Tuesday 2 July 2019

Daktari Atoa Ushahidi Kesi Ya Mbowe na Vigogo Wengine CHADEMA

Shahidi wa tano, Inspekta Msaidizi Dk. Juma Alfani (54) katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake, amedai mahakamani kwamba aliwapokea Koplo Rahim na Konstebo Fikiri wakiwa wanapiga kelele za kulalamika maumivu ya majeraha waliyopata kwenye maandamano.

Kadhalika, amedai kuwa Koplo Rahim alikuwa anaweweseka huku akilalamika maumivu shingoni kwa sababu alikuwa hajitambui na Konstebo Fikiri alikuwa anavuja damu nyingi kichwani.

Madai hayo aliyatoa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliyoketi chini ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba, wakati akisikiliza ushahidi wa Jamhuri dhidi ya vigogo tisa wa Chadema.

Jopo la Jamhuri liliongozwa na Mawakili wa Serikali Wakuu Faraja Nchimbi, Paul Kadushi, Dk. Zainabu Mango, Mawakili wa Serikali Jacqueline Nyantori, Wankyo Simon na Salimu Msemo.

Akiongozwa na Wakili Msemo, shahidi alidai kuwa Februari 16, mwaka jana, alikuwa kazini zamu ya usiku.

"Saa 5:40 usiku nikiwa wodi ya wazazi alikuja muuguzi wa zamu akaniarifu nahitajika kitengo cha dharura. Nilipokwenda niliwakuta wagonjwa wawili mmoja akivuja damu, huku akipiga kelele za maumivu na mwingine akiwa anaweweseka hana fahamu," alidai.

Aliongeza katika ushahidi wake kuwa: "Niliwaagiza wauguzi wawachome sindano za maumivu, nikamhoji aliyekuwa anatokwa damu kichwani, Fikiri kimetokea nini, akanieleza walikuwa wanatuliza maandamano ndipo wakajeruhiwa.

“Nilipojaribu kumhoji Rahim alikuwa anaweweseka na kuonyesha maumivu kwenye shingo upande wa kulia," alidai Dk. Alfani ni daktari wa Hospitali ya Polisi Barabara ya Kilwa ambayo ni ya rufani kwa zahanati zote za polisi.

Alidai kuwa baada ya kuwakagua majeruhi na kujiridhisha aliagiza wapelekwe wodini na walilazwa mpaka Februari 18, mwaka jana waliporuhusiwa. Pia alidai kuwa baada ya Rahimu kuendelea kulalamika maumivu aliagiza akafanyiwe kipimo cha CT Scan. Kesi hiyo inaendelea leo kusikilizwa ushahidi wa Jamhuri.

Jopo la utetezi liliongozwa na Wakili Profesa Abdallah Safari, Peter Kibatala, John Mallya na Hekima Mwasipu.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine ni Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya; Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko; Katibu Mkuu wa Chadema, Vicent Mashinji; Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika; Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa hao wanadaiwa kuwa kati ya Februari Mosi na Februari 16, mwaka huu Mbowe na wenzake wakiwa Kinondoni, Dar es Salaam kwa pamoja walikula njama na wengine ambao hawapo mahakamani ya kutenda kosa la jinai ikiwamo kuendelea na mkusanyiko isivyo halali na kusababisha chuki na uchochezi wa uasi.

Ilidaiwa kuwa Februari 16, mwaka jana, Bulaya alishawishi kutenda kosa la jinai katika viwanja vya Buibui vilivyoko Kinondoni, Dar es Salaam kwa kuwataka wakazi wa eneo hilo kufanya maandamano yenye vurugu.

Pia ilidaiwa kuwa Februari 16, mwaka jana katika barabara ya Kawawa eneo la Konondoni Mkwajuni kwa pamoja washtakiwa na wenzao zaidi ya 12, walifanya mkusanyiko na kukaidi amri halali ya ofisa wa Jeshi la Polisi Gerald Ngiichi na kusababisha kifo cha Akwilina Akwiline na askari polisi wawili Konstebo Fikiri na Koplo Rahim Msangi kujeruhiwa.


Share:

Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO) Watakiwa Kujiendesha Kwa Faida Na Kutoa Gawio Serikalini

Na. Edward Kondela
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeitaka Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO) kubadilika na kufanya shughuli zake kwa tija ili iweze kunufaika na rasilimali ardhi na mifugo inayomiliki.

Akizungumza wakati akitembelea na kujionea shughuli zinazofanywa katika ranchi za Ruvu iliyopo Mkoani Pwani na Mkata iliyopo Mkoani Morogoro jana (01.07.2019), Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amezitaka ranchi hizo zilizo chini ya NARCO kuhakikisha zinatumia vitu ardhi inazomiliki ili kufuga mifugo itakayoongeza tija kwa taifa.

Prof. Gariel akiwa katika Ranchi ya Ruvu amemuelekeza meneja wa ranchi hiyo Bw. Elisa Binamungu kuhakikisha ranchi hiyo inafuatilia pia madeni yote inayodai ili iweze kupata fedha na kujiendesha kwa kutumia fursa zilizopo za kuuza kwa tija mazao ya mifugo ikiwemo nyama na maziwa.

“Lengo la ziara yangu ni kuhakikisha mnatekeleza agizo alilolitoa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina June 15 mwaka huu, alipokutana na viongozi wa NARCO la kuwataka kubadilika kiutendaji na muweze kunufaika na ardhi na mifugo mnayomiliki hali kadhalika kuweza kutoa gawio serikalini.” Alisema Prof. Gabriel.

Akiwa katika Ranchi ya Mkata Prof. Gabriel amejionea ujenzi wa kisima kwa ajili ya kupata maji ya kunyweshea mifugo na kumuagiza meneja wa ranchi hiyo Bw. Iddy Athuman kuhakikisha kisima hicho kinakamilika katika mwaka wa fedha 2019/2020 kwa kuwa ranchi hiyo imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya maji kwa mifugo.

“Ni muhimu kisima hiki kikamilike kwa kuwa maji ni uchumi mtakapokuwa na maji mengi ndivyo mtakavyoweza kuwa na mifugo kulingana na uwepo wa maji, pia kuhusu wazo lenu la kuanza kufuga ng’ombe wa maziwa ni wazo zuri hususan kisima hiki kikianza kutumika na kuwa na maji ya kutosha.” Alifafanua Prof. Gabriel.

Wakiwa katika ranchi wanazozisimamia mameneja hao wamesema watatekeleza maagizo yote kwa wakati kama yalivyoelekezwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina ili ranchi hizo za Ruvu na Mkata ziweze kunufaika kupitia rasilimali ardhi na mifugo zinazomiliki.


Share:

Mkutano Wa Saba Wa Mwaka Wa Bodi Za Maji Kufanyika Tarehe 9 Hadi 11,julai ,2019




Share:

Waziri Wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga Akutana Na Mkurugenzi Mkaazi Wa Usaid Tanzania Ndg Andy Karas, Amueleza Mambo Makubwa Matano

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo - Dar es salaam
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb)  jana Tarehe 1 Julai 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Ndg Andy Karas katika Ofisi za Wizara ya Kilimo Jijini Dar es salaam.

Katika mazungumzo hayo Mhe Hasunga amemueleza Mkurugenzi huyo kuwa Wizara ya Kilimo imejipanga kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo ili kuondokana na dhana ya kilimo cha kujikimu na kuhamia katika kilimo cha kibiashara. Waziri Hasunga alisema kuwa ili kuongeza tija katika Kilimo, Wizara yake imejipanga kuimarisha utafiti.

Alisema kuwa maendeleo ya kilimo yanategemea zaidi utafiti hususani wa udongo vilevile kubaini teknolojia bora itakayo pelekea kukisogeza kilimo katika hatua kubwa ya mafanikio na kimageuzi.

Amesema kuwa pamoja na mambo mengine wizara ya kilimo pia imejipanga katika kuongeza thamani ya mazao ya kilimo kuliko kusafirisha pasina kuongeza thamani.

“Tukiongeza thamani ni wazi kuwa uchumi utapanda, lakini zaidi ajira ziataongezeka kwa wananchi, tutakuwa na Pato zuri la kigeni sambamba na utambulisho wa nchi” Alikaririwa Mhe Hasunga

Kuhusu sekta ya umwagiliaji Mhe Hasunga alisema kuwa Tanzania ina jumla ya Hekta zaidi ya Milioni 29 zinazofaa katika umwagiliaji lakini ni hekta 475,000 ndizo ambazo zimefanyiwa kazi.

“Kwa maana hiyo kuna fursa kubwa katika umwagiliaji hivyo ninyi kama wadau kadhalika natoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kuwekeza katika umwagiliaji” Alisema

Kuhusu Lishe Waziri Hasunga alisema kuwa wizara imeendelea kuweka hamasa kwa wakulima ili kuwa na lishe bora. Aliongeza kuwa watanzania wanapaswa kuwa na utamaduni wa kula vizuri ili kuondokana na magonjwa mbalimbali kama vile utapiamlo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Ndg Andy Karas ameipongeza serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa mikakati madhubuti ya kuimarisha sekta ya kilimo nchini.

Aidha, Karas amemuomba Waziri wa Kilimo kuteua watu wawili kutoka wizarani watakaokuwa kiungo muhimu baina ya serikali na miradi ya USAID sambamba na mtu atakayeratibu mikutano ya wadau wa maendeleo.


Share:

TAKUKURU Dodoma Yaibua Madudu Mradi Wa Maji Kelema, Chemba Baada Ya Kuingilia Kati Na Kuokoa Tsh.milioni 67,laki 5,elfu 42 Na Mia 600.

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa takukuru mkoa wa Dodoma imeingilia kati ujenzi wa mradi wa maji wa kijiji cha kelema kuu wilayani chemba  baada ya kubaini thamani ya fedha iliyotumika kutoendana na kazi halisi na kuokoa shilingi  Milioni  67 ,laki   5,42 elfu na mia 600.
 
Akitoa  taarifa ya robo ya nne    ya TAKUKURU  kwa waandishi wa habari ya kuanzia  Mwezi April  hadi Juni 2019, mkuu wa TAKUKURU  mkoa wa Dodoma Bw Sosthenes Kibwengo amesema kuwa hatua hiyo imefanyika ikiwa ni utekelezaji wa majukumu ya Takukuru chini ya kifungu cha saba [7] cha sheria ya kuzuia na kupamabana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 .
 
Mradi huo wa maji unagharimu kiasi cha Tsh.milioni 222,laki 9,elfu 78,mia 680 na ulipaswa kukamilika tangu mwaka 2015.

“TAKUKURU mkoa wa Dodoma  imeingilia kati mradi wa maji  Kelema Juu,baada ya kubaini fedha iliyotumika kutoendana hali halisi na kazi iliyofanyika na uwekaji mabomba ukiwa chini ya kiwango hali iliyosababisha kutotoa maji na malipo yakiwa zidifu  tofauti na makubaliano ya mradi na kuanzia tarehe 1,julai anaanza kurudia kuifanya  kazi”
 
Aidha,Bw.Kibwengo amesema TAKUKURU Mkoa wa Dodoma imefanikiwa kuokoa na kurejesha serikalini  Tsh.Milioni  11 laki 88,77elfu,mia 353  zilizolipwa bila utaratibu kama mshahara kwenye akaunti  ya mwalimu aliyekuwa amefariki.
 
Katika hatua nyinyine bw Kibwengo amesema kuwa wamefanikiwa  kumkamata Bw Gaston Meltus Francis amabaye ni mkurugenzi wa kampuni ya Global Space East Africa Limited iliyopewa kazi ya ujenzi wa kituo cha Afya cha Mima wilayani mpwapwa baada ya kubaini kampuni hiyo kulipwa isivyo halali kiasi cha shilingi milioni 86 laki nne na tano na mia mbili na tano kwa kazi ambazo hazikufanyika katika mradi huo.
                                 
Mkuu huyo wa TAKUKURU mkoa, Bw Kibwengo ameongeza kuwa TAKUKURU imefanya uchambuzi wa mifumo mbali mbali ya utendaji na utoaji wa huduma ili kubaini m  ianya na kushauri namna bora ya kuondokana nayo kwa lengo la kudhibiti vitendo vya rushwa huku pia ikitoa elimu kwa jamii  juu ya rushwa na kuzindua vilabu 39 ngazi ya shule na vyuo katika mapambano dhidi ya rushwa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.

Sanjari na hayo, TAKUKURU mkoa wa Dodoma imefuatilia na kukagua miradi 34 yenye thamani ya jumla ya shilingi bilioni 32 milioni 545 laki nne na elfu kumi na nane mia moja na kumi na sita ambapo asilimia 95.4 ya matumizi ya fedha za miradi hiyo ikionekana kufanyika vizuri.
 
Hata hivyo ,TAKUKURU Mkoa wa  Dodoma imebaini viashiria vya jinai katika miradi minnne ambapo TAKUKURU inafanya uchunguzi uhalali wa malipo   katika miradi hiyo kiasi  cha Tsh.bilioni 1 ,milioni 409 na laki 9 yaliyofanyika katika miradi hiyo ambayo ipo katika sekta  ya za ujenzi ,Afya,Elimu na Kilimo.

Katika taarifa ya TAKUKURU ya  robo za Jauari,Machi hadi Juni Mwaka huu ,TAKUKURU mkoa wa Dodoma ilipokea taarifa135 za Rushwa na Makosa mengineyo katika michanguo ifuatayo  ambapo,ardhi asilimia ,36%,serikali  za Mitaa asilimia 31%,Polisi asilimia 8%,Kilimo  asilimia 6%,mahakama na ujenzi kila moja asilimia 4%,asilimia 11% zilizobaki ni katika sekta za   ,Afya,maji,Madini,Ukusanyaji mapato huku ikiendelea na Mashauri  30 mahakamani hadi sasa.


Share:

TAIFA STARS,HARAMBEE STARS WAGONGWA TATU TATU


Sadio Mane aliifungia Senegal bao moja na kuisaidia timu yake kuchukua nafasi ya pili katika kundi C baada ya kuilaza Kenya 3-0 na kufuzu miongoni mwa timu 16 bora.
Penalti ya mshambuliji huyo wa liverpool iliokolewa na kipa Patrick Matasi wa Kenya kabla ya Senegal kufunga goli lake la kwanza kupitia Ismaila Sarr.

Mane baadaye alifunga penalti nyengine baada ya Philemon Otieno kupewa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu Sarr kunako dakika za mwisho.

Wakati huohuo kiungo wa kati wa Napoli Adam Ounas alifunga magoli mawili na kutoa pasi nzuri iliosababisha goli la tatu katika mechi yake ya kwanza katika michuano ya Afcon na kuisaidia Algeria kupata ushindi wa tatu mfululizo dhidi ya Tanzania.
Ounas alimpigia pasi murua mshambuliaji wa Leicester Islam Slimani katika bao la kwanza kabla ya ya kufunga magoili mawili katika kipindi cha kwanza kilichotawaliwa na Mbweha hao wa jangwani.

Algeria ambao walimaliza kileleni mwa kundi C walikuwa tayari wamefuzu miongoni mwa timu 16 bora baada ya kushinda mechi za kwanza mbili.

Sasa watacheza dhidi ya timu bora katika nafasi ya tatu katika raundi inayofuata.

Huku ikiwa tayari imefuzu, mkufunzi wa Algeria Djamel Belmadi alikifanyia kikosi chake cha kwanza mabadiliko tisa akimwanzisha Slimani ambaye amekosa kuchezeshwa kutokana na umahiri wa mshambuliaji Baghdad Bounedjah.
Slimani alifunga goli la kwanza na lake la kimataifa la 27 baada ya dakika 30 katika mechi yake ya 31 kufuatia pasi nzuri kutoka kwa Ounas.

Na katika mechi dhidi ya Senegal na Kenya , mabingwa hao wa afrika magharibi sasa watachuana na Uganda tarehe 5 mwezi Julai.

Kenya inaweza ikafuzu kama timu ya tatu bora ikitegemea matokeo katika mechi ya mwisho katika kundi E and F.

Hatahivyo matokeo ya Jumatatu yanamaanisha kwamba DR Congo inaweza kufuzu kutoka kundi A ikiwa na goli moja zaidi.
CHANZO.BBC SWAHILI
Share:

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE



Kocha wa United, Ole Gunnar Solskjaer amewaambia wakuu wa klabu hiyo kumsajili kiungo wa kati wa Newcastle Muingereza Sean Longstaff, 21, kwa mshahara wa pauni milioni 21 kwa wiki. (Star)
Barcelona wako tayari kulipa euro milioni 100 ya kumwezesha mshambuliaji wa Inter Milan Muargentina Lautaro Martinez, 21 kuondoka klabu hiyo kabla mkataba wake kukamilika. (Corriere dello Sport - in Italian)

Ofa ya Manchester United ya £31m ya kumnunua kiungo wa kati wa Ureno Bruno Fernandes, 24, imekataliwa na Sporting Lisbon. (Gazzetta dello Sport, via Express)

Ni rasmi sasa Meneja wa Derby County Frank Lampard amerejea Chelsea baada ya mchezaji huyo wa zamani wa blues kutia saini mkataba pauni milioni 4 kwa mwaka. (Mail)Bruno Fernandes

Kocha wa zamani wa Newcastle Rafael Benitez amekubali kujiunga klabu ya Uchina ya Dalian Yifang kwa mkataba wa thamani ya euro milioni 12 kwa mwaka baada ya kuondoka St James Park. (Sky Sports)

Rams wanajiandaa kufanya mazungumzo na kiungo wa kati wa zamani wa Uholanzi Phillip Cocu wiki hii kabla ya Lampard kuondoka.

Cocu alitupwa nje na kocha wa Fenerbahce mwezi Octoba. (Telegraph)

Kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 26, amekuwa akifanya mazoezi mjini New York licha ya wachezaji wenzake kurejea kambini kwa mazoezi ya kabla ya msimu mpya kuanza. (Sun)
Paul Pogba

Arsenal wanashauriana na mshambuliaji wa Algeria, Yacine Brahimi 29 ambaye yuko huru na kujiunga na klabu nyinhine baada ya kuhama Porto. (Sky Sports)

Gunners pia wamepewa nafasi ya kusaini mshambuliaji wa Lyon na Ufaransa Nabil Fekir - kwa uero milioni 30. (Mirror)

Winga wa Manchester City Mjerumani Leroy Sane ameangaziwa katika uzinduzi wa jezi za msimu wa mwaka 2019-20, licha ya tetesi kuwa Bayern Munich wamekuwa wakimnyatia nyota huyo wa miaka 23. (Express)Leroy Sane aliisaidia Ujerumani kufuzu kwa nusu fainali ya michuano u a kombe la Euro 2016

Crystal Palace wanamtaka mlinzi wa Arsenal Muingereza Carl Jenkinson, 27, kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na mlinzi Aaron Wan-Bissaka, ambaye amejiunga na Manchester United. (Sun)

Gunners wanajiandaa kuweka dau la pauni milioni 12 kumnunua mshambuliaji wa Hull City wa miaka 22-year- Muingereza Jarrod Bowen. (Sun)

Mshambuliaji wa Uholanzi Hossein Zamani, 16, amevifahamisha villabu vya Manchester United, Manchester City na AC Milan kuwa aAjax. (Mail)

CHANZO.BBC SWAHILI
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne 2 July





















Share:

Monday 1 July 2019

Tanzania na Nchi ya Falme za Kiarabu Zakubaliana kuimarisha hali ya usalama katika nchi za Somalia na Sudan.

Tanzania na Nchi ya Falme za Kiarabu zimekubaliana kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi ikiwa ni pamoja na kushirikiana katika masuala ya usalama wa eneo la Ghuba na bahari ya Hindi pia kusaidia kuimarisha hali ya usalama katika nchi za Somalia na Sudan.

Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi alipomtembelea na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan.

Katika Mazungumzo hayo wawili hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha udugu wa muda mrefu baina ya mataifa hayo mawili ikiwa ni pamoja na kufufua mazungumzo ya Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) ambayo kwa mara ya mwisho yalifanyika katika Mji wa Abu Dhabikatika Umoja wa Falme za Kiarabu ili kufufua na kutekeleza makubaliano ikiwa ni pamoja na kuangalia fursa za kiuchumi kwa faida ya pande zote mbili.

Akizungumza mara baada ya mazungumzo hayo Waziri Palamgamba John Kabudi amesema pamoja na masuala mbalimbali waliyokubaliana pia Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan ameahidi kufanya mazungumzo na Ubalozi wa Falme za Kiarabu uliopo Nchini Tanzania ili kuharakisha matayarisho ya Ubalozi huo kuhamia Dodoma baada ya serikali ya Tanzania kuupatia ubalozi huo eneo la kujenga ubalozi wa Nchi hiyo mjini Dodoma bure.

Waziri Kabudi ameongeza kuwa mazungumzo hayo yamekuwa ya manufaa kwa pande zote mbili na kwamba yataendelea kuimarisha mahusiano baina ya Nchi hizo mbili ikiwa ni pamoja na kufungua fursa za kibiashara kwa ajili ya maendeleo ya mataifa hayo.

Katika hatua nyingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof Palamagamba John Kabudi akizungumza wakati akihitimisha ziara yake Nchini China,amesema ziara hiyo imekuwa ya manufaa kiuchumi kwa Tanzania ambapo tayari wawekezaji takribani 150 wanatarajiwa kuwasili nchini Tanzania kwa nia ya kuangalia maeneo mbalimbali ya uwekezaji mapema mwezi septemba wakitanguliwa na ujumbe wa watu 10 mwezi Julai 2019,hii ikiwa ni kipindi kifupi sana mara baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuhudhuria mkutano wa kwanza wa maonesho ya uchumi na biashara kati ya China na Afrika uliofanyika katika mji wa Chanshang katika jimbo la Hunan,Nchini China.

Aidha ametanabaisha kuwa tayari wamepatikana wawekezaji wanaotaka kujenga nyumba ya kulala wageni yenye vyumba mia tatu katika mji wa Karatu ulioko mkoani Manyara kwa nia ya kuhamasisha watalii hususani kutoka China ambao wanatarajiwa kuongezeka maradufu kufuatia hatua ya Tanzania kuweka msisitizo katika kutangaza vivutio vyake vya Utalii.

Pia Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Beijing kimekubali ombi la Waziri Kabudi la kutaka kuongeza idadi ya wanafunzi watakaokwenda kusoma chuoni hapo kutoka 20 hadi kufikia idadi 40 nafasi zitakazotolewa kwa ufadhili wa chuo hicho kila mwaka ili kuandaa nguvu kazi ya kutosha wakati Tanzania ikijiandaa kuingia katika uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.


Share:

Katibu Mkuu CCM Atoa ONYO Kwa Viongozi Wadokozi wa Mali za Chama Hicho

Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally, amekemea viongozi wenye uchu na mali za chama, akiagiza waondolewe ili kuepusha migogoro isiyokuwa na tija ndani ya chama hicho.

“Msiwavumilie hawa viongozi wenye uchu na mali za chama. Wafukuzeni wote. CCM haina uhaba wa wanachama na kila mwanachama ana haki ya kuongoza. Hizi tabia za kulindana na kukingiana vifua ndizo zilizotufikisha hapa,” alisema.

Bashiru ameyasema hayo katika mkutano wa wanachama wa Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam jana.

Dk. Bashiru alisema kuna taarifa za kuwepo migogoro ya viongozi kugombania mali za chama kama ilivyo katika Kata ya Sinza, hasa Sinza B, suala ambalo linatakiwa kushughulikiwa.

Aliwataka wanachama na viongozi kuhakikisha wanatunza mali za chama na kuzilinda, pia kufuata utaratibu mpya uliowekwa, ambao unahitaji malipo yote yatumie mfumo rasmi tofauti na ilivyokuwa zamani.

“Kuna baadhi ya viongozi wanavuruga mfumo, hawalipi kwa kutumia ‘control number’, bado wanaendelea kupokea fedha taslimu na kuzipangia matumizi kiholela. Wengine wanasema mabanda hayana watu kumbe yana watu, wanafanya kama mali yao, hawa hawavumiliki,” alisema.

Alieleza kuwa kwa sasa hawatarajii kupokea fedha kutoka kwa matajiri, na kwamba chama kitaendelea kutumia rasilimali na miradi yake kujipatia kipato kujiendesha.


Share:

Zitto Kabwe Apasua Jipu Kutekwa Kwa Msaidizi Wake.

Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT- Wazalendo), Zitto Kabwe ameitaka Serikali ya Tanzania kuangalia kwa uzito suala la kutekwa kwa raia wa Kenya anayeishi Tanzania, Raphael Ongagi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Julai 1, 2019 jijini Dar es Salaam, Zitto amesema masuala ya utekaji yamekuwa yakileta taswira mbaya kwa nchi ya Tanzania.

Amesema Tanzania haipaswi kuwa na taswira hiyo kwa mataifa mengine hasa nchi jirani ambazo tumekuwa tukishirikiana nazo katika mambo mengi.

Kutokana na hali hiyo, Zitto amewataka watekaji hao kumwachia huru kwani hana taarifa zake wanazozihitaji.

Raia huyo wa Kenya anadaiwa kutekwa na watu wasiojulikana jijini Dar es Salaam, wakati akitoka shuleni kwa watoto wake kwenye kikao cha wazazi.

“Siku mbili baada ya Raphael kutekwa, akaunti zangu za mitandao ya kijamii zilidukuliwa na Raphael alikuwa na password zangu, hata hivyo hana taarifa zozote juu yangu hivyo ninawaambia watekaji hawawezi kupata taarifa zozote juu yangu kutoka kwa Raphael kwasababu watamtesa bure na hana taatifa ambazo anaweza kuwapa.

‪“Naamini wananisikia, hivyo wamuachie na kama kuna taarifa zozote wanazoona zina makosa waniite mwenyewe kwa taratibu za serikali mimi nitawapa hizo taarifa,” amesema Zitto

Amesema kuna watu wamefikia kusema rasilimali fedha zake zote zinapita kwa Raphael ambapo amesema hahusiki na chochote ni vyema wakamuita mwenyewe kama hilo ndiyo dhumuni lao.

Akielezea namna alivyokutana na Raphael, Zitto amesema ni raia wa Kenya ambaye tangu mwaka 2002 alikuja nchini na alipata marafiki wengi wa Tanzania na hata kufunga ndoa na Mtanzania.

“‪Baada ya kuamua kuingia kwenye biashara aliendelea kuwa mtu wangu wa karibu na mpaka anatekwa tumekuwa bado ni watu wa karibu hakuwa anajihusisha na siasa kwa namna yoyote,” amesema Zitto.

Hata hivyo, Zitto amesema anawasihi watekaji hao wamuache Raphael mahali kisha wao watakwenda kumchukua.


Share:

Fahamu Chanzo Halisi cha Kupungukiwa Nguvu za Kiume

Unafahamu kwa kina tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume na  maumbile ya kiume kusinyaa?

Wanaume wengi kwa sasa wanasumbuliwa na tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile  kuwa mafupi na wengi wao huamua kutafuta tiba ili waweze kujilejeshea nguvu zao za asili bila kujua ni nini chazo cha hilo tatizo 

Tambua kuwa hakuna dawa ya kuongeza maumbile ya kiume  kama  ulikuwa mdogo  tangu unazaliwa, labda kama tatizo limeazia ukubwani kwa kujichua ( kupiga punyeto)  au kutokana na magonjwa 

Pia hakuna dawa ya kuongeza nguvu za kiume kama tatizo umezaliwa nalo bali zipo tiba za kutibu na ukapona matatizo hayo kama yameanzia  ukubwani kutokana na sababu zifatazo ;
1,Unene kupita kiasi 
2.Kuvaa nguo za kubana 
3.Magonjwa ya moyo,kisukar,presha,vidonda vya tumbo,ngiri,tumbo kuunguruma na kujaa gesi,kupiga punyeto,Msongo wa mawazo.

Haya ndo mambo makuu yanayosababisha tatizo hilo. kwa ushauri zaidi , piga simu 0683645920


Share:

Waziri wa Nishati: Tumieni Umeme Kuanzisha Miradi Ya Maendeleo

Na Veronica Simba - Chato
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amewaasa wananchi wa Kitongoji cha Mwamagili, Wilaya ya Chato, mkoani Geita kutumia umeme aliowawashia rasmi jana, Juni 30, 2019 kwa kuanzisha miradi mbalimbali ya kimaendeleo.

Akizungumza na wananchi hao muda mfupi kabla ya kuwasha umeme katika nyumba ya mkazi wa kitongoji hicho, Kashonele Kagodoro, Dkt. Kalemani aliwaambia endapo watautumia ipasavyo, hali zao za maisha zitaboreka zaidi.

“Umeme huu siyo kwa ajili ya kuwasha taa peke yake. Anzisheni miradi mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo mashine za kukoboa na kusaga nafaka, saluni za kike na kiume na miradi mingine mbalimbali ili kuinua kipato chenu hivyo kuboresha maisha yenu.”

Aidha, Waziri Kalemani ambaye pia ni Mbunge wa eneo hilo (Chato), aligawa vifaa vya Umeme Tayari (UMETA) kwa nyumba zote 38 za kitongoji hicho, ambazo zilikuwa bado hazijaunganishiwa umeme ikiwa ni sehemu ya kuwahamasisha wananchi husika kulipia gharama ndogo ya shilingi 27,000 tu ili waunganishiwe nishati hiyo.

“Kwa kutumia kifaa hiki cha UMETA, mtaepuka gharama za kutandaza nyaya katika nyumba zenu. Niwaombe na kuwahamasisha muendelee kulipia kwa sababu bei ya kuunganishiwa umeme ni ndogo sana; shilingi 27,000 tu,” asisitiza Waziri.

Katika hatua nyingine, Waziri amelipia gharama za kuunganisha umeme katika Kanisa lililopo eneo hilo, ambayo pia ni sehemu ya kuhamasisha viongozi wa taasisi mbalimbali za umma kulipia gharama za umeme ili ziunganishwe.

Wananchi kadhaa waliopata fursa ya kueleza maoni yao mbele ya Waziri Kalemani, walipongeza jitihada za Serikali katika kuwapelekea nishati ya umeme.

“Hii ni ndoto kwangu. Sikutegemea. Tangu nizaliwe nilikuwa nikiona umeme maeneo ya mijini nilikowahi kutembelea. Sikuwahi kuwaza kuwa iko siku umeme utawashwa kijijini kwetu, tena katika nyumba yangu,” alisema Kagodolo.

Waziri Kalemani yuko Chato kwa ziara ya kazi.


Share:

Jinsi ya kukabiliana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume

Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunakuwa katika uwanja mpana zaidi wa tafakari za kibaiolojia na kisaikolojia walizonazo wanaume.

Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo sehemu kuu tatu zinaweza kabisa kukidhi mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili linavyowasumbua wanaume wengi duniani.

Sehemu kubwa ya malalamiko ya wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi maeneo matatu ambayo ni kukosa msisimko, kushindwa kurudia tendo na kukosa kabisa nguvu, huku kufika kileleni mapema kukihusishwa pia kama pacha wa janga hili ambalo linawasumbua zaidi wanaume.
 
Sababu zinazosababisha tatizo la nguvu za kiume zinawekwa katika makundi mawili.
*Matatizo ya kiafya ya mwili (organic causes).
*Matatizo ya kisaikolojia ( Psychological cause).
 
Matatizo ya kiafya:
  1. Magonjwa ya kisukari, (diabetes mellitus).
  2. Ugonjwa wa presha (blood pressure).
  3. Matatizo ya tezi dume (kama mtu amewahifanyiwa operation) (prostatectomy surgery),
  4. Upungufu au mvurugiko wa uzalishaji Homoni za uzazi (hormonal insufficiencies /hypogonadism).
  5. Athari za matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
Matatizo haya kwa pamoja hupelekea mishipa ya damu kuziba na mwishowe misuli inakosa nguvu za kuweza kusimama na hatimae uume husinyaa.
 
Tatizo la Kisaikolojia(Psychological reasons)
Ukweli wa mambo ulioibuliwa na wanasaikolojia umebaini wale wote wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana nguvu iwe ya kufika kileleni mapema, kutokuwa na msisimko na kushindwa kurudia tendo wamekosa maarifa tu ya kufahamu na hawaijui miili yao na wanaishi kwa kusikia zaidi ya kujitambua.

Watu hao kiuhalisia wanakabiliwa  na matatizo ya kimawazo, kama vile migogoro katika mahusiano, matatizo ya kimaisha na mambo mengine
 
Dalili za tatizo hili
  1. Kushindwa kusimamisha uume mara kwa mara,
  2.  Uume kulala(kusinyaa) katikati ya tendo la ndoa.
  3.  kushindwa kusimamisha ipasavyo.
  4. Kufika  haraka mara baada ya kuanza
  5. kujamiiana.
  6.  Maumivu ya misuli ya uume wakati wa tendo la ndoa.

Magonjwa yanayosababisha tatizo hili:
*kisukari (diabetes)
*presha (blood pressure)
*matatizo yafigo (kidney disorders)
*matatizo ya kisaikologia(psychological cause).
* upungufu wa homoni za uzazi (hormonal insufficiencies).
* Matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
* Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe kupita kiasi.
* matatizo ya tezi dume.

Matatizo haya yote Yanatibika kwa dawa. Wasiliana Nami kwa msaada zaidi: 0620510598 au 0759208637

 


Share:

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) yaanza kupokea maombi ya mikopo

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), leo inafungua dirisha la uombaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020.

Bodi hiyo imeboresha utoaji elimu kwa waombaji wapya pamoja na kutembelea kambi za jeshi walizopo wanafunzi kuwapa maelekezo ya kujaza fomu kabla ya kurejea majumbani kuomba mikopo.

Aidha, mwaka huu, wamefanya maboresho katika muongozo wa utoaji mikopo kwa umri wa waombaji waliopo vyuoni kwa kuongeza umri mpaka miaka 35 badala ya 33 na wanaruhusiwa waliomaliza miaka mitano iliyopita na si miaka mitatu.

Ofisa Mawasiliano Mwandamizi wa bodi hiyo,Veneranda Malima amesema hayo katika banda la bodi hiyo kwenye viwanja vya Maonesho vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam maarufu Sabasaba.

Alisema katika maonesho hayo wamesogeza huduma kwa jamii na wadau kwa kutoa taarifa za wanaorejesha mikopo, wanaotaka kujua salio na wanaotaka kulipa huku wanafunzi wanaotaka kufahamu kuhusu fedha zao za mafunzo ya vitendo watahudumiwa.

Malima alisema lengo la uboreshaji huo ni kutoa nafasi kwa wanufaika wengi kupata mikopo hasa kwa waliopata matatizo kama ya kufiwa na wazazi hivyo kuwa na uhitaji.


Share:

Afcon 2019: Taifa Stars Kuvaana na Algeria Leo

Timu  ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, leo inatarajia kushuka uwanjani kucheza na Algeria katika mchezo wa tatu wa Kundi C wa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon 2019), inayoendelea jijini Cairo nchini Misri.

Michuano hiyo ambayo ilianza Juni 21 na kutarajiwa kumalizika Julai 19, mwaka huu, nchini humo, timu ya Tanzania haina matumaini ya kutinga hatua ya 16 bora, hata kama itashinda dhidi ya Algeria, baada ya kuanza vibaya.

Hilo linatokana na Taifa Stars kupoteza michezo miwili dhidi ya Senegal na Kenya, ambayo ilifungwa mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza dhidi ya Senegal, kisha kupigwa mabao 3-2 na jirani zao Kenya.

Kwa matokeo hayo, mchezo wa leo kwa Taifa Stars utakuwa wa  kukamilisha ratiba ya michuano hiyo  kutokana na kutofanya vizuri michezo yake miwili.

Taifa Stars iliyofanikiwa kufuzu michuano hiyo, baada ya kuifunga Uganda  mabao 3-0 katika mchezo wa marudiano uliochezwa Machi 24, mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, imeonekana kushindwa kuhimili mikikimikiki ya Afcon .

Matokeo hayo yaliifanya Tanzania kumaliza nafasi ya pili Kwa kutoka Kundi L, kutokana na pointi,  nyuma ya Uganda aliongoza kundi hilo kwa pointi 13, Lesotho ilimaliza nafasi ya tatu kutokana na pointi sita na Cape Verde ilishika mkia kwa  pointi tano.   

Historia ya timu ya Tanzania  kufanya vibaya Afcon inajirudia baada ya mwaka 1980 nchini Nigeria kushika mkia katika Kundi A, lililoundwa na mwenyeji, Misri na Ivory Coast.


Share:

WANAUME WAPEWA BURE DAWA NGUVU ZA KIUME

IMEELEZWA kuwa asilimia 85 ya upungufu wa nguvu za kiume kwa wanaume unatokana na magonjwa ya moyo na kisukari, hivyo Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) imeamua kuleta dawa za kurejesha nguvu hizo wakati wanaume wakiendelea na matibabu ya vishawishi.


Dawa hizo zinatolewa katika Viwanja vya Maonesho vya Mwalimu Julius Nyerere vilivyopo Barabara ya Kilwa katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, ambapo taasisi hiyo katika banda lao wanatoa huduma bure ya upimaji, ushauri na dawa.

Akizungumza katika viwanja hivyo, Daktari bingwa na Mkuu wa Idara ya Utafiti na Mafunzo wa taasisi hiyo, Dk Pedro Pallangyo aliliambia gazeti hili kuwa wanatoa huduma za vipimo bure vya urefu, uzito, mapigo ya moyo, shinikizo la damu, sukari, kipimo cha umeme wa moyo (ECG), na kipimo cha utendaji kazi wa moyo (ECHO).

Alisema pia kuna mtaalamu wa lishe anayetoa ushauri bure wa lishe na ushauri na baada ya vipimo, watakaobainika kuwa na magonjwa ya moyo na magonjwa ambatano ya kifua, ganzi, shinikizo la damu na upungufu wa nguvu za kiume watapatiwa dawa.

“Kwa kiwango kikubwa upun- gufu wa nguvu za kiume unatokana na magonjwa ya moyo na kisukari huku chakula kikisababisha kwa kiwango kidogo cha asilimia tano, hivyo kwa wenye upungufu wa nguvu tuna dawa zitakazowasaidia kwa saa 24 hadi 48 wakati wakiendelea na matibabu ya chanzo cha ugonjwa,”alisema Dk Pedro.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger