Saturday 30 May 2020

LIVE: Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Ikulu Ya Chamwino

LIVE:  Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Ikulu Ya Chamwino


Share:

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Yatoa Bilioni 122.8

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imetoa Sh. bilioni 122.8 kwa vyuo na taasisi mbalimbali za elimu nchini kwa ajili ya ada, chakula na malazi ya wanafunzi wanaorejea vyuoni kuendelea na masomo Jumatatu.

Mkurugenzi wa HESLB, Abdul Razaq Badru, aliyasema hayo jana jijini Dodoma alipozungumza na waandishi wa habari.

Alibainisha kuwa, kati ya kiasi hicho, Sh. bilioni 63.7 ni kwa ajili ya chakula na malazi kwa wanafunzi 132,119 kupitia vyuo na taasisi za elimu 81 kwa kipindi cha miezi miwili kwanzia Juni Mosi hadi Julai 30, mwaka huu na kiasi kingine cha fedha ni malipo ya ada.

Alisema malipo ya robo ya nne ambayo ni ya mwisho kwa mwaka huu wa masomo, yatalipwa mwishoni mwa Julai mwaka huu.

Badru alisema kuwa katika kipindi cha wiki moja iliyopita kuanzia Mei 21 hadi Mei 29, mwaka huu, Sh. bilioni 59.1 zilipelekwa vyuoni kwa ajili ya ada za wanafunzi wanufaika ambazo zimelipwa kwa taasisi za elimu ya juu zaidi ya 70 nchini.

“Ni matumaini yetu kuwa fedha hizi zitavisaidia vyuo kutoa huduma bora kwa wateja wetu wapatao 132,119 waliopo katika taasisi za elimu mbalimbali nchini kote," alisema.

Vilevile, alisema tayari bodi imeshapeleka maofisa mikopo vyuoni kwa ajili ya kushughulikia mikopo ya wanafunzi.

Alisema wanafunzi wasiogope kurudi vyuoni kuendelea na masomo kwa sababu serikali imejipanga kwa kila kitu na kuwataka kuanza kuripoti kwa ajili ya kujisajili.

"Ninaomba wanafunzi wasiogope warudi shuleni, ili kuendelea na masomo kama ambavyo imetangazwa na serikali kuanzia Juni Mosi, mwaka huu," alisema.

Alisema usajili wa wanafunzi ulianza juzi na utaendelea hadi kesho, lakini watakaochelewa usajili utaendelea kufanyika Jumatatu.

Badru alisema Benki za biashara ziko tayari kwa ajili ya kusaidia mchakato wa malipo ya mikopo kwa wanafunzi wa vyuo.


Share:

Polisi Aliyemuua Kikatili Mmarekani Mweusi Ashitakiwa kwa Mauaji ya Bila Kukusudia

Afisa wa polisi anaetuhumiwa kwa mauaji ya kikatili ya  Mmarekani mweusi, George Floyd ametiwa mbaroni na kushtakiwa kwa kosa la mauaji   kufuatia kifo cha Raia huyo mweusi ambaye alimuua kwa kumkanyaga shingo na kumfanya akose pumzi

Hayo yanatokea katika kipindi ambacho mamlaka nchini  humo zimetangaza marufuku za kutotoka nje baada ya vurugu za maandamano ya siku tatu ambazo zimesababisha baadhi ya maeneo kuchomwa moto. 

Derek Chauvin, afisa wa polisi mzungu ambae alichukuliwa video, ikionesha kambana kwa kutumia goti shingoni, marehemu George Floyd kwa karibu dakika tisa, anashitakiwa kwa kusababisha kifo pasipo kukusudia


Share:

Sikonge Yaagizwa Ianze Kutibu Wananchi Katika Hospitali Ya Wilaya Yake

NA TIGANYA VINCENT
IDARA ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge imeagizwa kuhamia katika jengo la Utawala katika Hospitali ya Wilaya hiyo na waanze kutoa huduma ya watibabu kwa wananchi.

Kauli hiyo imeolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Peres Magiri wakati akitoa salamu za Serikali katika Kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya tatu

Alisema wakati wakiendelea kusubiri vifaa tiba na vifaa vingine kwa ajili ya Hospitali hiyo ya Wilaya ni vema wakaanza na utoaji wa huduma za matibabu kwa wagonjwa wa nje.

Magiri aliutaka uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge kutoa walau sehemu ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kujenga vyoo ili majengo yote muhimu ya awali yawepo na huduma zianze.

Alisema wanaweza kuanza kutoa huduma kama zile zinazotolewa kwa kiwango cha Zahanati cha kuanzia walau asubuhi hadi jioni kila siku.

Magiri alisema hatua hiyo itawasaidia wananchi wanaoishi karibu na eneo hilo wasipate shida ya kuembea umbali mrefu kutafuta huduma kupima malaria na magonjwa mengine.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Peter Nzalalila alisema majengo ya Hospitali ya Wilaya hiyo hayakujengwa kutazamwa bali kutoa huduma kwa wananchi.

Alisema ni vema Mejimenti ya Halmashauri hiyo ikaangalia uwezekano wa kuanza kutoa huduma za matatibu katika eneo hilo kwa kutumia watalaamu waliopo wakati wakisubiri kupata wengine.

MWISHO


Share:

LIVE: Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Ikulu Ya Chamwino

LIVE: Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Ikulu Ya Chamwino


Share:

Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Kabudi Ataka Nchi Za Sadc Kuimarisha Ushirikiano

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof Palamagamba Kabudi amezitaka Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuimarisha ushirikiano na umoja wakati huu wa kuenea kwa janga la  Virusi vya Corona huku bidhaa na huduma muhimu zinazovuka mipaka baina ya nchi na zikiendelea kutolewa.

Prof. Kabudi amesema hayo jijini Dar es salaam wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC kwa njia ya Video katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

“Nawaomba Nchi zote Wanachama wa SADC tuimarishe umoja na mshikamano wetu wakati huu wa kuenea kwa janga la Virusi vya Corona, huku bidhaa na huduma muhimu zinazovuka mipaka baina ya nchi nan chi zikiendelea kutolewa, huu ni wakati wa kuepuka vitendo vya kujitenga na kuongeza mashauriano baina ya nchi,” amesema.

Aidh Mhe Waziri ameziomba Nchi za SADC kuwapa heshima na kuthamini utu wa madereva wanaosafirisha bidhaa na huduma muhimu kuvuka mipaka ya nchi kwa wakati huu ambao ugonjwa wa corona umeenea katika nchi wanachama.

Amesema Nchi wanachama zinapaswa kuchukua hatua za kukabiliana na ueneaji wa virusi vya Corona bila ya kuwanyanyapaa madereva na kuwachukulia kama watu wanaosambaza virusi hivyo na kuongeza kuwa madereva hao wanapaswa kupewa heshima stahiki kama binadamu wengine na kuwashukuru kutokana na hatari wanayochukua ya kusafirisha mizigo na huduma wakati huu wa kuenea kwa janga hilo.

“Madereva wetu wamevunjika moyo kwa sababu wanaonekana kama wao ndio wanaosambaza virusi vya Corona na sio askari wazuri ambao wanatoa huduma ya kusafirisha huduma na biidhaa muhimu wakati huu wa mlipuko, katika nchi za jumuiya,”

Ameziomba nchi za SADC kuwapa heshima na kuthamini utu wa madereva hao huku zikiendelea kuchukua tahadhari za kupambana na janga la virusi vya corona na kuongeza kuwa umoja wetu ni muhimu sana kwa wakati huu.

“Naziomba nchi zetu tuwape heshima na kuthamini utu wa madereva hao na kuwapa heshima wanayostahili huku tukiendelea kuchukua tahadhari zinazotolewa na wataalamu wa afya katika kukabiliana na janga hilo,” alisema.

Prof. Kabudi amesema janga la COVID 19 linaonekana kama halitoisha ndani ya muda mfupi na nchi za ukanda wa SADC lazima ziishi  kwa kufuata mifumo salama katika biashara na usafirishaji wa huduma na bidhaa ili kupata ukuaji wa uchumi na kuondoa umasikini huku tukiwa bado tunakabiliana na janga hili la ueneaji wa virusi vya corona.

Amesema wakati hatua za kukabiliana na janga la Corona zikiendelea kuchukuliwa nchi za SADC lazima zikumbuke dhumuni la utangamano miongoni mwa nchi wanachama ambalo ni kuboresha ufanyaji biashara baina ya nchi na nchi na hivyo kutowaangusha waanzilishi wa Jumuiya ya SADC.

Amesema ufanyaji wa biashara baina ya nchi na nchi ndani ya SADC uko chini ya asilimia 20 hali ambayo inazuia nchi wanachama kuona ukuaji wa uchumi wake na kuongeza kuwa janga la corona lichukuliwe kama chachu ya kuongeza juhudi za kuinua kiwango cha ufanyaji biashara baina ya nchi na nchi kupitia utekelezajia wa Protokali ya SADC katika biashara ya 2005 na uanzishwaji wa eneo huru la biashara la SADC.

Ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri la SADC Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Isack Kamwele na Waziri wa Maliasilia na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala.


Share:

Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Kabudi Afanya Mazungumzo Na Balozi Wa Italia Nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italia nchini Mhe. Roberto Mengoni katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo pia yalihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Kanali Wilbert A. Ibuge, ambapo walijadili masuala mbalimbali yanayohusu mahusiano baina ya Tanzania na Italia.

Aidha, walitumia mazungumzo hayo kujadili hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania pamoja na Serikali ya Italia katika kupambana na ugonjwa wa COVID-19. Mhe. Waziri alifahamisha kuwa hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Serikali ya Tanzania kwenye mapambano ya ugonjwa huo zimezingatia mazingiria na hali halisi ya Tanzania pamoja na nchi jirani zinazozunguka Tanzania.

Kwa upande wake Balozi Mengoni alipongeza juhudi hizo za Serikali ambapo alifahamisha kuwa Serikali yake ya Italia inaziunga mkono na kwamba ipo tayari kutoa ushirikiano pale itakapohitajika kufanya hivyo.

Viongozi hao walikubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kihistoria baina ya Mataifa hayo mawili ambao umejikita katika sekta za elimu, afya, utalii pamoja na biashara na uwekezaji.


Share:

UTAFITI MPYA CHANJO YA CORONA WAONESHA MATUMAINI


Utafiti wa jarida la kitabibu la The Lancet umeonesha chanjo ya COVID-19 ya China imeleta matumaini baada ya kujaribiwa kwa watu wazima 108 wenye umri wa miaka 18 hadi 60 katika jimbo la Wuhan. 

Matokeo ya awali kutokana na jaribio la watafiti wa nchini China yameonesha chanjo hiyo ni salama, himilivu na yenye uwezo wa kuzalisha kinga dhidi ya SARS-COV-2 ambavyo ni visababishi vya COVID-19 kwa binadamu.

Utafiti huo umeonesha matumaini katika siku 28 za kwanza ambapo matokeo ya mwisho yanatarajia kutolewa ndani ya miezi sita, huku Profesa wa kitengo cha magonjwa ya kuambukiza na afya ya jamii katika Chuo Kikuu cha California, Robert Schooley akisema chanjo hiyo ni himilivu.

"Chanjo imeonesha kuwa ni himilivu kutokana na dozi tatu zilizojaribiwa na watu waliojaribiwa wameonekana kutengeneza kinga dhidi ya virusi vya Corona", amesema Prof. Schooley.

Prof. Schooley amesema kuwa utafiti zaidi unatakiwa kufanyika ili kubaini endapo nguvu ya kinga ya mwili itakuwepo na kinga ya T-cells inayopatikana mwilini itaendelea kupungua baada ya siku 28 huku akitaja umuhimu wa dunia kuungana katika utafiti wa maendeleo ya chanjo ya COVID-19 kwa pamoja.

Chanzo- EATV
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi May 30



















Share:

Friday 29 May 2020

Team Assistant at World Bank Dar Es Salaam,Tanzania

Team Assistant at World Bank Dar Es Salaam,Tanzania   Job #: req7419 Organization: World Bank Sector: Administration/Office Support Grade: GB Term Duration: 3 years 0 months Recruitment Type: Local Recruitment Location: Dar Es Salaam,Tanzania Required Language(s): English Preferred Language(s): Closing Date: 6/7/2020 (11:59pm UTC) Description Do you want to build a career that is truly worthwhile? Working at… Read More »

The post Team Assistant at World Bank Dar Es Salaam,Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Human Resources Associate at UNDP – United Nations Development Programme

Human Resources Associate, Dar es Salaam, Tanzania Organization: UNDP – United Nations Development Programme Country: Tanzania City: Dar es Salaam, Tanzania Office: UNDP Dar es Salaam Closing date: Sunday, 7 June 2020 Human Resources Associate Advertised on behalf of : Location : Dar es Salaam, TANZANIA Application Deadline : 07-Jun-20 (Midnight New York, USA) Type of Contract : FTA Local Post Level : GS-6 Languages Required : English Starting… Read More »

The post Human Resources Associate at UNDP – United Nations Development Programme appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Administration Assistant at UNOPS – United Nations Office for Project Services

Administration Assistant at UNOPS – United Nations Office for Project Services Job categoriesAdministration, Project Management Vacancy codeVA/2020/B5323/19871 Department/officeAFR, KEMC, Kenya Duty stationDar Es Salaam, United Republic of Tanzania Contract typeLocal ICA Support Contract levelLICA-4 DurationOn going subject to satisfactory performance and funding availability Application period22-May-2020 to 06-Jun-2020 Applications to vacancies must be received before midnight Copenhagen time (CET)… Read More »

The post Administration Assistant at UNOPS – United Nations Office for Project Services appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Save the children Job vacancy: Economic and Fiscal Governance (EFG) Officer – Zanzibar – (200002P0)

Job Description Economic and Fiscal Governance (EFG) Officer – Zanzibar – (200002P0) Economic and Fiscal Governance (EFG) Officer TEAM/PROGRAM: Operations LOCATION: Zanzibar GRADE: 4 CONTRACT LENGTH: 1 year, renewable CHILD SAFEGUARDING: Level 3: √ the post holder will have contact with children and/or young people either frequently (e.g. once a week or more) or intensively (e.g. four days… Read More »

The post Save the children Job vacancy: Economic and Fiscal Governance (EFG) Officer – Zanzibar – (200002P0) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

FAO JOBS: Specialist for the Development of Food Based Dietary Guidance, Tanzania

Closing date: Sunday, 7 June 2020 2001190 Specialist for the Development of Food Based Dietary Guidance – Tanzania Mainland Job Posting: 25/May/2020 Closure Date: 07/Jun/2020, 9:59:00 PM Organizational Unit : FRURT Job Type: Non-staff opportunities Type of Requisition : PSA (Personal Services Agreement) Grade Level : N/A Primary Location: Tanzania, United Republic of Duration : 50 Days within… Read More »

The post FAO JOBS: Specialist for the Development of Food Based Dietary Guidance, Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

FAO JOBS: Specialist for the Development of Food Based Dietary Guidance – Zanzibar 

Job Description  2001189 Specialist for the Development of Food Based Dietary Guidance – Zanzibar Job Posting : 25/May/2020 Closure Date : 07/Jun/2020, 9:59:00 PM Organizational Unit: FRURT Job Type : Non-staff opportunities Type of Requisition: PSA (Personal Services Agreement) Grade Level: N/A Primary Location : Tanzania, United Republic of-Zanzibar Duration: 50 Days within Four Months Post Number: N/A ___________________________________________________________________________________________________________________ FAO seeks gender, geographical and linguistic diversity in… Read More »

The post FAO JOBS: Specialist for the Development of Food Based Dietary Guidance – Zanzibar  appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Curriculum Development Coordinator(Tanzania National Only) Tanzania, Norwegian Refugee Council

Duties and responsibilities Adhere to NRC policies, tools, handbooks and guidelines Prepare and develop status reports as required by supervisor Promote and share ideas for improvement Ensure compliance with NRC procedures and policies Ensure compliance with NRC (global and national) policies and procedures, handbooks and guidelines and/or propose new initiatives to bridge gaps and implement these. Work with… Read More »

The post Curriculum Development Coordinator(Tanzania National Only) Tanzania, Norwegian Refugee Council appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Taarifa Kwa Umma Toka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU)

1. UTANGULIZI
Ndugu Waandishi wa Habari,
Awali ya yote napenda kumshukuru Mungu kwa jinsi anavyotulinda na kutuwezesha kutekeleza majukumu yetu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu.

Kipekee napenda kumpongeza na kumshukuru kwa dhati Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dr. John Pombe Joseph Magufuli kwa uongozi wake makini na thabiti katika kuliongoza Taifa letu. Aidha tunaishukuru Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa miongozo mbalimbali na usimamizi wa elimu hapa nchini.
 
Nichukue fursa hii kuzungumza nanyi hapa Jijini Mwanza katika Ofisi Ndogo ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ili kuvifahamisha Vyuo Vikuu, Wananchi, na Wadau wengine wa elimu ya juu kuhusu maandalizi ya kufunguliwa kwa muhula wa pili wa masomo kwa vyuo vikuu hapa nchini.

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania tunaamini kuwa ninyi ni wadau muhimu katika mchakato wa maendeleo kwani kupitia kwenu, taarifa mbalimbali zinazohusu Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania zinawafikia umma wa Watanzania.
 
Ndugu Waandishi wa Habari,
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) ni Taasisi ya Serikali, iliundwa mwaka 2005 kwa Sheria ya Vyuo Vikuu Sura ya 346 ya Sheria za Tanzania. TCU ilitokana na maboresho yaliyofanywa na Serikali kwa lililokuwa Baraza la Ithibati la Elimu ya Juu (HEAC) lililoanzishwa mwaka 1995 kwa Sheria ya Elimu Sura ya 523 ya Sheria za Tanzania.
 
Lengo la kuanzishwa HEAC ilikuwa kuthibiti ubora wa vyuo vikuu nchini vilivyokuwa vinaanzishwa na kuendeshwa na taasisi binafsi ili kupata wahitimu wenye elimu, maarifa, ujuzi na uwezo wa kustahimili ushindani kitaifa, kikanda na kimataifa.
 
TCU ina majukumu makubwa matatu, kwanza ni kusimamia sheria, kanuni na taratibu za uanzishaji na uendeshaji wa vyuo vikuu nchini. Pili kusaidia na kutoa miongozo kwa vyuo vikuu kuhusu uthibiti wa ubora wa vyuo vikuu, njia mbalimbali za uendeshaji wa vyuo, kuandaa na kuratibu mafunzo mbalimbali kwa Wahadhiri, waendashaji na viongozi wa vyuo vikuu nchini. Jukumu la tatu ni kutoa ushauri kwa umma, vyuo vikuu, na serikali kupitia waziri mwenye dhamana ya elimu ya juu nchini kuhusiana na mabadiliko mbalimbali ya sayansi, teknolojia, sera na muelekeo wa elimu ya vyuo vikuu nchini na duniani kwa ujumla.
 
2. MAANDALIZI YA VYUO VIKUU KUPOKEA WANAFUNZI
Ndugu Waandishi wa Habari,
Kufuatia maelekezo ya Serikali kwamba vyuo vikuu vyote vifunguliwe tarehe 01 Juni, 2020 Tume imetoa mwongozo na ushauri kwa vyuo vikuu vyote kupitia mkutano wa dharura uliyoitishwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia tarehe 23 Mei, 2020 jijini Dodoma ambapo TCU ilishauri mambo yafuatayo yazingatiwe na Vyuo Vikuu:

1) Kwa kuwa muda uliobaki kuhitimisha mwaka wa masomo ni mfupi, Vyuo vihakikishe kuwa ufundishaji wa mitaala unakamilika ndani ya muda uliobaki katika mwaka wa masomo 2019/2020 bila kuathiri ubora; na
2) Vyuo vihakikishe kuwa masuala ya mitihani na mafunzo kwa vitendo yanazingatiwa katika kukamilika katika muda uliobaki katika mwaka wa masomo 2019/2020 bila kuathiri ubora.
 
Aidha ilikubalika kuwa shughuli zote za masomo zikamilike kabla ya wiki ya mwisho ya mwezi Oktoba ili kutoa fursa kwa vyuo kujiandaa kupokea wanafunzi wapya wa mwaka wa kwanza na kuanza kwa mwaka mpya wa masomo 2020/2021.
 
3. WITO KWA VYUO VIKUU
Tume ya Vyuo Vikuu inatoa wito kwa vyuo vikuu vyote kuhakikisha kuwa vinazingatia miongozo mbalimbali ya ubora ili kutoa wahitimu mahiri wanaokidhi viwango vya ubora na mahitaji ya maendeleo ya taifa.
 
Aidha katika kuhakikisha kuwa ufundishaji wa mitaala unakamilika ndani ya muda uliobaki katika mwaka wa masomo 2019/2020, Vyuo vinashauriwa kutumia mbinu mbalimbali za ufundishaji ikwemo matumizi ya TEHAMA bila kuathiri ubora. Tume inashauri vyuo vikuu kutumia mbinu mbalimbali na mikakati mbalimbali ya ufundishaji ikiwa ni pamoja na matumizi ya teknolojia itakayowezesha kufikia azma ya Serikali ya kuendelea na shughuli za masomo bila kuathiri ubora na mipango mingine ya maendeleo.
 
4. HITIMISHO
TCU inatoa wito kwa wanafunzi kutoa ushirikiano kwa uongozi wa vyuo katika kufanikisha utoaji wa mafunzo katika kipindi hiki muhimu. Aidha, ili kuendana na kasi ya maendeleo duniani hatuna budi kubuni na kutumia njia na teknolojia mbalimbali za ufundishaji.
 
Imetolewa na:


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger