kwa kipindi cha miezi miwili kwanzia Juni Mosi hadi Julai 30, mwaka huu na kiasi kingine cha fedha ni malipo ya ada.

Alisema malipo ya robo ya nne ambayo ni ya mwisho kwa mwaka huu wa masomo, yatalipwa mwishoni mwa Julai mwaka huu.

Badru alisema kuwa katika kipindi cha wiki moja iliyopita kuanzia Mei 21 hadi Mei 29, mwaka huu, Sh. bilioni 59.1 zilipelekwa vyuoni kwa ajili ya ada za wanafunzi wanufaika ambazo zimelipwa kwa taasisi za elimu ya juu zaidi ya 70 nchini.

“Ni matumaini yetu kuwa fedha hizi zitavisaidia vyuo kutoa huduma bora kwa wateja wetu wapatao 132,119 waliopo katika taasisi za elimu mbalimbali nchini kote," alisema.

Vilevile, alisema tayari bodi imeshapeleka maofisa mikopo vyuoni kwa ajili ya kushughulikia mikopo ya wanafunzi.

Alisema wanafunzi wasiogope kurudi vyuoni kuendelea na masomo kwa sababu serikali imejipanga kwa kila kitu na kuwataka kuanza kuripoti kwa ajili ya kujisajili.

"Ninaomba wanafunzi wasiogope warudi shuleni, ili kuendelea na masomo kama ambavyo imetangazwa na serikali kuanzia Juni Mosi, mwaka huu," alisema.

Alisema usajili wa wanafunzi ulianza juzi na utaendelea hadi kesho, lakini watakaochelewa usajili utaendelea kufanyika Jumatatu.

Badru alisema Benki za biashara ziko tayari kwa ajili ya kusaidia mchakato wa malipo ya mikopo kwa wanafunzi wa vyuo.


Share:

Polisi Aliyemuua Kikatili Mmarekani Mweusi Ashitakiwa kwa Mauaji ya Bila Kukusudia

Afisa wa polisi anaetuhumiwa kwa mauaji ya kikatili ya  Mmarekani mweusi, George Floyd ametiwa mbaroni na kushtakiwa kwa kosa la mauaji   kufuatia kifo cha Raia huyo mweusi ambaye alimuua kwa kumkanyaga shingo na kumfanya akose pumzi

Hayo yanatokea katika kipindi ambacho mamlaka nchini  humo zimetangaza marufuku za kutotoka nje baada ya vurugu za maandamano ya siku tatu ambazo zimesababisha baadhi ya maeneo kuchomwa moto. 

Derek Chauvin, afisa wa polisi mzungu ambae alichukuliwa video, ikionesha kambana kwa kutumia goti shingoni, marehemu George Floyd kwa karibu dakika tisa, anashitakiwa kwa kusababisha kifo pasipo kukusudia


Share:

Sikonge Yaagizwa Ianze Kutibu Wananchi Katika Hospitali Ya Wilaya Yake

NA TIGANYA VINCENT
IDARA ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge imeagizwa kuhamia katika jengo la Utawala katika Hospitali ya Wilaya hiyo na waanze kutoa huduma ya watibabu kwa wananchi.

Kauli hiyo imeolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Peres Magiri wakati akitoa salamu za Serikali katika Kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya tatu

Alisema wakati wakiendelea kusubiri vifaa tiba na vifaa vingine kwa ajili ya Hospitali hiyo ya Wilaya ni vema wakaanza na utoaji wa huduma za matibabu kwa wagonjwa wa nje.

Magiri aliutaka uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge kutoa walau sehemu ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kujenga vyoo ili majengo yote muhimu ya awali yawepo na huduma zianze.

Alisema wanaweza kuanza kutoa huduma kama zile zinazotolewa kwa kiwango cha Zahanati cha kuanzia walau asubuhi hadi jioni kila siku.

Magiri alisema hatua hiyo itawasaidia wananchi wanaoishi karibu na eneo hilo wasipate shida ya kuembea umbali mrefu kutafuta huduma kupima malaria na magonjwa mengine.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Peter Nzalalila alisema majengo ya Hospitali ya Wilaya hiyo hayakujengwa kutazamwa bali kutoa huduma kwa wananchi.

Alisema ni vema Mejimenti ya Halmashauri hiyo ikaangalia uwezekano wa kuanza kutoa huduma za matatibu katika eneo hilo kwa kutumia watalaamu waliopo wakati wakisubiri kupata wengine.

MWISHO


Share:

LIVE: Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Ikulu Ya Chamwino

LIVE: Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Ikulu Ya Chamwino


Share:

Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Kabudi Ataka Nchi Za Sadc Kuimarisha Ushirikiano

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof Palamagamba Kabudi amezitaka Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuimarisha ushirikiano na umoja wakati huu wa kuenea kwa janga la  Virusi vya Corona huku bidhaa na huduma muhimu zinazovuka mipaka baina ya nchi na zikiendelea kutolewa.

Prof. Kabudi amesema hayo jijini Dar es salaam wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC kwa njia ya Video katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

“Nawaomba Nchi zote Wanachama wa SADC tuimarishe umoja na mshikamano wetu wakati huu wa kuenea kwa janga la Virusi vya Corona, huku bidhaa na huduma muhimu zinazovuka mipaka baina ya nchi nan chi zikiendelea kutolewa, huu ni wakati wa kuepuka vitendo vya kujitenga na kuongeza mashauriano baina ya nchi,” amesema.

Aidh Mhe Waziri ameziomba Nchi za SADC kuwapa heshima na kuthamini utu wa madereva wanaosafirisha bidhaa na huduma muhimu kuvuka mipaka ya nchi kwa wakati huu ambao ugonjwa wa corona umeenea katika nchi wanachama.

Amesema Nchi wanachama zinapaswa kuchukua hatua za kukabiliana na ueneaji wa virusi vya Corona bila ya kuwanyanyapaa madereva na kuwachukulia kama watu wanaosambaza virusi hivyo na kuongeza kuwa madereva hao wanapaswa kupewa heshima stahiki kama binadamu wengine na kuwashukuru kutokana na hatari wanayochukua ya kusafirisha mizigo na huduma wakati huu wa kuenea kwa janga hilo.

“Madereva wetu wamevunjika moyo kwa sababu wanaonekana kama wao ndio wanaosambaza virusi vya Corona na sio askari wazuri ambao wanatoa huduma ya kusafirisha huduma na biidhaa muhimu wakati huu wa mlipuko, katika nchi za jumuiya,”

Ameziomba nchi za SADC kuwapa heshima na kuthamini utu wa madereva hao huku zikiendelea kuchukua tahadhari za kupambana na janga la virusi vya corona na kuongeza kuwa umoja wetu ni muhimu sana kwa wakati huu.

“Naziomba nchi zetu tuwape heshima na kuthamini utu wa madereva hao na kuwapa heshima wanayostahili huku tukiendelea kuchukua tahadhari zinazotolewa na wataalamu wa afya katika kukabiliana na janga hilo,” alisema.

Prof. Kabudi amesema janga la COVID 19 linaonekana kama halitoisha ndani ya muda mfupi na nchi za ukanda wa SADC lazima ziishi  kwa kufuata mifumo salama katika biashara na usafirishaji wa huduma na bidhaa ili kupata ukuaji wa uchumi na kuondoa umasikini huku tukiwa bado tunakabiliana na janga hili la ueneaji wa virusi vya corona.

Amesema wakati hatua za kukabiliana na janga la Corona zikiendelea kuchukuliwa nchi za SADC lazima zikumbuke dhumuni la utangamano miongoni mwa nchi wanachama ambalo ni kuboresha ufanyaji biashara baina ya nchi na nchi na hivyo kutowaangusha waanzilishi wa Jumuiya ya SADC.

Amesema ufanyaji wa biashara baina ya nchi na nchi ndani ya SADC uko chini ya asilimia 20 hali ambayo inazuia nchi wanachama kuona ukuaji wa uchumi wake na kuongeza kuwa janga la corona lichukuliwe kama chachu ya kuongeza juhudi za kuinua kiwango cha ufanyaji biashara baina ya nchi na nchi kupitia utekelezajia wa Protokali ya SADC katika biashara ya 2005 na uanzishwaji wa eneo huru la biashara la SADC.

Ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri la SADC Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Isack Kamwele na Waziri wa Maliasilia na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala.


Share:

Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Kabudi Afanya Mazungumzo Na Balozi Wa Italia Nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italia nchini Mhe. Roberto Mengoni katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo pia yalihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge, ambapo walijadili masuala mbalimbali yanayohusu mahusiano baina ya Tanzania na Italia.

Aidha, walitumia mazungumzo hayo kujadili hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania pamoja na Serikali ya Italia katika kupambana na ugonjwa wa COVID-19. Mhe. Waziri alifahamisha kuwa hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali ya Tanzania kwenye mapambano ya ugonjwa huo zimezingatia mazingiria na hali halisi ya Tanzania pamoja na nchi jirani zinazozunguka Tanzania.

Kwa upande wake Balozi Mengoni alipongeza juhudi hizo za Serikali ambapo alifahamisha kuwa Serikali yake ya Italia inaziunga mkono na kwamba ipo tayari kutoa ushirikiano pale itakapohitajika kufanya hivyo.

Viongozi hao walikubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kihistoria baina ya Mataifa hayo mawili ambao umejikita katika sekta za elimu, afya, utalii pamoja na biashara na uwekezaji.


Share:

UTAFITI MPYA CHANJO YA CORONA WAONESHA MATUMAINI


Utafiti wa jarida la kitabibu la The Lancet umeonesha chanjo ya COVID-19 ya China imeleta matumaini baada ya kujaribiwa kwa watu wazima 108 wenye umri wa miaka 18 hadi 60 katika jimbo la Wuhan. 

Matokeo ya awali kutokana na jaribio la watafiti wa nchini China yameonesha chanjo hiyo ni salama, himilivu na yenye uwezo wa kuzalisha kinga dhidi ya SARS-COV-2 ambavyo ni visababishi vya COVID-19 kwa binadamu.

Utafiti huo umeonesha matumaini katika siku 28 za kwanza ambapo matokeo ya mwisho yanatarajia kutolewa ndani ya miezi sita, huku Profesa wa kitengo cha magonjwa ya kuambukiza na afya ya jamii katika Chuo Kikuu cha California, Robert Schooley akisema chanjo hiyo ni himilivu.

"Chanjo imeonesha kuwa ni himilivu kutokana na dozi tatu zilizojaribiwa na watu waliojaribiwa wameonekana kutengeneza kinga dhidi ya virusi vya Corona", amesema Prof. Schooley.

Prof. Schooley amesema kuwa utafiti zaidi unatakiwa kufanyika ili kubaini endapo nguvu ya kinga ya mwili itakuwepo na kinga ya T-cells inayopatikana mwilini itaendelea kupungua baada ya siku 28 huku akitaja umuhimu wa dunia kuungana katika utafiti wa maendeleo ya chanjo ya COVID-19 kwa pamoja.

Chanzo- EATV
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi May 30



















Share:

Friday 29 May 2020

Team Assistant at World Bank Dar Es Salaam,Tanzania

Team Assistant at World Bank Dar Es Salaam,Tanzania   Job #: req7419 Organization: World Bank Sector: Administration/Office Support Grade: GB Term Duration: 3 years 0 months Recruitment Type: Local Recruitment Location: Dar Es Salaam,Tanzania Required Language(s): English Preferred Language(s): Closing Date: 6/7/2020 (11:59pm UTC) Description Do you want to build a career that is truly worthwhile? Working at… Read More »

The post Team Assistant at World Bank Dar Es Salaam,Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger